Hamia kwenye habari

Utangulizi wa Vitabu vya Biblia

Video hizi fupi zinatupatia habari zenye thamani kuhusu maelezo ya msingi na mambo yaliyomo kwenye vitabu hivyo. Tumia masomo haya kuboresha funzo lako la kibinafsi na usomaji wako wa Biblia.

Utangulizi wa Mwanzo

Kitabu cha Mwanzo kinatupatia habari muhimu kuhusu chanzo cha wanadamu wote kutia ndani chanzo cha kuteseka na kifo.

Utangulizi wa Kutoka

Mungu alikomboa Waisraeli kutoka utekwani Misri na kuwafanya kuwa taifa lililowekwa wakfu kwake.

Utangulizi wa Yoshua

Ona jinsi Waisraeli wanavyoshinda na kugawanya nchi waliyopewa na Mungu.

Utangulizi wa Waamuzi

Kitabu hiki kilicho na masimulizi yenye kusisimua kinaitwa kwa jina la wanaume wenye ujasiri na wenye imani ambao Mungu aliwatumia kuwakomboa Waisraeli kutoka kwa mataifa yaliyowakandamiza.

Utangulizi wa Ruthu

Kitabu cha Ruthu kinasimulia kuhusu upendo wa kujidhabihu wa mjane mwenye umri mdogo kuelekea mama-mkwe wake na jinsi Yehova alivyowathawabisha wote wawili.

Utangulizi wa 1 Samweli

Ona jinsi historia ya Israeli inavyosonga kutoka kwenye kipindi cha Waamuzi hadi utawala wa wafalme.

Utangulizi wa 1 Wafalme

Ona historia ya Israeli kuanzia kipindi chenye utukufu na ufanisi chini ya utawala wa Mfalme Sulemani hadi kipindi chenye msukosuko cha mataifa mawili ya Israeli na Yuda.

Utangulizi wa 2 Wafalme

Ona jinsi uasi-imani unavyoathiri ufalme wa kaskazini wa Israeli, huku Yehova akiwabariki wachache wanaomtumikia kwa moyo kamili.

Utangulizi wa 1 Mambo ya Nyakati

Fuata nasaba na maisha yenye kusisimua ya Mfalme Daudi anayemwogopa Mungu tangu anapowekwa rasmi kuwa mfalme wa Israeli hadi kifo chake.

Utangulizi wa 2 Mambo ya Nyakati

Ona jinsi historia ya wafalme wa Yuda inakazia thamani ya ushikamanifu kwa Mungu.

Utangulizi wa Ezra

Yehova anatimiza ahadi yake ya kuwakomboa watu wake kutoka Babiloni na kurudisha ibada ya kweli Yerusalemu.

Utangulizi wa Nehemia

Kitabu cha Biblia cha Nehemia kina mambo muhimu ya kuwafundisha watumishi wote wa kweli leo.

Utangulizi wa Esta

Matukio yenye kusisimua ya siku za Esta yataimarisha imani yako katika uwezo wa Yehova Mungu wa kuwakomboa watu wake kutoka katika majaribu leo.

Utangulizi wa Ayubu

Wote wanaompenda Yehova watajaribiwa. Simulizi la Ayubu linatusaidia tuwe na uhakika kwamba tunaweza kudumisha utimilifu na kutetea enzi kuu ya Yehova.

Utangulizi wa Zaburi

Kitabu cha Zaburi kinategemeza enzi kuu ya Yehova, kinawasaidia na kuwafariji wale wanaompenda, na kuonyesha jinsi ulimwengu utakavyobadilika kupitia kwa Ufalme wake.

Utangulizi wa Methali

Jipatie mwongozo kutoka kwa Mungu kuhusu kila jambo maishani—iwe ni kuhusu biashara au mambo ya familia.

Utangulizi wa Mhubiri

Mfalme Sulemani anaeleza ni mambo gani ya maana zaidi maishani na kuyatofautisha na mambo yanayopingana na hekima ya Mungu.

Utangulizi wa Wimbo wa Sulemani

Upendo wa kweli wa msichana Mshulami kumwelekea mvulana mchungaji unafafanuliwa kuwa “mwali wa moto wa Yah.” Kwa nini?

Utangulizi wa Isaya

Isaya ni kitabu cha unabii wa kweli kinachoweza kuimarisha uhakika wetu katika Yehova akiwa Mtimizaji wa ahadi na Mungu wa wokovu wetu.

