Mambo Yenye Unaweza Kujifunza Katika Biblia

Kitabu hiki kitakusaidia ujifunze historia, kuanzia uumbaji, kuzaliwa na utumishi wa Yesu, mupaka wakati ufalme utakuja.

Barua ya Baraza Lenye Kuongoza

Namna gani tunaweza kutumia hiki kitabu?

SOMO LA 1

Mungu Aliumba Mbingu na Dunia

Biblia inasema kama Mungu aliumba mbingu na dunia. Juu ya nini aliumba kwanza malaika mumoja mbele ya kuumba kila mutu na kila kitu?

SOMO LA 2

Mungu Aliumba Mwanaume na Mwanamuke wa Kwanza

Mungu aliumba mwanaume na mwanamuke wa kwanza na akawatia mu bustani ya Edeni. Alitaka waanzishe familia na wafanye dunia yote ikuwe paradiso.

SOMO LA 3

Adamu na Eva Wanakataa Kumutii Mungu

Juu ya nini muti moja ya mu bustani ya Edeni ilikuwa ya pekee? Juu ya nini Eva alikula tunda ya ile muti?

SOMO LA 4

Aliua Mudogo Wake Juu ya Kasirani

Mungu aliitika zabihu ya Abeli lakini alikataa zabihu ya Kaini. Wakati Kaini aliona vile, alikasirika sana na akafanya jambo la mubaya sana.

SOMA LA 5

Safina ya Noa

Wakati malaika wenye walifanya zambi walikuja ku dunia na kuoa wanamuke, walizaa watoto wenye walikuwa na nguvu sana. Mambo ya mubaya ilienea fasi yote. Lakini Noa alikuwa tofauti​​—alipenda Mungu na alimutii.

SOMO LA 6

Watu Munane Waliokoka Garika

Mvua ilinyesha mu siku 40 muchana na usiku. Noa na familia yake walibakia ndani ya safina zaidi ya mwaka moja. Kisha, Mungu aliwaambia watoke katika safina.

SOMO LA 7

Munara wa Babeli

Watu waliamua kujenga muji na munara wenye kufika mupaka mbinguni. Juu ya nini Mungu alifanya waseme luga za kuachana?

SOMO LA 8

Abrahamu na Sara Walimutii Mungu

Juu ya nini Abrahamu na Sara waliacha maisha yao ya muzuri na kuhamia mu inchi ya Kanaani?

SOMO LA 9

Wanapata Sasa Mutoto!

Namna gani Mungu alitimiza mambo yenye aliambia Abrahamu? Angefanya vile kupitia mutoto gani wa Abrahamu, Isaka ao Ishmaeli?

SOMO LA 10

Mukumbuke Bibi ya Loti

Mungu alifanya mvua ya moto na kiberiti inyeshe mu miji ya Sodoma na Gomora. Juu ya nini ile miji iliharibiwa? Juu ya nini tunapaswa kukumbuka bibi ya Loti?

SOMO LA 11

Imani Yake Inajaribiwa

Mungu aliambia Abrahamu: ‘Tafazali, ukamate mutoto wako wa pekee na umutoe zabihu ku mulima katika Moria.’ Namna gani Abrahamu alitenda mbele ya jaribu hilo la imani?

SOMO LA 12

Yakobo Alipata Uriti

Isaka na Rebeka walikuwa na watoto mapasa, Esau na Yakobo. Esau alizaliwa wa kwanza na yeye njo alipaswa kuwa na haki ya uriti. Juu ya nini aliuzisha ile haki kwa chakula?

SOMO LA 13

Yakobo na Esau Wanasikilizana

Namna gani malaika alimubariki Yakobo? Yakobo alifanya nini ili asikilizane na Esau?

SOMO LA 14

Mutumwa Mwenye Alimutii Mungu

Yosefu alifanya mambo ya muzuri, lakini aliteseka sana. Juu ya nini?

SOMO LA 15

Yehova Hakumusahau Yosefu Hata Kidogo

Hata kama Yosefu alikuwa mbali na familia yao, Mungu alimuonyesha kama alikuwa pamoja naye.

SOMO LA 16

Yobu Alikuwa Nani?

