MACHI 27, 2024
URUSI
Walikuwa na Uhakika, Walijitayarisha, na Walikuwa na Mtazamo Mzuri
Mahakama ya Leninskiy ya Wilaya ya Barnaul iliyo katika Eneo la Altai itatangaza uamuzi wake hivi karibuni katika kesi inayowahusu Ndugu Yuriy Kolotinskiy, Ndugu Mikhail Reshetnikov, na Ndugu Anatoliy Sarychev. Mwendesha mashtaka bado hajatoa ombi la hukumu anayopendekeza.
Maelezo Mafupi Kuwahusu
Tunafurahi sana kuwa na ndugu kama hawa, ambao ni mifano mizuri ya imani na kumtegemea Yehova katika siku zetu. Tuna uhakika kwamba wataendelea kunufaika na upendo mshikamanifu wa Yehova na uaminifu.—Zaburi 25:10.
Mfuatano wa Matukio
Mei 25, 2021
Kesi ya uhalifu ilifunguliwa dhidi ya Mikhail
Mei 27, 2021
Nyumba ya Mikhail ilifanyiwa msako. Yeye na Antonina walihojiwa. Mikhail aliwekewa vizuizi vya kusafiri
Oktoba 6, 2022
Kesi ya uhalifu ilifunguliwa dhidi ya Anatoliy na Yuriy na ikaunganishwa pamoja na kesi ya Mikhail
Oktoba 7, 2022
Anatoliy na Yuriy waliwekewa vizuizi vya kusafiri
Januari 19, 2023
Kesi ya uhalifu ilianza