Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

“Alama Yenye Nguvu na Yenye Kuonekana Waziwazi”

“Alama Yenye Nguvu na Yenye Kuonekana Waziwazi”

UPANDE wa mashariki wa pembeni ya Muto Motoyasu katika muji wa Hiroshima, Japani, kuna nyumba moja kubwa ambayo sehemu yake imebaki yenye kubomoka tangu 1945. Sababu gani nyumba hiyo haijajengwa tena katika miaka karibu 70 ambayo imepita?

Kisha kumalizika kujengwa katika 1915, nyumba hiyo ya gorofa tatu iliyojengwa kwa matofali na simenti ilikuwa mahali pa kuonyeshea vitu vilivyotengenezwa katika viwanda. Lakini mambo yalibadilika tarehe 6 Mwezi wa 8, 1945, na saa 2 na dakika15 ya asubuhi. Wakati huo, bomu la kwanza la atomiki ambalo lilikuwa halijatumiwa katika vita lililipuka na kurushwa meta 550 hivi juu ya muji na karibu mara moja juu ya nyumba hiyo. Watu wote waliokuwa ndani walikufa mara moja. Hata hivyo, misingi ya nyumba hiyo haikubomoka.

Gazeti moja la UNESCO * linasema kama nyumba hiyo ambayo imelindwa bila kutengenezwa ni “alama yenye nguvu na yenye kuonekana waziwazi ya bomu inayoweza kuharibu sana ambayo wanadamu wamekwisha kutengeneza.” Katika 1996 nyumba hiyo iliwekwa kwenye oroza ya Maeneo ya Dunia Yanayostahili Kulindwa kwa jina la Ukumbusho wa Amani ya Hiroshima.

Inahuzunisha kwamba, makumbusho hayo haijamaliza vita inayotokea kila mara kwa sababu ya tamaa, mutu kupenda sana inchi yake, kuchukia watu wa taifa, rangi, dini, na kabila ingine. Lakini, vita itaendelea mupaka milele?

Biblia inajibu hapana! Andiko la Zaburi 46:9 linasema: ‘[Mungu] anakomesha vita mupaka kwenye mwisho wa dunia. Upinde anauvunja na kuukata mukuki vipande-vipande; magari ya kukokotwa anayateketeza motoni.’ Wakati huo, Mungu atatosha serikali za watu na kutia serikali yake itakayotawala dunia, ni kusema, Ufalme wa Mungu, ulio katika mikono ya Yesu Kristo, anayeitwa ‘Mufalme wa wafalme.’—Ufunuo 11:15; 19:16.

Kisha, vikumbusho vya matokeo mabaya ya vita havitakuwa vya lazima tena. Andiko la Isaya 65:17 linasema hivi: “Vitu vya zamani”, ni kusema, matatizo na maumivu ya moyoni ya leo, “hayatakumbukwa akilini, wala hayataingia moyoni.”

^ fu. 4 Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni.