Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

NAMNA MICHANGO YAKO INATUMIWA

Kutetea Uhuru wa Dini wa Wenyeji

Kutetea Uhuru wa Dini wa Wenyeji

TAREHE 1, MWEZI WA 5, 2021

 Kati ya mamia ya mamilioni ya watu wenye kuishi katika Amerika Latini, kuko mamilioni ya wale wenye wako na luga na desturi zao za kienyeji. Kati ya wale wenyeji, wengi ni ndugu na dada zetu wa kiroho, wenye wanapenda sana desturi yao. Juu ya kusaidia watu wajifunze kweli ya Biblia, wanatafsiri na kugawanya vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga zaidi ya 130 za wenyeji wa Amerika Latini. * Lakini, wamoja kati yao wamekutana na upinzani juu ya kuchagua kumutumikia Yehova na kukatala desturi zenye hazipatane na maandiko zenye zinapendwa sana fasi kwenye wanaishi. Michango yenye unatoa inatumiwa namna gani juu ya kuwasaidia?

Imewasaidia Kurudia Kwao

 Mu inchi ya Meksiko, ndugu na dada zetu wa jamii ya Huichol katika milima ya Jimbo ya Jalisco walikatala kwa heshima kushiriki mu desturi za kidini zenye zinapingana na mambo yenye Biblia inasema. * Lakini ile ilifanya watu fulani wawakasirikie. Tarehe 4, Mwezi wa 12, 2017, watu fulani wenye jeuri walishambulia kikundi ya Mashahidi wa Yehova na wengine wengi wenye walikuwa pamoya nao. Wale watu wenye jeuri waliwafukuza mu ile eneo, waliharibu nyumba zao, na waliwaogopesha kama wataua kila mutu mwenye atajaribu kurudia.

 Mashahidi wenye walikuwa mu miji ya karibu walihangaikia mahitaji ya kwanza-kwanza ya ndugu na dada zetu. Lakini iliomba nini juu ndugu zetu waweze kurudia kwao? Ndugu mwenye kuitwa Agustin anasema hivi: “Hatukukuwa na makuta ya kulipa mwanasheria wa kututetea ku tribinali, na hatukujua tuombe mashauri kwa nani kuhusu mambo ya sheria.”

 Juu ndugu zetu hawakukuwa huru kumuabudu Yehova, Tawi ya Amerika ya Kati ilichukua hatua bila kukawia. Kwanza, iliomba wakubwa wa serikali wafanye uchunguzi juu ya ile jambo. Kisha, Idara ya Waratibu ya Baraza Yenye Kuongoza ya Mashahidi wa Yehova iliwaruhusu kutumika na Idara ya Kisheria ya Makao Makubwa, na iliwaruhusu kupeleka ile mambo ku tribinali kwa ajili ya ndugu na dada zetu wa jamii ya Huichol. Kwa hiyo, mambo ilifika ku Tribinali Kubwa ya Meksiko.

 Kikundi ya wanasheria wa inchi mbalimbali walitayarisha mawazo yenye kuwa wazi yenye ilionyesha kama sawa vile wengine wanapaswa kuheshimia desturi za wenyeji, wenyeji pia wanapaswa kuheshimia na kulinda desturi zao. Wanadamu wote, ikuwe wanaishi wapi, wako na haki fulani zenye zinapaswa kuheshimiwa.

 Tarehe 8, Mwezi wa 7, 2020, Tribinali Kubwa ya Meksiko ilipatia Mashahidi wa Yehova sheria. Ilisema kama wale wote wenye walikuwa wamefukuzwa walipaswa kuruhusiwa kurudia kwao. Agustín, mwenye tulishazungumuzia, anaonyesha shukrani yake na ya wengine kwa kusema hivi: “Tuko wenye shukrani na wenye furaha sana juu ya mambo yenye ndugu wametufanyia. Kama hawangetusaidia, hatungeweza kitu.”

