Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Utaamini Nini?

Utaamini Nini?

“Haiko kusema ulimwengu unaweza kujitokea wenyewe, ukweli ni kwamba ulijitokezaka wenyewe.”​—Stephen Hawking na Leonard Mlodinow, wanafizikia, 2010.

“Mungu aliumba mbingu na dunia.”​—Biblia, Mwanzo 1:1.

Mungu njo aliumbaka ulimwengu na vitu vyenye uzima ao vilijitokeaka tu? Maneno ya wanasayansi wenye wanatajwa ku mwanzo wa hii habari, na maneno ya kwanza yenye iko mu Biblia inatoa majibu yenye kuwa tofauti kabisa ku ile ulizo. Kuko watu wenye wanaamini kabisa kama ulimwengu na vitu vyenye uzima vyenye viko ndani yake vilijitokeaka tu vyenyewe. Na kuko wenye wanaamini kama Mungu njo aliviumbaka. Lakini kuko wengine wengi wenye hawajue waamini nini. Ile ulizo imezungumuziwa sana mu vitabu vyenye watu wanapendaka sana na mu programu mbalimbali za televizyo.

Pengine walimu wako walikuambiaka kwa uhakika kama hakuna mwenye aliumbaka ulimwengu na vitu vyenye uzima vyenye viko ndani yake, ni kusema, vilijitokeaka tu vyenyewe. Lakini walikuonyeshaka mambo yenye kuhakikisha kabisa kama hakuna Muumbaji? Ao pengine ulishakasikia viongozi wa dini wanahubiri kama kuko Muumbaji. Sasa, walikuonyeshaka mambo yenye kuahakikisha kama ile yenye wanasema ni ya kweli? Ao walikuambiaka uamini tu mambo yenye wanasema?

Pengine ulishakafikiria ile ulizo na ukawaza kama hakuna mwenye anaweza kuhakikisha ikiwa kuko Muumbaji ao hapana. Na pengine uko unajiuliza hii ulizo ingine: Kujua ile iko na faida gani?

Hii gazeti itazungumuzia mambo fulani ya kweli yenye imesaidia watu wengi waamini kama kuko Muumbaji. Kisha itakusaidia ujue juu ya nini ni jambo ya maana kujua namna uzima ulianzaka.