Kumbukumbu la Torati 30:1-20

  • Kumrudia Yehova (1-10)

  • Amri za Yehova si ngumu sana (11-14)

  • Kuchagua kati ya uzima na kifo (15-20)

30  “Maneno haya yote yatakapotimia kwenu, baraka na laana ambayo nimeweka mbele yenu,+ nanyi myakumbuke*+ katika mataifa yote ambako Yehova Mungu wenu atawatawanya,+  nanyi mrudi kwa Yehova Mungu wenu+ na kuisikiliza sauti yake kulingana na yote ninayowaamuru leo, ninyi na wana wenu, kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote,+  ndipo Yehova Mungu wenu atakapowarudisha mateka wenu+ na kuwaonyesha ninyi rehema+ na kuwakusanya tena kutoka katika mataifa yote ambako Yehova Mungu wenu aliwatawanya.+  Hata watu wenu wakitawanywa mpaka mwisho wa mbingu, Yehova Mungu wenu atawakusanya na kuwarudisha kutoka huko.+  Yehova Mungu wenu atawarudisha katika nchi ambayo baba zenu walimiliki, nanyi mtaimiliki; naye atawafanikisha na kuwafanya mwongezeke kuliko baba zenu.+  Yehova Mungu wenu ataisafisha* mioyo yenu na mioyo ya wazao wenu,+ ili mumpende Yehova Mungu wenu kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote na ili muweze kuishi.+  Ndipo Yehova Mungu wenu atawaletea laana hizi zote maadui wenu, waliowachukia na kuwatesa.+  “Kisha mtarudi na kuisikiliza sauti ya Yehova na kushika amri zake zote ninazowaamuru leo.  Yehova Mungu wenu atawaletea mafanikio mengi katika kazi yote ya mikono yenu,+ atawafanya muwe na watoto wengi na mifugo mingi na mazao mengi ya ardhi yenu, kwa maana Yehova atafurahia tena kuwafanikisha, kama alivyofurahia kuwafanikisha mababu zenu.+ 10  Kwa maana wakati huo mtaisikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu na kushika amri zake na sheria zilizoandikwa katika kitabu hiki cha Sheria, nanyi mtarudi kwa Yehova Mungu wenu kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote.+ 11  “Sasa amri hii ninayowaamuru leo si ngumu sana kwenu, wala haiko mbali msiweze kuifikia.+ 12  Haiko mbinguni, hivi kwamba mseme, ‘Ni nani atakayepanda juu mbinguni ili atuletee, tuisikie na kuishika?’+ 13  Wala haiko ng’ambo ya bahari, hivi kwamba mseme, ‘Ni nani atakayevuka ng’ambo ya bahari atuletee, tuisikie na kuishika?’ 14  Kwa maana neno hilo liko karibu sana nanyi, katika kinywa chenu wenyewe na katika moyo wenu wenyewe,+ ili mlitende.+ 15  “Tazameni, naweka mbele yenu leo uzima na mema, na kifo na mabaya.+ 16  Ikiwa mtazisikiliza amri za Yehova Mungu wenu ninazowaamuru leo, kwa kumpenda Yehova Mungu wenu,+ kutembea katika njia zake, na kushika amri zake na maagizo yake na sheria zake,* basi mtaishi+ na kuongezeka, na Yehova Mungu wenu atawabariki katika nchi mnayoenda kuimiliki.+ 17  “Lakini moyo wenu ukikengeuka+ na kukataa kusikiliza, mshawishiwe na kuiinamia miungu mingine na kuiabudu,+ 18  nawaambia ninyi leo kwamba hakika mtaangamia.+ Hamtaishi kwa muda mrefu katika nchi mnayovuka Yordani ili kuimiliki. 19  Nachukua mbingu na dunia kuwa mashahidi dhidi yenu leo kwamba nimeweka uzima na kifo mbele yenu, baraka na laana;+ nanyi lazima mchague uzima ili mwendelee kuishi,+ ninyi na wazao wenu,+ 20  kwa kumpenda Yehova Mungu wenu,+ kwa kuisikiliza sauti yake, na kushikamana naye,+ kwa maana yeye ni uzima wenu na kwa uwezo wake mtaishi kwa muda mrefu katika nchi ambayo Yehova aliapa kwamba angewapa mababu zenu Abrahamu, Isaka, na Yakobo.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “myatie tena moyoni mwenu.”
Angalia Kamusi.
Tnn., “ataitahiri.”
Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Tnn., “maamuzi yake ya hukumu.”