Hamia kwenye habari

Biblia Ina Maoni Gani Kuhusu Picha Chafu za Ngono? Je, Ni Kosa Kutuma Ujumbe wa Ngono Kwenye Intaneti

Biblia Ina Maoni Gani Kuhusu Picha Chafu za Ngono? Je, Ni Kosa Kutuma Ujumbe wa Ngono Kwenye Intaneti

Jibu la Biblia

 Biblia haitaji moja kwa moja kuhusu picha chafu za ngono, na ngono za kwenye Intaneti, au mambo mengine yanayofanana na hayo. Hata hivyo, Biblia inaeleza waziwazi maoni ya Mungu kuhusu mambo ambayo yanamchochea mtu afanye uzinzi au awe na maoni yasiyofaa kuhusu ngono. Fikiria Maandiko yafuatayo:

  •   “Kwa hiyo, viueni viungo vya mwili wenu vilivyo duniani kwa habari ya uasherati, uchafu, hamu ya ngono.” (Wakolosai 3:5) Kutazama picha chafu za ngono kunachochea tamaa mbaya, badala ya kuziua. Zinamfanya mtu asiwe safi, au awe mchafu, mbele za Mungu.

  •   “Kila mtu ambaye anaendelea kumtazama mwanamke na kumtamani tayari amefanya uzinzi pamoja naye moyoni mwake.” (Mathayo 5:​28) Kuangalia picha za watu wakifanya ngono haramu kunaamsha mawazo mabaya ambayo yanaongoza kwenye matendo mabaya.

  •   “Uasherati na ukosefu wa usafi wa kila namna au pupa visitajwe hata kidogo katikati yenu.” (Waefeso 5:3) Hatupaswi hata kutaja ngono haramu kwa lengo la kujiburudisha, wala hatupaswi hata kidogo kutazama au kusoma habari hizo.

  •   “Matendo ya mwili ni wazi, nayo ni uasherati, uchafu, . . . na mambo kama hayo. Kuhusu mambo hayo mimi ninawaonya ninyi kimbele, kama vile nilivyowaonya kimbele, kwamba wale walio na mazoea ya kufanya mambo ya namna hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.” (Wagalatia 5:​19-​21) Mungu huwaona wale watu wanaotazama picha chafu za ngono, au kutuma picha za ngono kwenye Intaneti, kuzungumza au kutuma ujumbe unaohusu ngono kwenye simu, au kutumia picha za ngono kwa njia ya simu, kuwa wasio safi, au wachafu kimaadili. Ikiwa tungekuwa na mazoea ya kufanya mambo ya aina hiyo, basi tungepoteza kabisa kibali cha Mungu.