Alimutii Yehova hata wakati ilikuwa nguvu kufanya vile.

SOMO LA 17

Musa Alichagua Kumuabudu Yehova

Wakati alikuwa mutoto, Musa aliokolewa kwa sababu ya hekima ya mama yake.

SOMA LA 18

Muti Mudogo Unawaka Moto

Juu ya nini moto haukuunguza ule muti?

SOMO LA 19

Mapigo Tatu ya Kwanza

Farao aliletea watu wake matatizo juu kiburi kilifanya akatae kufanya jambo moja tu.

SOMO LA 20

Mapigo Ingine Sita

Namna gani hii mapigo ilikuwa tofauti na mapigo tatu ya kwanza?

SOMA LA 21

Pigo ya Kumi

Hii pigo ilikuwa mubaya sana na ilifanya Farao mwenye kiburi aache Waisraeli waende.

SOMO LA 22

Muujiza ku Bahari Nyekundu

Farao alipona wakati wa ile mapigo kumi, lakini je, aliokoka muujiza huu wa Mungu?

SOMO LA 23

Waisraeli Wanamutolea Yehova Ahadi

Waisraeli walimutolea Mungu ahadi ya pekee wakati walitia kambi ku Mulima Sinai.

SOMO LA 24

Walishindwa Kutimiza Ahadi Yao

Wakati Mungu alikuwa anapatia Musa zile Amri Kumi, watu walikuwa wanatenda zambi nzito sana.

SOMA LA 25

Wanajenga Tabenakulo

Mu ile hema ya pekee mulikuwa sanduku ya agano.

Wapelelezi 12

Namna gani ripoti ya Yoshua na Kalebu ilikuwa tofauti na ya wale wapelelezi wengine kumi wenye walipeleleza inchi ya Kanaani.

SOMO LA 27

Walimuasi Yehova

Kora, Datani, Abiramu, na wanaume wengine 250 walikosa kutambua jambo fulani La maana kumuhusu Yehova.

SOMO LA 28

Punda ya Balaamu Inasema

Punda iliona mutu fulani mwenye Balaamu hakuona.

SOMO LA 29

Yehova Alichagua Yoshua

Mungu alipatia Yoshua maagizo yenye inaweza kutusaidia leo.

SOMO LA 30

Rahabu Alificha Wapelelezi

Kuta za Yeriko zilianguka. Lakini nyumba ya Rahabu haikuanguka, hata kama ilikuwa imejengwa ku ukuta.

SOMO LA 31

Yoshua na Wagibeoni

Yoshua alisali kwa Mungu na kusema: “Jua, simama bila kutikisika!” Je, Mungu alijibu?

SOMO LA 32

Kiongozi Mupya na Wanamuke Mbili Wenye Uhodari

Kisha Yoshua kufa, Waisraeli walianza kuabudu sanamu. Maisha ilikuwa nguvu, lakini Yehova aliwasaidia kupitia muamuzi Baraka, nabii mwanamuke Debora, na Yaeli!

SOMO LA 33

Rutu na Naomi

Wanamuke wawili wenye bwana zao walikufa walirudia Israeli. Rutu, mumoja kati ya wale wanamuke, alienda kufanya kazi mu shamba, na kule Boazi akamuona.

SOMO LA 34

Gideoni Alishinda Wamidiani

Kisha Wamidiani kutesa Waisraeli, watu walianza kumulilia Yehova awasaidie. Namna gani maaskari kidogo wa Gideoni waliweza kushinda maaskari 135000 Wamidiani?

SOMO LA 35

Hana Anasali Apate Mutoto Mwanaume

Elkana, Hana, Penina, na watoto wao walienda kuabudu ku tabenakulo kule Shilo. Wakati wako kule, Hana anasali apate mutoto. Mwaka wa kufuata, Samweli anazaliwa!

SOMO LA 36

Ahadi ya Yefta

Yefta alitoa ahadi gani, na juu ya nini? Binti ya Yefta alifanya nini kisha kujua ahadi ya baba yake?

