Hamia kwenye habari

Je, Yesu ni Mungu Mweza Yote?

Je, Yesu ni Mungu Mweza Yote?

Jibu la Biblia

 Wapinzani wa Yesu walimshtaki kwamba alijifanya kuwa sawa na Mungu. (Yohana 5:18; 10:30-33) Hata hivyo, Yesu hakuwahi kamwe kudai kwamba alikuwa sawa na Mungu Mweza-Yote. Alisema: “Baba ni mkuu kuliko mimi.”—Yohana 14:28.

 Wafuasi wa mapema wa Yesu hawakuamini kwamba alikuwa sawa na Mungu Mweza Yote. Kwa mfano, mtume Paulo aliandika kwamba baada ya Yesu kufufuliwa, Mungu “alimpandisha [Yesu] kwenye cheo cha juu zaidi.” Bila shaka, Paulo hakuamini kwamba Yesu alikuwa Mungu Mweza Yote. Kwa sababu kama angekuwa Mungu Mweza Yote, angepandishwaje kwenye cheo cha juu zaidi?—Wafilipi 2:9.