Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Walijitoa kwa Kujipendea—Katika Mikronesia

Walijitoa kwa Kujipendea—Katika Mikronesia

KATHERINE alikomalia États-Unis, na alipokuwa na miaka 16 alibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova. Alikuwa na bidii katika kazi ya kuhubiri lakini katika eneo lake watu wengi hawakupendezwa. Anasema hivi: “Nilisoma habari za watu ambao walisali ili Mungu awatumie mutu wa kuwasaidia kumujua. Kila mara nilitumaini kwamba ningepata mutu kama huyo, lakini sikumupata.”

_Kisha kuhubiri miaka mingi katika eneo hilo, Katherine alianza kufikiria kuhamia katika eneo lingine ambamo watu wangekubali ujumbe wa Ufalme. Lakini alijiuliza kama angeweza kufanya hivyo. Katika maisha yake alikuwa amesafiri mbali na familia yake mara moja tu, na kwa muda wa juma mbili; na kila siku alikuwa anakumbuka sana familia yao. Lakini, kwa sababu alitaka kujionea furaha inayotokana na kusaidia watu kumujua Yehova, aliamua kuenda. Kisha kufikiria maeneo mengi yaliyokuwa na uhitaji, aliandikia biro ya tawi ya Guam ili kupata habari za lazima. Katika Mwezi wa 7 mwaka wa 2007, alipokuwa na miaka 26, Katherine alihamia katika kisiwa cha Saipan, kilicho katika Bahari ya Pasifiki, kilometre 10000 mbali na kwao. Mambo yalimuendea namna gani?

SALA MBILI ZINAJIBIWA

Muda mufupi kisha kuhamia katika kutaniko mupya, Katherine alikutana na Doris, mwanamuke aliyekuwa na miaka karibu 45, na ambaye alikubali kujifunza Biblia. Kisha kujifunza na mwanamuke huyo sura tatu za kwanza-kwanza za kitabu Biblia Inafundisha, Katherine alianza kuwa na wasiwasi. Anaeleza hivi: “Doris alikuwa mwanafunzi muzuri, na nilipenda funzo hilo liendelee. Ilikuwa mara yangu ya kwanza kuongoza kwa ukawaida funzo la Biblia; kwa hiyo nilifikiri kwamba Doris alihitaji dada mwenye uzoefu zaidi ili kujifunza pamoja naye, pengine dada aliye na miaka yake.” Katherine alimuomba Yehova amusaidie kupata dada anayestahili ili aendelee kujifunza na Doris. Kisha aliamua kumujulisha Doris kwamba atamutafutia dada mwengine wa kujifunza naye Biblia.

Katherine anaeleza: “Mbele nimuambie jambo hilo, Doris aliniambia kwamba angependa kuniambia jambo fulani. Kisha kumusikiliza, nilimuelezea namna Yehova alinisaidia kupambana na hali fulani sawa na yake. Alinishukuru.” Kisha Doris alimuambia Katherine: “Yehova ananisaidia kupitia wewe. Siku ulifika kwangu kwa mara ya kwanza, nilikuwa  nimesoma Biblia kwa muda wa saa nyingi. Nilikuwa nikilia, nikimuomba Mungu anitumie mutu wa kunisaidia kuelewa Biblia. Kisha, uligonga kwenye mulango wangu. Yehova alijibu sala yangu!” Katherine anatokwa na machozi wakati anaeleza habari hiyo inayogusa moyo. Anasema hivi: “Maneno ya Doris yalikuwa jibu kwa sala yangu. Yehova alionyesha kwamba nilistahili kuendelea kujifunza na Doris.”

Doris alibatizwa katika mwaka wa 2010; leo anaongoza mafunzo mengi ya Biblia. Katherine anasema: “Mimi ni mwenye shukrani sana kuona namna muradi wangu wa tangu zamani wa kutaka kusaidia mutu anayependezwa akuwe mutumishi wa Yehova unatimia!” Leo, Katherine ni painia wa pekee katika kisiwa cha Kosrae, kilicho katika Bahari ya Pasifiki.