Utangulizi wa Yeremia

Yeremia alidumu kwa uaminifu katika mgawo wake akiwa nabii licha ya hali ngumu. Fikiria kuhusu mfano wake na jinsi mfano huo unavyoweza kuwanufaisha Wakristo leo.

Utangulizi wa Maombolezo

Kitabu hiki kiliandikwa na nabii Yeremia, na kinaelezea huzuni iliyotokana na uharibifu wa Yerusalemu na kuonyesha jinsi toba inavyotokeza rehema ya Mungu.

Utangulizi wa Ezekieli

Kwa unyenyekevu na ujasiri Ezekieli alitimiza mgawo wowote aliopewa na Mungu, hata migawo migumu sana. Mfano wake ni muhimu sana kwetu leo.

Utangulizi wa Danieli

Danieli na waandamani wake waliendelea kuwa waaminifu kwa Yehova licha ya hali zote. Mfano wao pamoja na utimizo wa unabii unaweza kutusaidia sasa, katika siku za mwisho.

Utangulizi wa Hosea

Unabii wa Hosea una masomo muhimu kwa ajili yetu leo kuhusu rehema ya Yehova kuwaelekea wakosaji wanaotubu na aina ya ibada anayotaka.

Utangulizi wa Yoeli

Yoeli alitabiri kuhusu “siku ya Yehova” iliyokuwa ikikaribia na akaonyesha njia pekee ya kuokoka ni nini. Unabii wake ni muhimu hata zaidi leo.

Utangulizi wa Amosi

Yehova alimtumia mwanamume huyu mnyenyekevu kwa ajili ya kazi muhimu. Tunaweza kujifunza masomo gani muhimu kutokana na mfano wa Amosi?

Utangulizi wa Yona

Nabii alikubali kurekebishwa, akatimiza mgawo wake, na akafundishwa somo muhimu kuhusu upendo mshikamanifu na rehema za Mungu. Mambo aliyojionea yatagusa moyo wako.

Utangulizi wa Mika

Unabii huu ulioongozwa kwa roho unaimarisha uhakika wetu kwamba Yehova hadai mengi mno kutoka kwetu na yote anayotaka ni kwa faida yetu.

Utangulizi wa Nahumu

Unabii unatupa uhakika kwamba sikuzote Yehova hutimiza neno lake na kwamba anawafariji wote wanaotafuta amani na wokovu chini ya Ufalme wake.

Utangulizi wa Habakuki

Tunaweza kuwa na uhakika kwamba sikuzote Yehova anajua wakati unaofaa na njia bora zaidi ya kuwaokoa watu wake.

Utangulizi wa Sefania

Kwa nini tunapaswa kujihadhari tusifikiri kwamba siku ya hukumu ya Yehova haitafika?

Utangulizi wa Hagai

Unabii unakazia umuhimu wa kutanguliza ibada ya Mungu badala ya mapendezi ya kibinafsi.

Utangulizi wa Zekaria

Maono na unabii mwingi ulioongozwa kwa roho uliwaimarisha watu wa Mungu katika nyakati za kale. Unabii huohuo unaendelea kutuhakikishia kwamba Yehova atatutegemeza leo.

Utangulizi wa Mathayo

Furahia kujifunza mambo ya msingi kuhusu kitabu hiki cha Biblia, injili ya kwanza kati ya zile injili nne.

Utangulizi wa Marko

Kitabu cha Marko ndicho kitabu kifupi zaidi kati ya Injili zote. Simulizi hili linatusaidia kuwazia kuhusu utawala wa wakati ujao wa Yesu akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu.

Utangulizi wa Luka

Ni habari gani ambayo inapatikana tu katika Injili ya Luka?

Utangulizi wa Yohana

Simulizi la Yohana linakazia jinsi Yesu alivyowapenda wanadamu, mfano alioweka wa unyenyekevu, na utambulisho wake akiwa Masihi​—Mfalme wa wakati ujao wa Ufalme wa Mungu.

Utangulizi wa Matendo ya Mitume

Wakristo wa mapema walifanya kazi kwa bidii ili kufanya wanafunzi wa watu wa mataifa yote. Kitabu cha Biblia cha Matendo kinaweza kuchochea bidii na uchangamfu wako katika huduma.

Utangulizi wa Waroma

Mwongozo uliotolewa kupitia roho ya Mungu kuhusu jinsi Yehova hana ubaguzi na umuhimu wa kuwa na imani katika Yesu Kristo.

