Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Je, Ulijua?

Je, Ulijua?

Je, Ulijua?

Barua zilitumwa namna gani wakati wa zamani?

Serikali ao guvernema ya Perse, ilikuwa na mupango kama vile wa poste ili kutuma barua za mambo ya taifa. Kitabu cha Biblia cha Esta kinaeleza namna gani mupango huo ulikuwa unatumika: ‘[Mordekai] akaandika kwa jina la Mufalme Ahasuero na kutia muhuri kwa pete ya mufalme na kupeleka barua kwa mukono wa wajumbe waliopanda farasi wenye kusafirisha barua wanaotumiwa katika utumishi wa kifalme, wana-farasi wenye mbio.’ (Esta 8:10) Katika Utawala wa Roma, kulikuwa pia mupango huo wa poste ili kutuma barua ao ujumbe juu ya mambo ya serikali na ya jeshi.

Barua za kipekee, kama vile zile zilizoandikwa na mutume Paulo ao zingine, hazikustahili kutumwa kwa njia hiyo. Matajiri walikuwa wakituma watumwa wao ili kupeleka barua. Lakini, watu wengi walituma barua zao kupitia watu waliofahamiana nao, ao hata wageni, waliokuwa wakisafiri kuelekea mahali ambapo walitaka kutuma barua. Watu wa familia, marafiki, maaskari, ao wafanyabiashara, wote hao walisaidia kupeleka barua. Lakini shida kubwa ilikuwa ni kutojua ikiwa mutu aliyepeleka barua alikuwa mwenye kutumainika na ikiwa atafikisha ujumbe namna ulivyotumwa. Biblia inaonyesha kama Paulo alituma barua zake fulani kupitia Wakristo wenzake waliokuwa wakisafiri.​—Waefeso 6:21, 22; Wakolosai 4:7.

Kazi ya kununua na kuuzisha ilifanywa namna gani katika Israeli ya zamani?

Mapato ya taifa la Israeli yalitegemea kilimo, kufuga wanyama, na biashara ya kubadilishana vitu. Biblia inataja soko zilizokuwa kwenye milango ya muji, kama vile “Lango la Kondoo,” “Lango la Samaki,” na “Lango la Vigae.” (Nehemia 3:1, 3; Yeremia 19:2) Kila jina la lango linaonyesha vitu ambavyo viliuzishwa mahali hapo. Tena, Maandiko yanataja “njia ya wapika mikate” ya Yerusalemu na pia vitu vingine vingi vilivyouzishwa.​—Yeremia 37:21, La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo.

Tuseme nini juu ya bei ya vitu? Kitabu kimoja kinachofasiria Biblia kinasema hivi: ‘Bei ya vitu iliendelea kubadilika-badilika, na ni vigumu kujua kwa uhakika bei ya kitu fulani, wakati fulani, na mahali fulani.’ Lakini, habari zilizo katika vitabu fulani vya zamani, na hata katika Biblia, zinaonyesha kama bei za vitu zilikuwa zinapanda tangu zamani. Kwa mufano, wakati wa zamani watumwa walikuwa wanauzishwa. Yosefu aliuzishwa kwa bei ya vipande 20 vya feza, inawezekana vipande hivyo vya feza ilikuwa ni shekeli. Labda hiyo ndiyo ilikuwa bei ya mutumwa katika miaka ya 1700 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. (Mwanzo 37:28) Miaka 300 baadaye, bei ya mutumwa ilikuwa ni shekeli 30. (Kutoka 21:32) Katika miaka ya 700 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, bei ya mutumwa ilikuwa ni shekeli 50. (2 Wafalme 15:20) Miaka 200 baadaye, wakati wa utawala wa Waperse, bei ya mutumwa ilipanda sana mupaka shekeli 90 ao zaidi. Hilo linaonyesha kama kupanda kwa bei ni tatizo la tangu zamani na linaendea mupaka leo.

[Picha katika ukurasa wa 22]

Mujumbe wa Perse anayepeleka barua

[Picha katika ukurasa wa 22]

Soko la matunda

[Picha zimetolewa na]

© DeA Picture Library/Art Resource, NY