Zaburi 90:1-17

  • Mungu wa milele na mwanadamu mwenye kuishi wakati mufupi

    • Miaka elfu moja ni kama jana (4)

    • Mwanadamu anaishi miaka makumi saba mupaka makumi munane (10)

    • “Utufundishe namna ya kuhesabia siku zetu” (12)

Sala ya Musa, mutu wa Mungu wa kweli.+ 90  Ee Yehova, umekuwa makao yetu*+ katika vizazi vyote.   Mbele milima haijazaliwa Ao mbele haujatokeza* dunia na inchi yenye kuzaa,+ Tangu milele mupaka milele, wewe ni Mungu.+   Unamufanya mwanadamu mwenye anaweza kufa arudie katika mavumbi; Unasema: “Murudie, ninyi wana wa binadamu.”+   Kwa maana miaka elfu moja (1 000) mbele ya macho yako ni kama vile siku ya jana ikiisha kupita,+ Kama vile kesha moja la usiku.   Unawafagilia mbali;+ wanakuwa kama usingizi tu; Asubui, wao ni kama majani yenye kuchipuka.+   Asubui yanatoa maua na kuwa mupya, Lakini mangaribi yanafifia na kukauka.+   Kwa maana tumeteketezwa na hasira yako+ Na tumeogopeshwa sana na kasirani yako kali.   Unatia makosa yetu mbele yako;*+ Siri zetu zinafunuliwa na mwangaza wa uso wako.+   Siku zetu zinafifia* kwa sababu ya kasirani yako kali; Na miaka yetu inafikia mwisho kama sauti ya chini-chini. 10  Urefu wa maisha yetu ni miaka makumi saba (70), Ao makumi munane (80)+ kama mutu iko* na nguvu za pekee.* Lakini imejaa taabu na huzuni; Na inapita haraka, na tunaenda zetu.+ 11  Ni nani anaweza kuelewa nguvu za hasira yako? Kasirani yako kali ni kubwa kama woga wenye unastahili kuonyeshwa.+ 12  Utufundishe namna ya kuhesabia siku zetu+ Ili tupate moyo wa hekima. 13  Rudia, Ee Yehova!+ Hilo litaendelea mupaka wakati gani?+ Sikilia huruma watumishi wako.+ 14  Utushibishe asubui kwa upendo wako mushikamanifu,+ Ili tupige vigelegele vya shangwe na kushangilia+ siku zetu zote. 15  Utufanye tushangilie kulingana na siku zenye umetutesa,+ Kwa kadiri ya miaka mingi yenye tumepata musiba.+ 16  Watumishi wako waone kazi zako, Na wana wao waone utukufu wako.+ 17  Wema wa Yehova Mungu wetu ukuwe juu yetu; Fanya kazi ya mikono yetu ifanikiwe.* Ndiyo, fanya kazi ya mikono yetu ifanikiwe.*+

Maelezo ya Chini

Ao pengine, “kimbilio letu.”
Ao “haujatokeza kama kwa maumivu ya kuzaa.”
Ao “Unajua makosa yetu.”
Ao “Maisha yetu yanafifia.”
Ao “eko.”
Ao “kwa sababu ya uwezo wa pekee.”
Ao “Fanya kazi ya mikono yetu ikuwe imara kabisa.”
Ao “fanya kazi ya mikono yetu ikuwe imara kabisa.”