Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KITU HIKI KILIJIFANYA CHENYEWE?

Nyuzi za Kome Mwenye Kuishi Katika Bahari

Nyuzi za Kome Mwenye Kuishi Katika Bahari

KOME mwenye kuishi katika bahari anabana kwenye miamba, mbao, ao kwenye sehemu ya chini ya mashua (bateau). Lakini, tofauti na viumbe fulani wenye kuishi katika bahari wenye wanabana nguvu sana kwenye kitu fulani, kome mwenye kuishi katika bahari anabana kupitia nyuzi ndogo zenye kuitwa byssus. Hata kama nyuzi hizo zinafanya ikuwe mwepesi zaidi kwa kome kutafuta chakula na kuhama, zinaonekana kuwa hazina nguvu kabisa ya kubana wakati wa mawimbi ya bahari. Namna gani nyuzi hizo zinasaidia kome abane na mawimbi ya bahari yasimubebe?

Fikiria jambo hili: Nyuzi za byssus ziko ngumu kwenye mwisho wa upande moja, lakini teketeke kwenye mwisho wa upande mwengine. Wanasayansi walivumbua kwamba 80% ya sehemu yenye kuwa ngumu ya nyuzi hizo na 20% ya sehemu yenye kuwa teketeke ni za lazima sana ili kumusaidia kome abane nguvu sana kwenye kitu fulani. Kwa hiyo, nyuzi hizo zinaweza kuendelea kubana zaidi wakati zinasukumwa-sukumwa na maji ya bahari.

Profesa Guy Genin anasema kama matokeo ya uchunguzi huo ni yenye “kushangaza sana.” Anaongezea hivi: “Jambo la ajabu katika kiumbe huyo ni muungano wa sehemu hiyo yenye kuwa mwepesi na sehemu yenye kuwa ngumu.” Wanasayansi wanaamini kwamba namna nyuzi za kome zimefanywa inaweza kuigwa na kutumiwa katika njia mbalimbali kama vile kubanisha vitu kwenye majengo na mashua zenye kupita chini ya maji, kuunganisha mishipa kwenye mifupa, na kubanisha sehemu zenye zilipasuliwa wakati wa kufanya upasuaji. Herbert Waite, profesa kwenye masomo ya juu ya Kalifornia katika Santa Barbara, Amerika, anasema hivi: “Ulimwengu unajaa maajabu yenye yanaweza kutufundisha mambo mengi, na hata ufundi wa kubanisha vitu.”

Unawaza namna gani? Nyuzi za kome mwenye kuishi katika bahari zilijitokeza zenyewe? Ao ziliumbwa?