Ona video zinazopatikana

Zambi Ni Nini?

Zambi Ni Nini?

Jibu ya Biblia

 Zambi ni tendo, hisia, ao wazo yenye inapingana na kanuni za Mungu. Mutu anafanya zambi wakati anavunja sheria ya Mungu, kwa kufanya mambo ya mubaya yenye Mungu hakubali. (1 Yohana 3:4; 5:17) Biblia inasema pia kama ni zambi kukosa kufanya mambo yenye tunajua kama ni ya muzuri.​—Yakobo 4:17.

 Mu luga zenye zilitumiwa juu ya kuandika Biblia, maneno yenye kutafsiriwa zambi inamaanisha “kutokufikia kusudi,” ao kutokufikia kitu yenye mutu alikuwa navizia. Kwa mufano, mu Israeli ya zamani mulikuwa kikundi ya maaskari wenye walikuwa najua sana kurusha majiwe, na walikuwa wanalenga kitu fulani “bila kukosea.” Kama maneno “bila kukosea” inatafsiriwa neno kwa neno, inaweza kuwa hivi: “Bila kufanya zambi.” (Waamuzi 20:16) Kwa hiyo, kufanya zambi ni kukosa kufikia kusudi ya kanuni kamilifu za Mungu, ao kushindwa kuzifuata.

 Juu Mungu njo alituumba, iko na haki ya kututilia kanuni zenye tunapaswa kufuata. (Ufunuo 4:11) Tutatoa hesabu mbele yake juu ya matendo yetu.​—Waroma 14:12.

Inawezekana kabisa kuepuka kufanya zambi?

 Hapana. Biblia inasema kama “wote wamefanya zambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.” (Waroma 3:23; 1 Wafalme 8:46; Muhubiri 7:20; 1 Yohana 1:8) Juu ya nini?

 Ku mwanzo, wanadamu wa kwanza, Adamu na Eva, hawakukuwa na zambi, juu wakati waliumbwa, walikuwa wakamilifu na waliumbwa kwa mufano wa Mungu. (Mwanzo 1:27) Lakini walipoteza ukamilifu wakati walikosa kumutii Mungu. (Mwanzo3:5, 6, 17-​19) Wakati walizala watoto, waliwapitishia zambi na hali ya kutokamilika. (Waroma 5:12) Njo maana Mufalme Daudi wa Israeli alisema hivi: “Nilizaliwa nikiwa na hatia ya kosa.”​—Zaburi 51:5.

Zambi fulani ni kubwa kuliko zingine?

 Ndiyo. Kwa mufano, Biblia inasema kama watu wa Sodoma ya zamani walikuwa “waovu, na walikuwa wanatenda zambi nzito” na zambi zao zilikuwa “nzito sana.” (Mwanzo 13:13; 18:20) Tuone mambo tatu yenye inatusaidia kujua ukubwa wa zambi.

  1.   Uzito. Biblia inatuambia tuepuke zambi nzito sawa vile kufanya uasherati, kuabudu sanamu, kuiba, kulewa, kunyanganya, kuua, na kupashana habari na pepo wachafu. (1 Wakorinto 6:9-​11; Ufunuo 21:8) Biblia inaonyesha kama zile zambi ziko tofauti na zambi zenye mutu anafanyaka bila kufikiri ao bila kukusudia, kwa mufano, maneno ao matendo yenye kuumiza wengine. (Mezali 12:18; Waefeso 4:31, 32) Lakini Biblia inatutia moyo tusizarau zile zambi zenye tunafanyaka bila kufikiri ao bila kukusudia juu zinaweza kutufikisha ku zambi nzito.​—Matayo 5:27, 28.

  2.   Nia. Watu fulani wanafanyaka zambi juu hawajue sheria za Mungu. (Matendo 17:30; 1 Timoteo 1:13) Biblia haiseme kama, ikiwa mutu anafanya zambi na hajue, ni kusema hana kosa. Lakini inaonyesha kama mutu mwenye anafanya zambi bila kujua iko tofauti na ule mwenye anavunja sheria ya Mungu kimakusudi. (Hesabu 15:30, 31) Watu wenye kufanya zambi kimakusudi wanachochewa na “moyo muovu.”​—Yeremia 16:12.

  3.   Ni mara ngapi zambi imefanywa. Tena Biblia inaonyesha kama kuko tofauti kati ya mutu mwenye anafanya zambi mara moya na mutu mwenye anafanya zambi kwa wakati murefu. (1 Yohana 3:4-8) Mungu atahukumu wale wenye ‘wanazoea kutenda zambi kimakusudi,’ hata kisha kujua mambo yenye kuwa sawa.​—Waebrania 10:26, 27.

 Wale wenye wamefanya zambi nzito wanaweza kusumbuliwa sana na zamiri kwa sababu ya zambi zenye walifanya. Kwa mufano, Mufalme Daudi aliandika hivi: “Kwa maana makosa yangu yamekuwa mengi sana juu ya kichwa changu; kama muzigo muzito, ni mengi sana siwezi kuyabeba.” (Zaburi 38:4) Lakini Biblia iko na hii maneno yenye kufariji: “Mutu muovu aache njia yake na mutu mubaya mawazo yake; na amurudilie Yehova, mwenye atamuonyesha rehema, kwa Mungu wetu, kwa maana atasamehe kwa njia kubwa.”​—Isaya 55:7.