Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

NAMNA MICHANGO YAKO INATUMIWA

Kutolewa kwa Kitabu cha Maana Sana Kuliko Vitabu Vyote

Kutolewa kwa Kitabu cha Maana Sana Kuliko Vitabu Vyote

TAREHE 1 MWEZI WA 1, 2021

 “Nimeingojea kwa muda murefu, miaka 19!” Ule ndugu yetu alikuwa anangojea nini? Tafsiri ya Ulimwengu Mupya ya Maandiko ya Kigiriki mu luga yao, Kibengali. Watu wengi wanasema vile wakati Tafsiri ya Ulimwengu Mupya inatolewa mu luga yao. Lakini, unajua inaomba nini juu ya kutafsiri zile Biblia na kuzichapisha?

 Kwanza, ule mugao unapewa timu ya ndugu na dada chini ya uongozi wa Halmashauri ya Uandikaji ya Baraza Lenye Kuongoza. Ile kazi inachukua ile timu wakati gani? Ndugu Nicholas Ahladis, mwenye anatumikaka na Departema za Kutafsiri kule Warwick, New York, anafasiria hivi: “Ile kazi inatia ndani mambo mingi kama vile: Ni watafsiri ngapi wamepatikana juu ya kufanya ile kazi? Ile luga iko na mambo gani ya pekee? Wasomaji wa ile luga wanajua kwa kadiri gani namna maisha ya watu wenye waliishi wakati Biblia ilikuwa? Je, ile luga inazungumuziwa tofauti-tofauti kulingana na maeneo? Kwa kukadiria, timu inafanya mwaka moja kufikia miaka tatu juu ya kutafsiri tu Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo na miaka ine ao zaidi juu ya kutafsiri Biblia yote. Ile kazi inaweza kufanya miaka mingi sana kama ni kutafsiri Biblia mu luga ya ishara.”

 Haiko tu watafsiri njo wanahitajiwa. Kuko pia lazima ya kuwa na wasomaji wa inje wa miaka na mahali tofauti-tofauti, na wakati fulani hata wa inchi mbalimbali. Wanasoma kazi yenye watafsiri walifanya, kisha wanatoa maoni yao na wanafanya vile bila kulipiwa. Mawazo yenye wanatoa inasaidia Biblia ikuwe bila makosa, ikuwe wazi na ieleweke muzuri. Na kama vile ndugu moja wa Afrika ya Kusini mwenye kuzoeza watafsiri wa Biblia alisema, “watafsiri wanaona ile kazi kuwa daraka nzito yenye wako nayo mbele ya Yehova na wasomaji wa Neno lake.”

 Kisha kumaliza kazi ya kutafsiri, Biblia inapaswa kuchapishwa na kuunganishwa. Juu ile iwezekane, wachapishaji wanatumia vitu mbalimbali karibu kumi: karatasi, wino, karatasi za kufanya jalada, vitu vyenye kunata, muchanganyiko wa kusaidia kupata majalada mepesi, karatasi za feza, tepe ao rubans, bandeaux, vitu vyenye kusaidia Biblia ifungiwe nguvu, na vya kusaidia iunganishwe pamoja. Mu 2019, zaidi ya dola milioni 20 ilitumiwa juu tu ya kupata vile vitu vya kusaidia Biblia ichapishwe. Ndugu na dada wenye kufanya ile kazi walifanya ma saa zaidi ya 300 000 mu ile mwaka juu ya kuchapisha na kusafirisha Biblia.

“Biblia njo kitabu ya maana sana kati ya vitabu vyote vyenye tunachapishaka”

 Juu ya nini kupitisha ile wakati yote na kutumia ile feza yote juu tu ya ile kazi? Ndugu Joel Blue wa Departema ya Uchapishaji alisema: “Biblia njo kitabu ya maana sana kati ya vitabu vyote vyenye tunachapishaka. Kwa hiyo, tunapenda ikuwe na umbo ya muzuri juu itukuze Mungu mwenye tunaabudu na ujumbe wenye tunahubiri.”

 Hatuchapishe tu Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mupya za kawaida, tunachapisha pia Biblia kwa ajili ya wasomaji wenye kuwa na uhitaji wa pekee. Kwa mufano, Tafsiri ya Ulimwengu Mupya kwa ajili ya vipofu inapatikana mu luga kumi. Kuchapisha Biblia moja ya vipofu inaweza kukamata saa munane, na sehemu zake zote zinaweza kuenea fasi ya metre 2,3. Tunachapisha pia Biblia zingine za pekee kwa ajili ya wafungwa mu magereza kwenye vitabu tu vyenye havina majalada ya nguvu-nguvu njo vinakubaliwa kuingizwa.

 Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mupya iko na matokeo ya muzuri juu ya maisha ya wasomaji wake. Tuzungumuzie kutaniko la luga ya Kiluba lenye kuwa fasi yenye kuitwa Tombe, mu Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Kama unatumia barabara, Tombe iko ku kilometre zaidi ya 1 700 na muji mukubwa wa ile inchi. Mashahidi wa Yehova pale Tombe walikuwa tu na Biblia moja, na ilikuwa mu luga ya Kiluba cha zamani sana. Ni ileile Biblia moja njo ndugu walikuwa wanapatiana juu ya kutayarisha sehemu zao za mikutano. Lakini, kuanzia Mwezi wa 8, 2018, kila mumoja mu kutaniko alikuwa na Biblia yake Tafsiri ya Ulimwengu Mupya mu Kiluba, yote ya muzima.

 Dada moja mwenye kuzungumuza luga ya Kialemanye alisema hivi juu ya Tafsiri ya Ulimwengu Mupya yenye ilirekebishwa mu luga yao: “Sijiulizake tena kama napaswa kusoma Biblia. Lakini, niko najiuliza, ‘wakati gani naweza kusoma sana?’” Mufungwa moja aliandika hivi: “Nilipewa Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mupya, na ikabadilisha maisha yangu. Ile Biblia ilinisaidia nielewe muzuri sana Neno la Mungu. Nilipenda kujua mambo mingi juu ya Mashahidi wa Yehova na namna ya kuwa mumoja wao.”

 Wasomaji wote wa Biblia Tafsiri ya Ulimwengu Mupya wanashukuru sana juu ya michango yenye ilitolewa juu ichapishwe. Hii michango ya kutegemeza kazi ya mu dunia yote, ilitolewa kupitia donate.mt711.com. Aksanti sana kwa roho yenu ya kutoa.