Ona video zinazopatikana

“Ninafanya Mambo Yenye Ninaweza”

“Ninafanya Mambo Yenye Ninaweza”

 Irma, mwenye anaishi mu inchi ya Ujerumani, iko na miaka karibu 90. Amefanya aksidenti mbili za mubaya sana na amepasuliwa mara mingi, kwa hiyo, hawezi tena kuhubiri nyumba kwa nyumba kama zamani. Sasa, Irma anahubiri kwa kuandikia barua watu wa jamaa yake na watu wengine wenye anajuana nao. Watu wanafurahia barua zenye Irma anawaandikia ili kuwatia moyo na kufariji wale wenye walifiwa, na kwa hiyo, mara mingi wanamuita ili kumuuliza ni wakati gani watapata barua ingine. Anapokea pia barua mingi zenye watu wanamuandikia ili kumushukuru na kumuomba awaandikie tena. Irma anasema hivi: “Ile mambo yote inaniletea furaha na inanipatia nguvu ya kuendelea kuhubiri.”

 Irma anaandikia pia barua watu wenye kuzeeka wenye kuishi mu nyumba za kutunzia wazee. Anasema hivi: “Mwanamuke mumoja mwenye kuzeeka aliniita ku telefone na akaniambia kama barua yangu ilimufariji sana wakati bwana yake alikufa. Anachunga barua hiyo katika Biblia yake na anazoea kuisoma mangaribi. Mwanamuke mwingine, mwenye bwana yake alikufa juzi-juzi, alisema kama barua yangu ilimusaidia sana kupita hotuba ya padri. Alikuwa na maulizo mingi na akaniuliza ikiwa ningependa anitembelee.”

 Mutu mumoja mwenye Irma anajuana naye, mwenye haiko Shahidi, mwenye alikuwa amehamia mbali sana aliomba Irma amuandikie barua. Irma anasema hivi: “Ule mwanamuke aliweka barua zangu zote. Kisha yeye kufa, mutoto wake mwanamuke aliniita ku telefone. Aliniambia kama alikuwa amesoma barua zote zenye niliandikiaka mama yake na akaniuliza ikiwa ningeweza kumuandikia yeye pia barua zenye kuzungumuzia mambo ya Biblia.”

 Irma anafurahia sana kazi yake ya kuhubiri. Anasema hivi: “Ninamuomba Yehova aendelee kunipatia nguvu ya kumutumikia. Hata kama siwezi tena kuhubiri nyumba kwa nyumba, ninafanya mambo yenye ninaweza.”