KUPAMBANA NA MAGUMU YA AINA TATU

Ndugu na dada zaidi ya 100 wa inchi mbalimbali (walio na miaka kati ya 19 na 79) wametumikia katika Mikronesia, mahali ambako kuna uhitaji mukubwa sana wa wahubiri. Erica, dada ambaye alihamia Guam katika mwaka wa 2006 wakati alikuwa na miaka 19, anaeleza vizuri namna ndugu na dada hao wanajisikia. Anasema hivi: “Ni jambo lenye kufurahisha sana kuwa painia katika eneo ambamo watu wana kiu ya kupata kweli. Ninamushukuru sana Yehova kwa kunipatia pendeleo hilo la utumishi. Hilo ndilo jambo nzuri zaidi katika maisha!” Leo, Erica ni painia wa pekee katika eneo la Ebeye, katika Visiwa vya Marshall. Bila shaka, mutu anapata magumu fulani anapotumikia katika inchi ya kigeni. Acheni tuzungumuzie tu magumu ya aina tatu na tuone namna wale waliohamia Mikronesia wanapambana nayo.

Erica

Hali mupya ya maisha. Simon alikuwa na miaka 22 alipofika katika kisiwa cha Palau katika mwaka wa 2007; muda mufupi baadaye, alitambua kwamba kazi ya kimwili ambayo angefanya haingemutolea mushahara ambao alikuwa anapokea katika inchi yake Angleterre. Anasema hivi: “Nilipaswa kujifunza kutonunua vitu ovyo-ovyo. Sasa, ninachagua kwa uangalifu chakula ambacho ninapaswa kununua, na ninanunua vitu mahali ambapo vinauzishwa bei chini. Kama chombo fulani kinaharibika, ninanunua sehemu ingine iliyotumiwa na ninatafuta mutu fulani wa kunitengenezea chombo hicho.” Kuishi maisha mepesi kulimusaidia namna gani? Simon anasema: “Hilo limenisaidia kujua mambo ya lazima zaidi katika maisha na namna ninaweza kuishi na vitu vichache. Mara nyingi niliona wazi kwamba Yehova alikuwa ananisaidia. Kwa muda wa miaka 7 ambayo nimefanya katika eneo hilo, sijakosa hata siku moja chakula ao nafasi ya kulala.” Kwa kweli, Yehova anasaidia wale wanaoishi maisha mepesi kwa sababu wanataka kutafuta kwanza Ufalme.—Mt. 6:32, 33.

Kuwa mbali na familia. Erica anasema hivi: “Ninawapenda sana watu wa jamaa yangu, kwa hiyo niliogopa kwamba kuwakumbuka kila mara kungekuwa na matokeo mabaya juu ya kazi yangu ya mahubiri.” Alifanya nini ili kujitayarisha? Anasema hivi: “Mbele ya kuhama, nilisoma katika Munara wa Mulinzi habari kuhusu kuwakumbuka kila mara watu wa jamaa. Hilo lilinisaidia kabisa nitayarishe moyo wangu ili kupambana na tatizo hilo. Kwa mufano nilisoma habari ya mama mumoja aliyemutia moyo binti yake kwa kumuambia hivi: ‘Yehova anaweza  kukuhangaikia vizuri zaidi kuliko mimi.’ Maneno hayo yalinitia moyo sana.” Hannah na Patrick, bwana yake, wanatumikia katika eneo la Majuro, katika visiwa vya Marshall. Kupendezwa na ndugu na dada katika kutaniko kunamusaidia Hannah apambane na tatizo la kuishi mbali na familia. Anasema hivi: “Kila mara ninamushukuru Yehova kwa sababu amenipatia ndugu na dada wa duniani pote ambao pia ni familia yangu. Bila musaada wao wenye upendo, singeweza hata kidogo kutumikia katika maeneo yaliyo na uhitaji mukubwa wa wahubiri.”