SOMO LA 37

Yehova Anazungumuza na Samweli

Kuhani Mukubwa Eli alikuwa na watoto mbili wanaume wenye walikuwa makuhani ku tabenakulo, lakini hawakutii sheria za Yehova. Kijana Samweli hakukuwa vile, na Yehova alizungumuza naye.

SOMO LA 38

Yehova Alipatia Samsoni Nguvu

Mungu alipatia Samsoni nguvu mingi juu apigane na Wafilisti, lakini wakati Samsoni alikamata uamuzi wa mubaya, Wafilisti walimukamata.

SOMA LA 39

Mufalme wa Kwanza wa Israeli

Yehova alikuwa amepatia Waisraeli waamuzi wa kuwaongoza, lakini wao waliomba wakuwe na mufalme. Samweli alitia Sauli mafuta juu akuwe mufalme wa kwanza wa Israeli, lakini kisha wakati fulani Yehova alikataa Sauli. Juu ya nini?

SOMO LA 40

Daudi na Goliati

Yehova anachagua Daudi akuwe mufalme wa pili wa Israeli, na Daudi anaonyesha juu ya nini alistahili kuchaguliwa.

SOMO LA 41

Daudi na Sauli

Juu ya nini mwanaume mumoja alichukia mwenzake, na ule mwenye alichukiwa alitenda namna gani?

SOMO LA 42

Yonatani Alikuwa Hodari na Mushikamanifu

Mutoto wa mufalme alikuwa rafiki wa sana wa Daudi.

SOMO LA 43

Zambi ya Mufalme Daudi

Uamuzi wa mubaya unaleta magumu mingi sana.

SOMO LA 44

Sulemani Anajengea Yehova Hekalu

Mungu alikubali ombi la Mufalme Sulemani na alimupatia mapendeleo makubwa.

SOMO LA 45

Ufalme Unagawanyika

Waisraeli mingi wanaacha kumuabudu Yehova.

SOMO LA 46

Mambo Yenye Ilifanyika Kwenye Mulima Karmeli

Nani njo Mungu wa kweli? Yehova ao Baali?

SOMO LA 47

Yehova Alitia Eliya Moyo

Unawaza kama anaweza kukutia moyo na wewe?

SOMO LA 48

Mutoto wa Mujane Anafufuliwa

Miujiza mbili mu nyumba ileile!

SOMO LA 49

Malkia Muovu Anapata Malipizi

Yezebeli anafanya mipango ya mubaya ya kumuua Naboti juu amunyanganye shamba lake la mizabibu! Yehova Mungu anaona uovu wa Yezebeli na tendo lake la kukosa haki.

SOMO LA 50

Yehova Anasaidia Yehoshafati

Yehoshafati mufalme muzuri anasali kwa Mungu wakati mataifa adui inaogopesha Yuda.

SOMO LA 51

Mupiganaji-vita na Mutoto Mudogo Mwanamuke

Mutoto mwanamuke Mwisraeli alielezea bibi ya bwana mukubwa wake kuhusu nguvu za Yehova, na Naamani aliponyeshwa kwa njia ya muujiza.

SOMO LA 52

Jeshi la Yehova Lenye Farasi na Magari ya Vita ya Moto

Namna mutumishi wa Elisha aliona kwamba ‘wale wenye kuwa pamoja na sisi ni wengi kuliko wale wenye kuwa pamoja nao.’

SOMO LA 53

Yehoyada Anatenda kwa Uhodari

Kuhani muaminifu anapinga malkia muovu.

SOMO LA 54

Yehova Alivumilia Yona

Ni jambo gani lilifanya nabii mumoja wa Mungu amezwe na samaki kubwa? Namna gani alitoka mu tumbo la ile samaki? Na Yehova alimufundisha nini?

SOMO LA 55

Malaika wa Yehova Alilinda Hezekia

Maadui wa Yuda walisema kama Yehova hatalinda watu wake, lakini walijidanganya!

SOMO LA 56

Yosia Alipenda Sheria ya Mungu

Yosia aliwekwa kuwa mufalme wakati alikuwa na miaka munane, na alisaidia watu wake wamuabudu Yehova.

SOMO LA 57

Yehova Anatuma Yeremia Aende Kuhubiri

Mambo yenye huyu nabii kijana alisema iliwafanya wazee wa Yuda wakasirike sana.

