Ona video zinazopatikana

Biblia Inafundisha Nini Kuhusu Kusema Katika Luga?

Biblia Inafundisha Nini Kuhusu Kusema Katika Luga?

Jibu ya Biblia

 ‘Kusema katika luga’ ni uwezo wa kimuujiza wenye Wakristo fulani wa kwanza-kwanza walikuwa nao wenye uliwasaidia waseme luga yenye hawayajifunzaka. (Matendo 10:46) Kila mutu mwenye alijua ile luga alimuelewa ule mwenye alikuwa anaisema. (Matendo 2:4-8) Kusema katika luga iko kati ya zawadi za roho takatifu zenye Mungu alipatia Wakristo fulani wa wakati ya mitume.​—Waebrania 2:4; 1 Wakorinto 12:4, 30.

 Kusema katika luga kulianzia wapi na wakati gani?

 Wakristo walisema katika luga kwa mara ya kwanza mu Yerusalemu asubui ya Sikukuu ya Kiyahudi ya Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y. Wanafunzi 120 hivi wa Yesu walikuwa wamekusanyika pamoya na “wote wakajazwa roho takatifu na wakaanza kusema katika luga mbalimbali.” (Matendo 1:15; 2:1-4) Watu wengi “kutoka kila taifa chini ya mbingu” wakakusanyika na “kila mumoja aliwasikia wanasema katika luga yake mwenyewe.”​—Matendo 2:5, 6.

 Kusudi ya kusema katika luga ilikuwa nini?

  1.   Kuonyesha kama Mungu alikuwa anaunga mukono Wakristo. Zamani, Mungu alifanya miujiza ili kuonyesha kama alikuwa anaunga mukono watu waaminifu sawa vile Musa. (Kutoka 4:1-9, 29-31; Hesabu 17:10) Kusema katika luga kulikuwa pia na kusudi ya vile, ni kusema, kuonyesha kama Mungu alikuwa naunga mukono kutaniko ya Kikristo yenye ilikuwa imetoka kuanzishwa. Mutume Paulo aliandika hivi: “Luga haziko alama kwa ajili ya wenye kuamini lakini ni kwa ajili ya wenye hawaamini.”​—1 Wakorinto 14:22.

  2.   Kusaidia Wakristo waweze kutoa ushahidi. Wale wenye walisikiliza wanafunzi wa Yesu siku ya Pentekoste walisema hivi: “Tunawasikia wakisema katika luga zetu juu ya mambo makubwa ya Mungu.” (Matendo 2:11) Kwa hiyo, kusudi ingine ya kusema katika luga ilikuwa kusaidia Wakristo “kutoa ushahidi kamili” na ‘kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote,’ kama vile Yesu alikuwa amewaagiza. (Matendo 10:42; Matayo 28:19) Ile siku, watu karibu 3 000 wenye waliona namna wanafunzi wa Yesu wanazungumuza katika luga na kusikiliza ushahidi wenye walikuwa wanatoa wakakuwa wanafunzi.​—Matendo 2:41.

 Kusema katika luga kulipaswa kuendelea?

 Hapana. Zawadi za roho takatifu, kutia ndani zawadi ya kusema katika luga, zilikuwa za wakati fulani tu. Biblia ilisemaka hivi: “Kama kuko zawadi za unabii, zitaondolewa; kama kuko luga, zitaisha.”​—1 Wakorinto 13:8.

 Kusema katika luga kuliisha wakati gani?

 Kwa kawaida, mitume njo walikuwa napatia Wakristo wengine zawadi za roho takatifu. Mara mingi mitume waliweka mikono yao juu ya waamini wenzao ili wazipate. (Matendo 8:18; 10:44-46) Inaonekana kama wale wenye walipokea zawadi za roho kutoka kwa mitume hawakukuwa na uwezo wa kuzipatia wengine. (Matendo 8:5-7, 14-17) Kwa mufano, ofisa wa serikali anaweza kupatia shofere karatasi ya kumuruhusu kutembeza gari, lakini ule shofere hana mamlaka ya kisheria ya kupatia mutu mwingine karatasi ya kumuruhusu kutembeza gari. Inaonekana kusema katika luga kuliisha wakati mitume na wale wenye walikuwa wanapata ile zawadi kutoka kwao walikufa.

 Inawezekana kusema katika luga leo?

 Ni wazi kama zawadi ya kusema katika luga iliisha karibu na mwisho wa karne ya kwanza K.K.Y. Leo, hakuna mutu mwenye anaweza kusema kama anasemaka katika luga kwa nguvu ya Mungu. *

 Nini njo inaweza kutambulisha Wakristo wa kweli?

 Yesu alisema kama upendo njo ungetambulisha wanafunzi wake. (Yohana 13:34, 35) Vilevile, mutume Paulo alifundisha kama upendo njo sifa yenye ingetambulisha Wakristo wa kweli. (1 Wakorinto 13:1, 8) Alionyesha kama roho ya Mungu ingefanya Wakristo wakuwe na sifa zenye kwa ujumla zinaitwa “tunda la roho,” na sifa ya kwanza ni upendo.​—Wagalatia 5:22, 23.