Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Juu ya Nini Mungu Hajibiake Sala Zote?

Juu ya Nini Mungu Hajibiake Sala Zote?

Baba yetu wa mbinguni, Yehova Mungu, iko tayari kusikiliza sala zetu zenye kutoka katika moyo, na anapenda kufanya vile. Lakini kuko mambo yenye inafanyaka asijibie sala zetu. Ni mambo gani, na tunapaswa kukumbuka nini wakati tuko tunasali? Ona mashauri fulani yenye Biblia inatutolea.

“Wakati munasali, musiseme mambo yaleyale tena na tena.”​—Matayo 6:7.

Yehova hapendi turudilie sala zenye tulishachunga mu akili, ao kusoma sala mu kitabu. Lakini, anapenda tusali kwake kutoka katika moyo. Wazia vile unaweza kujisikia ikiwa uko na rafiki mwenye anakuambiaka maneno ileile kila siku. Marafiki wa kweli wanazungumuzaka waziwazi na wanasemaka mambo yenye inatoka katika moyo. Wakati tunasali kwa Baba yetu wa mbinguni kwa kutumia maneno yetu wenyewe, ile inaonyesha kama tunamuona kuwa rafiki yetu.

“Wakati munaomba, hamupokee kwa sababu munaomba kwa kusudi la mubaya.”​—Yakobo 4:3.

Tunaelewa kama Mungu hawezi kujibia sala zetu ikiwa tunamuomba mambo yenye hapendi tufanye ao tukuwe nayo. Kwa mufano, Yehova anaweza kujibia sala ya mutu mwenye kucheza muchezo wa kupata feza? Anatuambia waziwazi kama hatupaswe kuwa na pupa na kuamini mambo ya bahati. (Isaya 65:11; Luka 12:15) Kwa kweli hatupaswe kutazamia kama Mungu atajibia sala za vile! Ili Mungu ajibie sala zetu, tunapaswa kuhakikisha kama sala zetu zinapatana na mambo yenye anatuambia mu Biblia.

“Mwenye anakataa kusikiliza sheria​—hata sala yake inachukiza.”​—Mezali 28:9.

Zamani, Mungu hakujibia sala za wale wenye hawakutii sheria zake za haki. (Isaya 1:15, 16) Mungu hajabadilika. (Malaki 3:6) Kama tunapenda Mungu ajibie sala zetu, tunapaswa kujikaza kuishi kulingana na sheria zake. Tuseme nini kama tulifanyaka mambo ya mubaya zamani? Ile inamaanisha kama Yehova hawezi hata kidogo kusikiliza sala zetu? Jibu ni hapana! Kwa upendo Mungu atatusamehe kama tunabadilisha maisha yetu na kujikaza sana ili kumufurahisha.​—Matendo 3:19.