SOMO LA 58

Yerusalemu Inaharibiwa

Watu wa Yuda waliendelea kuabudu miungu ya uongo, njo maana Yehova aliwaacha.

SOMO LA 59

Vijana Ine Wenye Walimutii Yehova

Vijana Wayudea waliazimia kubakia waaminifu kwa Yehova hata wakati walikuwa mu nyumba ya mufalme kule Babiloni.

SOMO LA 60

Ufalme Wenye Utaendelea Milele

Danieli anafasiria maana ya ndoto ya kushangaza ya Nebukadneza.

SOMO LA 61

Walikataa Kuinamia Sanamu

Shadraki, Meshaki, na Abednego wanakataa kuabudu sanamu ya zahabu ya mufalme wa Babiloni.

SOMO LA 62

Ufalme Wenye Uko Sawa Muti Mukubwa

Ndoto ya Nebukadneza inaonyesha mambo yenye itamupata.

SOMO LA 63

Maneno Inaandikwa Kwenye Ukuta

Maneno yenye haieleweke inaandikwa ku ukuta wakati gani, na inamaanisha nini?

SOMO LA 64

Danieli Anatupwa Ndani ya Shimo la Simba

Ukuwe unasali kwa Yehova kila siku, sawa vile Danieli alikuwa anafanya!

SOMO LA 65

Esta Anaokoa Watu Wake

Hata kama alikuwa yatima kutoka inchi ingine, alifikia kuwa malkia.

SOMO LA 66

Ezra Alifundisha Watu Sheria ya Mungu

Kisha Waisraeli kumusikiliza Ezra, walimutolea Mungu ahadi fulani ya pekee.

SOMO LA 67

Kuta za Yerusalemu

Wakati Nehemia alivumbua kama maadui wake walitaka kuwashambulia, juu ya nini hakuogopa?

SOMO LA 68

Elizabeti Anakuwa na Mutoto

Juu ya nini bwana ya Elizabeti aliambiwa kwamba hangeweza tena kusema mupaka wakati mutoto atazaliwa?

SOMO LA 69

Gabrieli Anatembelea Maria

Alimupatia ujumbe wenye ulibadilisha maisha yake.

SOMO LA 70

Malaika Wanatangaza Kama Yesu Amezaliwa

Wachungaji wenye walisikia ile tangazo walitenda haraka.

SOMO LA 71

Yehova Alimulinda Yesu

Mufalme muovu alitaka kuua Yesu.

SOMO LA 72

Wakati Yesu Alikuwa na Miaka 12

Namna gani Yesu alishangaza walimu mu hekalu?

SOMO LA 73

Yohana Anatayarisha Kuja kwa Masiya

Wakati Yohana alikomaa, akakuwa nabii. Alifundisha kama Masiya anakaribia kuja. Watu walifanya nini wakati walisikia mafundisho yake?

SOMO LA 74

Yesu Anakuwa Masiya

Yohana anamaanisha nini wakati anasema kama Yesu njo Mwana-Kondoo wa Mungu?

SOMO LA 75

Ibilisi Anamujaribu Yesu

Ibilisi anamujaribu Yesu mara tatu. Anamujaribu namna gani? Yesu anatenda namna gani?

SOMO LA 76

Yesu Anasafisha Hekalu

Juu ya nini Yesu anafukuza wanyama inje ya hekalu na kupindua meza za wenye wako wanabadilisha feza?

SOMO LA 77

Mwanamuke Kwenye Kisima

Mwanamuke Musamaria anashangaa wakati Yesu anazungumuza naye. Juu ya nini? Yesu anamuambia jambo gani lenye alikuwa hajaambiaka mutu mwingine?

SOMO LA 78

Yesu Anahubiri Habari ya Ufalme

Yesu anaalika wanafunzi wake fulani wakuwe ‘wavuvi wa watu.’ Kisha, anachagua wafuasi 70 ili wahubiri habari njema.

SOMO LA 79

Yesu Anafanya Miujiza Mingi

Kila fasi kwenye Yesu anaenda, wagonjwa wanakuja kumuona juu awasaidie, na anawaponyesha. Hata anamufufua mutoto mwanamuke.