“Mambo Mingi Sana Kwa Ajili ya Watu Kidogo Sana”

 Ile wakati, ndugu zetu mu San Juan de Ilumán, kijiji fulani mu inchi ya Ecuador kwenye wenyeji wengi wa Bonde ya Otavalo wanaishi, walipambana pia na upinzani. Mu 2014, kisha kupata dokima zote za kuwaruhusu kujenga, walianza kujenga Jumba ya Ufalme. Lakini, padri fulani alikuya na kikundi ya watu zaidi ya 100 na akalazimisha ndugu waache kujenga. Kisha, waliambia Mashahidi wa Yehova waache kukusanyika.

 Idara ya Kisheria ya tawi ya Ecuador na ya Makao Makubwa zilitumika pamoya ili kutetea ile kutaniko yenye haikukuwa tena na uhuru wa kumuabudu Yehova. Ndugu zetu walipeleka mambo ku tribinali. Ile ilifanya watu waache kuwapinga, na kutaniko iliruhusiwa kuanza tena kukusanyika na kumaliza kujenga Jumba ya Ufalme. Lakini, juu ya kulinda haki za ndugu zetu mu wakati yenye kuya, wenye kututetea waliomba Tribinali Kubwa itoe uamuzi wake kuhusu hii ulizo ya maana sana: Wenyeji wanapaswa kuheshimia haki za kila mwanadamu hata aishi wapi?

 Tarehe 16, Mwezi wa 7, 2020 Tribinali ya Kikatiba ya Ecuador, Tribinali Kubwa ya Ecuador, ilisikiliza kesi yetu. Ndugu wenye kuwa wanasheria mu Ecuador waliwakilisha kutaniko. Zaidi ya ile, ndugu zetu ine wenye kuwa na uzoefu mu haki za kimataifa walitutetea ku tribinali. Juu ya vizuizi vya ugonjwa wa Coronavirus, walizungumuza na wako mu inchi zao kupitia vidéoconférence. Njo mara ya kwanza yenye tribinali imeruhusu wanasheria wenye kuwakilisha Mashahidi wa Yehova mu dunia yote wasambe kupitia vidéoconférence. * Wale wanasheria, walizungumuzia haki za kimataifa zenye kuonyesha kama wenyeji hawapaswe kunyanganywa haki zao juu tu wao ni wenyeji.

Kupitia vidéoconférence, wanasheria wa inchi mbalimbali walitetea haki za ndugu zetu

Ndugu zetu mu Bonde ya Otavalo wako nachunga kwa hamu uamuzi wa  Tribinali ya Kikatiba. Na wameguswa sana na musaada wenye walipewa. César, muzee mu kutaniko ya Ilumán Quichua, anasema hivi: “Ni Yehova tu, kupitia tengenezo yake, njo anaweza kufanya mambo mingi sana kwa ajili ya watu kidogo sana.”

 Wanasheria wote wenye wako nasaidia mu ile kesi ni Mashahidi wa Yehova, na wanafurahia kutumia uzoefu wao bila kulipwa. Lakini, inaomba wakati na makuta ili kupeleka mambo ku tribinali, kujitayarisha ili kusamba, na kusamba ku tribinali. Wanasheria wetu na ndugu wengine walitumia saa zaidi ya 380 juu ya kutayarisha namna watasamba, na saa zingine 240 juu ya kutafsiri dokima zenye zinahusu mambo ya Meksiko. Karibu wanasheria 40 mu dunia yote walipitisha saa za mingi sana mu mambo ya Ecuador. Nini njo imetusaidia kulipia garama zenye zilihusu kutetea ndugu zetu? Ni michango yenye umetoa kwa kutumia njia mbalimbali zenye kuonyeshwa ku donate.mt711.com. Aksanti sana kwa ukarimu wako.

^ Mashahidi wa Yehova wanatafsiri pia vichapo vyao mu luga zingine za mingi za Amerika Latini na mu luga za ishara zenye kutumiwa tu mu ile eneo.

^ Watu wa jamii ya Huichol wanajulikana pia kwa jina ya Wixáritari, na mara mingi luga yao inaitwa Wixárika.

^ Hata kama tengenezo yetu ya mu dunia yote haikukuwa mu ile kesi, waamuzi waliruhusu ndugu zetu waende ku tribinali sawa vile “rafiki wa tribinali.”