Ona video zinazopatikana

BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

“Sasa Sisikie Tena Haya”

“Sasa Sisikie Tena Haya”
  • Alizaliwa Mwaka wa: 1963

  • Inchi: Mexico

  • Alikuwa: Mutoto wa mu barabara; alikuwa anajiona kuwa wa bure

MAISHA YANGU YA ZAMANI

 Nilizaliwa Ciudad Obregón kaskazini mwa Mexico; niko wa tano mu familia ya watoto kenda. Tulikuwa tunaishi pembeni ya muji, kwenye baba yangu alikuwa na shamba. Ilikuwa fasi ya muzuri ya kuishi, familia yetu ilikuwa na umoja na ilikuwa yenye furaha. Kwa kuhuzunisha, wakati nilikuwa na miaka tano, upepo mukali uliharibisha shamba letu na tukalazimika kuhamia katika muji mwingine.

 Baba yangu alianza kupata feza mingi. Lakini wakati uleule, akakuwa mulevi. Ile ilivuruga ndoa yake na ikatuletea sisi watoto wake matatizo. Tulianza kuvuta tumbako, yenye tulikuwa tunamuiba baba yetu. Wakati nilikuwa tu na miaka sita, nililewa kwa mara ya kwanza. Muda kidogo tu kisha pale, wazazi wangu wakaachana na nikaendelea kuwa na tabia za mubaya sana.

 Mama yetu alienda kuishi na mwanaume mwingine na akatupeleka kule. Ule mwanaume hakumupatia feza, na mama hakukuwa anapata feza mingi ili kututegemeza. Kwa hiyo, mimi na ndugu zangu tulifanya kazi zenye tulikuwa na uwezo wa kufanya, lakini tulikuwa tunapata kwa shida feza za kutimiza mahitaji yetu ya musingi. Nilikuwa ninasafishia watu viatu na nilikuwa ninauzisha mikate, magazeti ya habari, bazoka, na vitu vingine. Nilikuwa pia ninatembea mu barabara ili kutafuta chakula ku yalala za matajiri.

 Wakati nilikuwa na miaka kumi, mwanaume mumoja aliniomba nitumike naye nafasi kwenye watu walikuwa wanatupa uchafu wa muji. Nilikubali, nikaacha masomo, na nikatoka ku nyumba. Kila siku alinilipa feza yenye haienee dola moja na alinipatia chakula chenye kiliokotwa ku yalala. Niliishi katika nyumba yenye nilijenga na vitu mbalimbali vyenye niliokota ku yalala. Watu wenye niliishi nao walizoea kutumia maneno machafu na walikuwa waasherati. Wengi walikuwa watumwa wa dawa za kulewesha na walevi. Ile ilikuwa wakati mubaya katika maisha yangu, na nilikuwa ninalia kila usiku, nilitetemeka kwa woga. Kwa sababu nilikuwa maskini na sikusoma mingi, nilikuwa ninasikia haya sana. Niliishi mu ile eneo ya kutupia uchafu karibu miaka tatu, kisha nikahamia katika jimbo lingine la Mexico. Kule nilitumika katika mashamba, nilikuwa ninachuma maua na pamba, kukusanya miwa, na kuvuna viazi.

Niliishi miaka tatu nafasi ya kutupia uchafu kama hii

 Kisha miaka ine, nikarudia Ciudad Obregón. Shangazi yangu mumoja, mwenye alikuwa mufumu, alinipatia chumba katika nyumba yake. Nilianza kuota ndoto zenye kuogopesha, nilishuka moyo na nikafikia kuwa na mawazo ya kujiua. Usiku moja nilisali hivi kwa Mungu: “Bwana, kama uko, ninapenda nikujue, na nitakutumikia maisha yote. Kama kuko dini ya kweli, ninapenda niijue.”

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU

 Nilikuwa ninapenda sana kujifunza juu ya Mungu. Wakati nilikuwa ningali mutoto, nilienda ku makanisa mbalimbali, lakini yote ilinivunja moyo. Kati ya ile makanisa yote, hakuna hata moja yenye ilikuwa inazungumuzia Biblia ao yenye ilinisaidia kutimiza tamaa yangu ya kumujua Mungu. Dini fulani zilihangaikia sana feza, na viongozi wa dini zingine walikuwa waasherati.

 Wakati nilikuwa na miaka 19, bwana wa dada yangu mumoja, aliniambia kama Mashahidi wa Yehova walimuonyesha mambo yenye Biblia inasema juu ya kutumia sanamu katika ibada. Alinisomea Kutoka 20:4, 5. Inasema kama hatupaswe kufanya sanamu ya kuchongwa. Mustari wa 5 unasema: “Haupaswe kuviinamia wala kushawishiwa kuvitumikia, kwa sababu mimi, Yehova Mungu wako, ni Mungu mwenye anataka watu washikamane na yeye tu.” Kisha bwana wa dada yangu akaniuliza, “Kama Mungu anatumia sanamu ili kufanya miujiza ao kama anapenda tuzitumie katika ibada, juu ya nini anazikataza?” Ile ilinifanya nifikiri sana. Kisha, tulikuwa na mazungumuzo mingi yenye kutegemea Biblia. Kwa sababu nilifurahia sana ile mazungumuzo, ilionekana kama vile wakati ulipita haraka.

 Kisha, alinipeleka ku mukutano wa Mashahidi wa Yehova. Nilifurahishwa sana na mambo yenye niliona na kusikia kule. Hata vijana walishiriki katika programu, na walisema muzuri ku jukwaa (estrade)! Nilijiambia hivi: ‘Watu hawa wako wanapata elimu ya muzuri hapa!’ Hata kama nilikuwa na nywele ndefu na nilikuwa muchafu, Mashahidi wa Yehova walinikaribisha kwa uchangamufu. Familia moja ilinialika kwa ajili ya chakula cha mangaribi kisha mukutano!

 Kupitia funzo langu la Biblia pamoja na Mashahidi, nilijifunza kuwa Yehova ni Mungu mwenye upendo na anatuhangaikia bila kuangalia uwezo wetu wa kifeza, hali yetu ya maisha, kabila yetu, ao elimu yenye tumepata. Kwa kweli, Mungu hana ubaguzi. (Matendo 10:34, 35) Ku mwisho, nilitimiza tamaa yenye nilikuwa nayo ya kumujua Mungu. Sikujisikia tena kuwa ninakosa kitu fulani cha maana mu maisha.

FAIDA YENYE NIMEPATA

 Maisha yangu yote ilianza kubadilika sana na ikakuwa ya muzuri! Niliacha kuvuta tumbako, kutumia pombe sana, na kutumia maneno machafu. Uchungu wenye nilikuwa nao wakati nilikuwa mutoto ulianza kupotea na sikukuwa ninaota tena ndoto zenye kuogopesha. Pia, sikujiona tena kuwa mutu wa bure, kama vile nilikuwa ninajisikia juu ya magumu yenye nilipata wakati nilikuwa mutoto na juu sikusoma mingi.

 Niko na bibi muzuri sana mwenye kumupenda Yehova na ananitegemeza sana. Kwa sasa ninatumika kama mwangalizi mwenye kusafiri wa Mashahidi wa Yehova, na nitatembelea makutaniko ili kutia moyo na kufundisha waabudu wenzangu wenye wako kama ndugu na dada zangu. Kwa musaada wa Biblia na mafundisho ya muzuri yenye Mungu anatutolea, sisikie tena haya.

Mimi na bibi yangu tunafurahia kusaidia wengine kama vile nilisaidiwa