SOMO LA 80

Yesu Anachagua Mitume 12

Juu ya nini Yesu anawachagua? Unakumbuka majina yao?

SOMO LA 81

Mahubiri Kwenye Mulima

Yesu anafundisha watu mingi wenye walikusanyika pembeni ya mulima mambo ya maana sana.

SOMO LA 82

Yesu Anafundisha Wanafunzi Wake Namna ya Kusali

Yesu anawaambia wanafunzi wake waendelee kuomba mambo gani?

SOMO LA 83

Yesu Anakulisha Maelfu ya Watu

Huu muujiza unatufundisha nini juu ya Yehova na Yesu?

SOMO LA 84

Yesu Anatembea Juu ya Maji

Unaweza kuwazia namna mitume wanajisikia wakati wanaona ule muujiza?

SOMO LA 85

Yesu Anaponyesha Mutu Siku ya Sabato

Juu ya nini haiko watu wote njo wanafurahia mambo yenye Yesu iko anafanya?

SOMO LA 86

Yesu Anamufufua Lazaro

Wakati Yesu anaona namna Maria iko analia, yeye pia anaanza kulia. Lakini huzuni yao iligeuka kuwa furaha.

SOMO LA 87

Pasaka ya Mwisho ya Yesu

Yesu anapatia mitume wake maagizo ya maana wakati iko anakula chakula pamoja nao kwa mara ya mwisho.

SOMO LA 88

Yesu Anakamatwa

Yuda Iskariote anaongoza watu mingi wenye wako na fimbo na mipanga juu wamukamate Yesu.

SOMO LA 89

Petro Anamukana Yesu

Ni nini ilifanyika mu kiwanja cha nyumba ya Kayafa? Namna gani walitendea Yesu ndani ya nyumba?

SOMO LA 90

Yesu Anakufa Kule Golgota

Juu ya nini Pilato anaruhusu Yesu auawe?

SOMO YA 91

Yesu Anafufuliwa

Ni mambo gani ya kufurahisha ilitokea kisha Yesu kuuawa?

SOMO LA 92

Yesu Anawatokea Wavuvi

Anafanya nini ili wamutambue?

SOMO LA 93

Yesu Anarudia Mbinguni

Lakini mbele ya kurudia, anapatia wanafunzi wake maagizo fulani ya maana sana.

SOMO LA 94

Wanafunzi Wanapokea Roho Takatifu

Roho takatifu iliwapatia nguvu gani kwa njia ya muujiza?

SOMO LA 95

Hakuna Kitu Kingeweza Kuwazuia Kuhubiri

Viongozi wa dini wenye walifanya Yesu auawe, wanajaribu sasa kunyamazisha wanafunzi. Lakini hawawezi.

SOMO LA 96

Yesu Anamuchagua Sauli

Sauli ni adui wa sana wa Wakristo, lakini iko karibu kubadilika.

SOMO LA 97

Kornelio Anapokea Roho Takatifu

Juu ya nini Mungu anamutuma Petro ku nyumba ya ule mwanaume , mwenye haiko Muyahudi?

SOMO LA 98

Ukristo Unaenea Katika Mataifa Mingi

Mutume Paulo na wamisionere wenzake wanaanza kuhubiri mu maeneo ya mbali.

SOMO LA 99

Mulinzi wa Gereza Anajifunza Kweli

Hii hadisi inahusu namna gani pepo muchafu, tetemeko la inchi, na upanga?

SOMO LA 100

Paulo na Timoteo

Wale wanaume wawili wanatumika pamoja, na walikuwa marafiki kwa miaka mingi.

SOMO LA 101

Paulo Anapelekwa Roma

Safari imejaa hatari, lakini hakuna tatizo lenye linaweza kumuzuia huyu mutume.

SOMO LA 102

Yohana Anapokea Ufunuo

Yesu anamuonyesha Yohana maono mingi juu ya wakati wenye kuja.

SOMO LA 103

‘Ufalme Wako Ukuje’

Ufunuo wenye Yohana alipewa unaonyesha namna Ufalme wa Mungu utabadilisha maisha ku dunia.