Utangulizi wa 1 Wakorintho

Barua ya Paulo inatia ndani mashauri yaliyoongozwa na roho kuhusu umoja, usafi wa maadili, upendo, na imani katika ufufuo.

Utangulizi wa 2 Wakorintho

Yehova, “Mungu wa faraja yote,” huwaimarisha na kuwategemeza watumishi wake.

Utangulizi wa Wagalatia

Barua ya Paulo kwa Wagalatia inafaa leo kama ilivyofaa ilipoandikwa kwa mara ya kwanza. Inaweza kuwasaidia Wakristo wote wa kweli kudumisha uaminifu.

Utangulizi wa Waefeso

Barua hii iliyoongozwa na roho inakazia kusudi la Mungu la kuleta amani na umoja kupitia Yesu Kristo.

Utangulizi wa Wafilipi

Tunapoendelea kuwa imara chini ya majaribu, tunawatia moyo wengine kusimama imara.

Utangulizi wa Wakolosai

Tunaweza kumpendeza Yehova kwa kutumia mambo tunayojifunza, kwa kusameheana kwa hiari, na kutambua cheo cha Yesu na mamlaka yake.

Utangulizi wa 1 Wathesalonike

Tunahitaji kuendelea kuwa macho kiroho, ‘kuhakikisha mambo yote,’ ‘kusali bila kuacha,’ na kutiana moyo.

Utangulizi wa 2 Wathesalonike

Paulo anarekebisha maoni yenye kasoro kuhusu kuja kwa siku ya Yehova, na anawatia moyo akina ndugu kusimama imara katika imani.

Utangulizi wa 1 Timotheo

Mtume Paulo aliandika 1 Timotheo ili kuweka mwelekezo wa kitengenezo kutanikoni na kuonya dhidi ya mafundisho ya uwongo na dhidi ya kupenda pesa.

Utangulizi wa 2 Timotheo

Paulo anamtia moyo Timotheo atimize kikamili huduma yake.

Utangulizi wa Tito

Barua ya Paulo kwa Tito inazungumzia matatizo katika kutaniko la Krete na kuorodhesha sifa za kiroho ambazo wazee wanapaswa kuwa nazo.

Utangulizi wa Filemoni

Barua hii fupi yenye ujumbe mzito ina masomo muhimu kwa Wakristo, kama vile unyenyekevu, fadhili, na kusamehe.

Utangulizi wa Waebrania

Ibada ya Kikristo inategemea mambo makubwa zaidi kuliko hekalu la kidunia na dhabihu za wanyama.

Utangulizi wa Yakobo

Yakobo anatumia mifano kufundisha kanuni muhimu za Kikristo.

Utangulizi wa 1 Petro

Barua ya kwanza ya Petro inatutia moyo tuwe watendaji na kumtupia Mungu mahangaiko yetu yote.

Utangulizi wa 2 Petro

Barua ya pili ya Petro inatutia moyo tuwe waaminifu tunaposubiri mbingu mpya na dunia mpya.

Utangulizi wa 1 Yohana

Barua ya Yohana inatuonya dhidi ya wapinga-Kristo na kutusaidia kuona kile tunachopaswa kupenda na tusichopaswa kupenda.

Utangulizi wa 2 Yohana

Barua ya pili ya Yohana inatukumbusha tuendelee kutembea katika kweli na kujilinda dhidi ya wadanganyifu.

Utangulizi wa 3 Yohana

Barua ya tatu ya Yohana inatufundisha somo muhimu kuhusu ukarimu wa Kikristo.

Utangulizi wa Yuda

Yuda anafunua wazi njia za kiovu za wale wanaojaribu kuwadanganya na kuwapotosha Wakristo.

Utangulizi wa Ufunuo

Maono yenye kusisimua ya kitabu cha Ufunuo yanaonyesha jinsi Ufalme wa Mungu utakavyotimiza kusudi la Mungu kwa ajili ya wanadamu na dunia.

Utangulizi wa Biblia

Ona jinsi kila kitabu kinavyochangia kichwa kikuu cha Biblia yote—jinsi Ufalme mikononi mwa Kristo Yesu utakavyolitetea jina la Yehova.

Huenda Ukapenda Pia

VITABU NA BROSHUA

Biblia​—Ina Ujumbe Gani?

Kuna ujumbe gani wa msingi wa Biblia?