Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Teknolojia Iko na Matokeo Gani juu ya Ndoa Yako?

Teknolojia Iko na Matokeo Gani juu ya Ndoa Yako?

Wakati bibi na bwana wanatumia muzuri teknolojia, ndoa yao itakuwa nguvu. Kwa mufano, ile inaweza kusaidia bibi na bwana waendelee kuongea hata kama hawako fasi moja.

Lakini, bibi na bwana fulani wanatumia mubaya teknolojia ili . . .

  • kuiba wakati wenye wangetumia pamoja.

  • kuwafanya watumike ku nyumba, hata kama hakuna lazima kabisa ya kufanya vile.

  • kuwafanya wafichane mambo fulani ao hata kukosa uaminifu.

MAMBO UNAPASWA KUJUA

KUPITISHA WAKATI PAMOJA

Bwana mumoja mwenye kuitwa Michael anasema hivi: “Wakati fulani, saa yenye miye na bibi yangu tuko pamoja, hakuwake kabisa pale. Macho yake ni ku telefone tu na kisha anasema hivi, ‘mbona siyamaliza hata kuangalia byote.’” Bwana mwingine mwenye kuitwa Jonathan anasema kama mu hali za vile “bibi na bwana wanaweza kuwa pamoja kimwili lakini kila mutu anajisikia sawa vile iko fasi yake.”

JAMBO YA KUFIKIRIA: Ni mara ngapi unakuwaka uko unazungumuza ku telefone ao kuandikia ujumbe mutu fulani mu wakati yenye ungetumia ili kuzungumuza pamoja na bibi yako?​—WAEFESO 5:33.

KAZI

Watu fulani wako na kazi yenye inawalazimisha kujibia ku telefone ao ujumbe fulani hata usiku wakati wako ku nyumba. Lakini hata watu wenye kazi yao haiwalazimishe ile mambo, wanaweza tu kupitisha wakati mingi na wako wanatumika wakati wako ku nyumba. Bwana mumoja mwenye kuitwa Lee anasema hivi: “Inakuwaka nguvu sana kwangu, kukosa kuitika ku telefone ao kujibia ujumbe fulani wa kazi mu wakati yenye nilipanga kupitisha pamoja na bibi yangu.” Bibi mumoja mwenye kuitwa Joy anasema hivi: “Natumikiaka ku nyumba, njo maana inakuwaka nguvu kujua wakati wenye napaswa kuacha kutumika. Inaomba kujikaza sana ili kuwa na usawaziko.”

JAMBO YA KUFIKIRIA: Unasikilizaka kwa uangalifu bibi ao bwana yako wakati iko anazungumuza na weye?​—LUKA 8:18.

UAMINIFU

Watu wengi wanasema kama walikosana na bibi ao bwana yao, juu mumoja kati yao alikuwa na mashaka kuhusu mambo yenye mwingine alitia ku Enternete. Hata watu fulani wanasema kama wanatiaka mambo fulani ku Enternete kwa uficho, mambo yenye hawawezi kupenda bibi ao bwana yao ajue.

Watu wengi wanaamini kama Enterne iko na mambo fulani hatari yenye kufichwa na ile inaweza kuwa mwepesi kwa mutu kufanya uzinifu. Haishangaze kuona kama wanasheria wa mambo ya kuvunja ndoa wanasema kama Enternete inafanya bibi na bwana wengi wavunje ndoa.

JAMBO YA KUFIKIRIA: Kama uko bwana, je, unafichikaka bibi yako wakati uko unaongea na mwanamuke fulani? Kama uko bibi, Je, unafichikaka bwana yako wakati uko unaongea na mwanaume fulani?​—MEZALI 4:23.

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

TANGULIZA MAMBO YA MAANA ZAIDI

Mutu mwenye hahangaikiake kukula, hawezi kuwa na afya ya muzuri. Ni vile pia kwa mutu mwenye hahangaikiake kupitisha wakati pamoja na bibi ao bwana yake. Ile inaweza kuleta matatizo mu ndoa yao.​—Waefeso 5:28, 29.

KANUNI YA BIBLIA: “Muhakikishe mambo ya maana zaidi.”​—WAFILIPI 1:10.

Zungumuza na bibi ao na bwana yako juu ya mambo fulani yenye kuwa hapa chini ao andika mawazo fulani yenye itasaidia juu teknolojia isivuruge ndoa yenu.

  • Kujikaza kula pamoja hata mara moja kwa siku

  • Kuamua wakati fulani wenye hamutakuwa natumikisha vyombo vya kielektroniki

  • Kupanga programu ili kufanya jambo fulani la maana sana pamoja

  • Kuzimisha vyombo vyetu vya kielektroniie usiku na kuvitia mbali na kwenye tunalala

  • Kuzimisha ao kutia mbali vyombo vyenu vya kielektroniki kwa dakika 15 juu weye na bibi yako muzungumuze bila kusumbuliwa

  • Kufunga Enternete kwa wakati fulani