Hamia kwenye habari

Je, Biblia Inaruhusu Talaka?

Je, Biblia Inaruhusu Talaka?

Jibu la Biblia

 Biblia inaruhusu talaka. Hata hivyo, Yesu alitaja sababu moja tu ya kuvunja kifungo cha ndoa, aliposema: “Mtu yeyote anayemtaliki mke wake na kumwoa mwingine, ila kwa sababu ya uasherati [kufanya ngono nje ya ndoa], anafanya uzinzi.”—Mathayo 19:9.

 Mungu anachukia mtu anayetumia udanganyifu na hila ili kupata talaka. Mungu mwenyewe atawahukumu wale wanaowaacha waume au wake zao bila sababu nzuri, hasa ikiwa wanafanya hivyo wakiwa na nia ya kufunga ndoa na mtu mwingine.—Malaki 2:13-16; Marko 10:9.