Simon

Kupata marafiki. Simon anasema hivi: “Wakati unafika katika inchi ya kigeni, karibu mambo yote ni tofauti kabisa. Wakati fulani ninashindwa kuongea na wengine juu ya mambo ya kuchekesha kwa sababu ninawaza kwamba hawatanielewa vizuri.” Erica anasema hivi: “Mwanzoni, nilijisikia kuwa peke yangu, lakini hilo lilinisaidia kuchunguza sababu zilizonifanya nihamie katika eneo lingine. Sikuhama kwa sababu ya faida yangu mwenyewe lakini ili kufanya mengi katika kazi ya Yehova.” Anaongeza hivi: “Hatua kwa hatua, nilipata marafiki wazuri, ambao ninapenda sana.” Simon alijikaza sana ili kujifunza luga ya Palauan, ambayo inamusaidia ‘kupanuka’ kuelekea ndugu na dada wa eneo lake mupya. (2 Kor. 6:13) Jitihada zake za kujifunza luga hiyo zilimusaidia afanye urafiki pamoja na ndugu na dada. Wakati ndugu wanaohamia katika inchi za kigeni wanatumika pamoja na ndugu wanaokuta huko, hilo linawasaidia wote kuwa marafiki wa karibu. Wale wanaojitoa ili kutumikia katika maeneo yaliyo na uhitaji mukubwa wa wahubiri wanapata baraka gani zingine?

‘KUVUNA KWA UWINGI’

Mutume Paulo alisema hivi: ‘Yeye anayepanda kwa uwingi atavuna pia kwa uwingi.’ (2 Kor. 9:6) Bila shaka kanuni iliyo katika maneno hayo inahusu pia wale wanaopanua utumishi wao. Ni matunda gani ambayo ‘wanavuna kwa uwingi’ katika Mikronesia?

Patrick na Hannah

Katika Mikronesia, kuna nafasi nyingi za kuanzisha mafunzo ya Biblia na kuona namna watu wanaojifunza Neno la Mungu na kulitumikisha wanafanya maendeleo ya kiroho. Patrick na Hannah walihubiri pia katika kisiwa kidogo cha Angaur, kilicho na wakaaji 320. Kisha kuhubiri huko kwa miezi miwili, walikutana na mama mumoja anayelea mutoto wake peke yake. Bila kukawia alikubali kujifunza Biblia, alikubali kweli kwa moyo wote, na alifanya mabadiliko makubwa katika maisha yake. Hannah anasema hivi: “Kila mara tulipomaliza kujifunza na mama huyo na kuondoka tukiwa juu ya kinga zetu, tuliangaliana na Patrick na kusema: ‘Aksanti Yehova!’” Hannah anaongeza: “Ninajua kama Yehova angemuvuta mwanamuke huyo kwa njia moja ao nyingine, lakini kwa sababu ya kutumikia katika maeneo yenye uhitaji mukubwa wa wahubiri, tulipata pendeleo la kumusaidia amujue Yehova. Hilo ndilo jambo nzuri zaidi ambalo tumejionea katika maisha yetu yote!” Erica anasema hivi: “Wakati unasaidia mutu ajifunze kumujua Yehova, unapata furaha kubwa sana!”

UNAWEZA PIA KUJITOLEA?

Katika maeneo mengi, kuna uhitaji mukubwa wa wahubiri wa Ufalme. Je, unaweza pia kuhamia katika maeneo yanayohitaji musaada? Sali kwa Yehova ili aendelee kuchochea nia yako ya kupanua utumishi. Zungumuza juu ya muradi wako pamoja na wazee wa kutaniko, mwangalizi wa muzunguko, ao pamoja na wale ambao wamekwisha kutumikia katika maeneo yenye uhitaji. Unapopanga kuhamia katika eneo fulani, andikia tawi inayoongoza kazi katika eneo hilo, na uulize habari zaidi. * Pengine wewe pia unaweza kujiunga na maelfu ya ndugu na dada, vijana na wazee, walioa ao kuolewa, ao walio peke yao, ambao walijitoa kwa kujipendea, na ambao wameonja furaha ya ‘kuvuna kwa uwingi.’

^ fu. 17 Soma habari “Je, Unaweza ‘Kuvuka Uingie Makedonia’?” katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 8, 2011.