Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kitabu cha Kukunjwa cha Zamani “Chenye Hakingeweza Kufunguliwa”

Kitabu cha Kukunjwa cha Zamani “Chenye Hakingeweza Kufunguliwa”

Kitabu cha kukunjwa cha Ein Gedi chenye kuungua mubaya hakikuweza kusomwa tangu wakati kilivumbuliwa katika mwaka wa 1970. Mashine yenye kuwa na uwezo wa kutokeza umbo ilionyesha kama kitabu hicho kiko na sehemu ya kitabu cha Mambo ya Walawi; sehemu hiyo ilikuwa na jina la pekee la Mungu

KATIKA mwaka wa 1970, watu wenye kuchimbua vitu vya zamani walivumbua kitabu kimoja cha kukunjwa chenye kuungua mubaya katika Ein Gedi, Israeli, karibu na inchi kavu pembeni ya Bahari ya Chumvi, upande wa mangaribi. Walipata kitabu hicho cha kukunjwa wakati walikuwa wanachimbua sinagogi moja lenye liliunguzwa wakati kijiji kimoja kiliharibiwa, pengine kati ya mwaka wa 500 na 550 K.K.Y. Kwa sababu kitabu hicho cha kukunjwa kilikuwa katika hali ya mubaya sana, haingewezekana kusoma mambo yenye iliandikwa ndani, na hata haingewezekana kukifungua bila kukiharibisha. Lakini, kwa kutumia mashine yenye kuwa na uwezo wa kutokeza umbo, kitabu hicho cha kukunjwa kiliweza “kufunguliwa.” Na kwa musaada wa programu mupya ya ordinatere ya kukamata picha, tunaweza kusoma mambo yenye kuwa katika kitabu hicho.

Picha ya maandishi ya kitabu hicho cha kukunjwa imeonyesha nini? Kitabu hicho ni maandishi ya Biblia. Mambo yenye kuandikwa ku sehemu zenye zilibakia za kitabu hicho ilikuwa maandiko ya mwanzo-mwanzo ya kitabu cha Mambo ya Walawi. Ile maandiko iko na jina la pekee la Mungu katika Kiebrania, kwa kutumia Tetragramatoni. Inaonekana kuwa kitabu hicho kiliandikwa kati ya mwaka wa 50 K.K.Y. na mwaka wa 400 K.K.Y., ile inafanya kikuwe kitabu cha kukunjwa cha Kiebrania cha zamani sana chenye kimevumbuliwa kisha kuvumbuliwa kwa Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi (maandishi ya Qumran). Katika gazeti Jerusalem Post, Gil Zohar anasema kama “mbele kitabu cha kukunjwa cha Ein Gedi kivumbuliwe, kulipita miaka karibu 1 000 kisha kuvumbua maandishi ya zamani sana ya Biblia, ni kusema, Vitabu vya Kukunjwa vya Bahari ya Chumvi (tangu mwaka wa 100 M.K.Y.) na maandishi ingine ya zamani sana, ni kusema, Kodeksi ya Alepo (tangu karibu mwaka wa 930 K.K.Y.)” Kulingana na watu wenye elimu, maandishi ya kitabu hicho cha kukunjwa chenye hakingeweza kufunguliwa inaonyesha kama Maandishi ya Wamasora ya Torati “ililindwa kwa uaminifu, na kama makosa ya waandikaji haikubadilisha ujumbe.”