Kulingana na Yohana 14:1-31

  • Yesu ndiye njia pekee ya kumukaribia Baba (1-14)

    • ‘Mimi ndiye njia, kweli, na uzima’ (6)

  • Yesu anaahidi roho takatifu (15-31)

    • “Baba ni mukubwa kuliko mimi” (28)

14  “Mioyo yenu isivurugike.+ Mukuwe na imani katika Mungu;+ mukuwe na imani katika mimi pia.  Katika nyumba ya Baba yangu kuko makao mengi. Haingekuwa vile, ningewaambia ninyi, kwa maana ninaenda kuwatayarishia ninyi nafasi.+  Pia, kama ninaenda na kuwatayarishia ninyi nafasi, nitakuja tena na nitawapokea ninyi katika nyumba yangu mwenyewe, ili kwenye niko, ninyi pia mukuwe pale.+  Na kule ninaenda, ninyi munajua njia.”  Tomasi+ akamuambia: “Bwa­na, sisi hatujue kwenye unaenda. Namna gani tunaweza kujua njia?”  Yesu akamuambia: “Mimi ndiye njia+ na kweli+ na uzima.+ Hakuna mwenye anakuja kwa Baba isipokuwa kupitia mimi.+  Kama mungekuwa mumenijua, mungekuwa mumemujua Baba yangu pia; tangu wakati huu na kuendelea ninyi mumemujua na mumemuona.”+  Filipo akamuambia: “Bwana, utuonyeshe Baba, na hilo linatutosha.”  Yesu akamuambia: “Je, hata kisha mimi kuwa pamoja na ninyi kwa wakati murefu vile, Filipo, bado haujanijua? Kila mutu mwenye ameniona mimi amemuona Baba pia.+ Namna gani unasema, ‘Utuonyeshe Baba’? 10  Je, hauamini kwamba mimi niko katika umoja na Baba, na Baba iko* katika umoja na mimi?+ Mambo yenye ninawaambia ninyi, siyaseme kwa kujitungia mimi mwenyewe,+ lakini Baba mwenye anakaa katika umoja na mimi anafanya kazi zake. 11  Muniamini kwamba niko katika umoja na Baba na Baba iko* katika umoja na mimi; kama haiko vile, muamini kwa sababu ya kazi zenyewe.+ 12  Kwa kweli kabisa ninawaambia ninyi, kila mutu mwenye ananiamini atafanya pia kazi zenye mimi ninafanya; na atafanya kazi kubwa kuliko hizi,+ kwa sababu ninaenda kwa Baba.+ 13  Pia, kila jambo lenye munaomba katika jina langu, nitalifanya, ili Baba atukuzwe kuhusiana na Mwana.+ 14  Mukiomba jambo lolote katika jina langu, nitalifanya. 15  “Kama munanipenda, mutashika amri zangu.+ 16  Na nitamuomba Baba, na atawapatia ninyi musaidizi* mwingine akuwe pamoja na ninyi milele,+ 17  roho ya ile kweli,+ yenye ulimwengu hauwezi kupokea, kwa sababu hauione na hauijue.+ Ninyi munaijua, kwa sababu hiyo inakaa pamoja na ninyi na iko ndani yenu. 18  Sitawaacha ninyi peke yenu.* Ninakuja kwenu.+ 19  Kisha tu wakati kidogo ulimwengu hautaniona tena, lakini ninyi mutaniona,+ kwa sababu ninaishi na ninyi mutaishi. 20  Siku hiyo mutajua kwamba mimi niko katika umoja na Baba yangu na ninyi muko katika umoja na mimi na mimi niko katika umoja na ninyi.+ 21  Kila mutu mwenye kuwa na amri zangu na kuzishika, huyo ndiye mwenye ananipenda. Na kila mutu mwenye ananipenda atapendwa na Baba yangu, na mimi nitamupenda na nitajionyesha waziwazi kwake.” 22  Yuda,+ hapana Yuda Iskariote, akamuuliza: “Bwana, kumetokea nini ili ukusudie kujionyesha waziwazi kwetu lakini hapana kwa ulimwengu?” 23  Yesu akamujibu: “Kama mutu yeyote ananipenda, atashika neno langu,+ na Baba yangu atamupenda, na tutakuja kwake na kukaa pamoja naye.*+ 24  Kila mutu mwenye hanipendi hashike maneno yangu. Neno lenye munasikia haliko langu, lakini ni la Baba mwenye alinituma.+ 25  “Nimewaambia ninyi mambo haya wakati ningali pamoja na ninyi. 26  Lakini musaidizi, roho takatifu yenye Baba atatuma katika jina langu, huyo atawafundisha mambo yote na kuwakumbusha mambo yote yenye niliwaambia.+ 27  Ninawaachia ninyi amani; ninawapatia amani yangu.+ Siwapatie amani kwa njia yenye ulimwengu unaitoa. Mioyo yenu isivurugike wala kuregea kwa woga. 28  Mulisikia kwamba niliwaambia, ‘Ninaenda na nitakuja tena kwenu.’ Kama mungenipenda, mungefurahi kwamba ninaenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mukubwa kuliko mimi.+ 29  Kwa hiyo sasa nimewaambia mbele jambo hilo litokee, ili muamini wakati litatokea.+ 30  Sitasema na ninyi tena mambo mengi, kwa maana mutawala wa ulimwengu+ anakuja, na hana uwezo juu yangu.+ 31  Lakini, ili ulimwengu ujue kwamba ninamupenda Baba, ninafanya kama vile Baba aliniamuru.+ Musimame, tutoke hapa.

Maelezo ya Chini

Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “mufariji.”
Ao “mayatima.”
Ao “na tutafanya makao yetu kwake.”