Ona video zinazopatikana

KITU HIKI KILIJIFANYA CHENYEWE?

Uwezo wa Imbwa wa Kunusa

Uwezo wa Imbwa wa Kunusa

Watu wenye kufanya uchunguzi wanasema kama imbwa wanaweza kutumia uwezo wao wa kunusa ili kujua ikiwa imbwa mwingine iko na miaka ngapi, ikiwa ni imbwa dume ao dike, na ikiwa iko na kasirani ao hapana. Imbwa wanaweza hata kuzoezwa ili watambue harufu ya mabombe na dawa za kulewesha. Wanadamu wanatumia zaidi sana macho yao juu ya kujua mambo yenye kuwazunguka, lakini imbwa wanatumia uwezo wao wa kunusa. Imbwa wanaonaka na pua yao.

Fikiria hili: Uwezo wa imbwa wa kunusa unapita uwezo wetu mara maelfu. Kulingana na shirika moja la Amerika (National Institute of Standards and Technology), imbwa “anaweza kusikia harufu ya sehemu za kidogo-kidogo za vitu vyenye vimegawanywa mara miliare moja. Ni kama vile kusikia utamu wa sukari kidogo, ni kusema, sehemu moja ya ine (1/4) ya sukari yenye kuenea kwenye kijiko cha chai, yenye wamemwanga mu maji ya kisima cha olimpiki.”

Juu ya nini uwezo wa kunusa wa imbwa unapita sana uwezo wetu wa kunusa?

  • Pua ya imbwa iko na umaji-maji, kwa hiyo anaweza kuvuta harufu kwa vyepesi.

  • Pua ya imbwa iko na njia mbili za kupitisha hewa, moja ni ya kupumua, na ingine ni ya kunusa. Wakati imbwa anavuta hewa, hewa inaingia mu sehemu ya pua yenye kuwa na vitu vya kutambua harufu.

  • Sehemu ya pua ya imbwa yenye inamusaidia kusikia harufu iko na santimetre 130 za muraba ao zaidi, lakini ya mwanadamu iko tu na santimetre 5 za muraba.

  • Katika pua ya imbwa, chembe zenye kuvuta harufu zinaweza kuwa za mingi mara 50 kupita zetu sisi wanadamu.

Ile yote inamusaidia imbwa atambue sehemu mbalimbali za harufu yenye iko nguvu kutambua. Kwa mufano, sisi wanadamu tunaweza kusikia harufu ya supu, lakini kulingana na watu fulani wenye elimu, imbwa anaweza kutambua kila kitu chenye kilitiwa mu ile supu.

Watu fulani wenye kufanya uchunguzi ku masomo moja ya kutafuta habari juu ya kansere, wanasema kama ubongo wa imbwa na pua yake vyenye vinatumika pamoja ni “moja kati ya vyombo vya ajabu zaidi vya kutambua harufu ku dunia.” Wanasayansi wako wanatengeneza “pua” za kielektroniki zenye zinaweza kutambua mabombe, vitu vyenye serikali inakataza kuuza ao kuuzisha, na magonjwa, kutia ndani kansere.

Unawaza namna gani? Uwezo wa imbwa wa kunusa ulijitokeza wenyewe? Ao uliumbwa?