Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KICHWA | BIBLIA INAZUNGUMUZIA HABARI GANI?

“Tumeona Masiya”!

“Tumeona Masiya”!

Miaka 400 hivi kisha kitabu cha mwisho cha Biblia cha Maandiko ya Kiebrania kuandikwa, unabii wa Mika kuhusu Masiya ulitimia: Yesu alizaliwa huko Bethlehemu. Miaka 30 hivi kisha hapo, katika mwaka wa 29 kisha kuzaliwa kwa Yesu, sehemu ya kwanza ya unabii wa Danieli juu ya kuja kwa Masiya ilitimia. Yesu alibatizwa, na Mungu akamutia mafuta kupitia roho takatifu. Kwa wakati uliofaa, Masiya aliyengojewa kwa muda murefu, Uzao ulioahidiwa, alifika!

Yesu alianza mara moja kazi yake, ni kusema, “kutangaza habari njema ya ufalme wa Mungu.” (Luka 8:1) Kama ilivyokuwa imetabiriwa, Yesu alikuwa mwema, mupole, na aliwahangaikia wengine kwelikweli. Mafundisho yake yalikuwa yenye kufaidi na yenye upendo, na aliponyesha watu waliokuwa na ‘kila namna ya uzaifu,’ na hivyo akaonyesha kwamba Mungu alikuwa pamoja naye. (Mathayo 4:23) Watu wa kila umri walimuendea Yesu kwa uwingi na kusema: “Tumeona Masiya”!​—Yohana 1:41, La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo.

Yesu alitabiri kwamba mbele Ufalme usimamie kabisa mambo yote, kungekuwa na vita, matetemeko ya inchi, na matatizo mengine mengi katika dunia. Aliwatia watu wote moyo ‘waendelee kukesha.”​—Marko 13:37.

Yesu alikuwa mutu mukamilifu ambaye aliendelea kumutii Mungu, lakini alikuwa na maadui ambao mwishowe walimuua. Kwa hiyo, kifo chake kilikuwa toleo kamilifu ili kununua kile ambacho Adamu na Eva walipoteza, ni kusema, tumaini la uzima wa milele katika Paradiso.

Kifo cha Yesu kilitimiza unabii, kwa kuwa kisha siku tatu, Mungu alimufufua Yesu akiwa kiumbe wa roho mwenye nguvu. Kisha Yesu aliwatokea wanafunzi wake zaidi ya 500. Mbele ya kupanda mbinguni, Yesu aliwapa wafuasi wake kazi ya kutangaza habari njema kumuhusu na kuhusu Ufalme wake kwa “watu wa mataifa yote.” (Mathayo 28:19) Walitimiza namna gani mugawo huo?

​—Habari hii inategemea Mathayo, Marko, Luka, Yohana, 1 Wakorintho.