Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Hekima Yenye Kulinda

Hekima Yenye Kulinda

‘Fidia ya mutu ni mali yake, lakini maskini hana cha kutishwa [cha kuogopa].’—METHALI 13:8, BIBLIA HABARI NJEMA.

HATA ikiwa kuwa tajiri kunaweza kuleta faida fulani, mali inaweza kuleta magumu, zaidi sana katika wakati wetu wa hatari. (2 Timotheo 3:1-5) Katika inchi fulani, matajiri, na hata watembeaji wenye kuonekana kuwa na mali nyingi, wamefuatwa na watu wenye kuiba na pia watu wenye kukamata watu kwa nguvu kusudi walipwe feza ili kuwaachilia.

Juu ya inchi moja yenye kuendelea sana, ripoti moja ya habari ilisema hivi: “Wizi wenye jeuri, udanganyifu na kukamata watu kwa nguvu ni mambo yanayoleta uadui kati ya matajiri na maskini. Restora zinaweka walinzi wenye kuwa na silaha; nyumba za matajiri zina kuta zenye kuwa na singa zenye miiba, taa kubwa-kubwa, kamera na watu wa kufanya ulinzi.” Katika inchi zingine nyingi kuna hali kama hiyo.

Lakini Biblia inasema kuwa maskini hana cha kuogopa. Namna gani unaweza kufaidika na hekima hiyo ya maana sana? Ikiwa unaishi katika eneo lenye kujulikana sana kuwa na uovu na matendo ya kupigana na kuuana ao ikiwa unapenda kusafiri kuenda katika eneo kama hilo, usifanye watu wakukazie uangalifu kwa kuonekana kuwa tajiri. Fikiria kwa uangalifu vitu unavaa na vitu unabeba mbele ya watu, zaidi sana ikiwa mali yako itaonekana. Andiko la Methali 22:3 linasema kuwa ‘mutu mwerevu ni yule ambaye ameona musiba na kujificha, lakini wasio na uzoefu wameendelea mbele nao lazima waumie.’

Hekima iliyo katika Biblia inaonyesha kuwa Muumbaji wetu anatuhangaikia. Anataka tukuwe salama. Andiko la Mhubiri 7:12 linasema kuwa “hekima [kama hiyo] ni ulinzi,” kwa sababu ‘inawahifazi [inawalinda] hai waliyo nayo.’