Ufunuo kwa Yohana 7:1-17

  • Malaika wanne wanaozuia pepo za maangamizi (1-3)

  • Wale 144,000 watiwa muhuri (4-8)

  • Umati mkubwa ukiwa umevaa kanzu nyeupe (9-17)

7  Baada ya hayo nikaona malaika wanne wamesimama juu ya pembe nne za dunia, wakizishika kwa nguvu zile pepo nne za dunia ili upepo wowote usivume juu ya dunia au juu ya bahari au juu ya mti wowote.  Nami nikamwona malaika mwingine akipanda kutoka mashariki,* akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai; naye akawaambia kwa sauti kubwa wale malaika wanne waliopewa ruhusa ya kuidhuru dunia na bahari,  akisema: “Msiidhuru dunia au bahari au miti, hadi tutakapowatia muhuri+ watumwa wa Mungu wetu katika mapaji ya nyuso zao.”+  Nami nikaisikia idadi ya wale waliotiwa muhuri, 144,000,+ waliotiwa muhuri kutoka kila kabila la wana wa Israeli:+  Kutoka kabila la Yuda 12,000 waliotiwa muhuri; kutoka kabila la Rubeni 12,000; kutoka kabila la Gadi 12,000;  kutoka kabila la Asheri 12,000; kutoka kabila la Naftali 12,000; kutoka kabila la Manase+ 12,000;  kutoka kabila la Simeoni 12,000; kutoka kabila la Lawi 12,000; kutoka kabila la Isakari 12,000;  kutoka kabila la Zabuloni 12,000; kutoka kabila la Yosefu 12,000; kutoka kabila la Benjamini 12,000 waliotiwa muhuri.  Baada ya hapo nikaona, na tazama! umati mkubwa, ambao hakuna mtu aliyeweza kuuhesabu, kutoka mataifa yote na makabila na jamii na lugha,+ wakiwa wamesimama mbele ya kiti cha ufalme na mbele ya Mwanakondoo, wakiwa wamevaa kanzu nyeupe;+ na walikuwa na matawi ya mitende mikononi mwao.+ 10  Nao wanaendelea kusema kwa sauti kubwa: “Wokovu unatoka kwa Mungu wetu, anayeketi kwenye kiti cha ufalme,+ na kwa Mwanakondoo.”+ 11  Malaika wote walikuwa wamesimama kukizunguka kile kiti cha ufalme na wale wazee+ na wale viumbe hai wanne, nao wakaanguka kifudifudi mbele ya kile kiti cha ufalme na kumwabudu Mungu, 12  wakisema: “Amina! Sifa na utukufu na hekima na shukrani na heshima na uwezo na nguvu ziwe kwa Mungu wetu milele na milele.+ Amina.” 13  Ndipo mmoja wa wale wazee akaniuliza: “Hawa waliovaa kanzu nyeupe,+ ni nani nao walitoka wapi?” 14  Basi nikamwambia mara moja: “Bwana wangu, wewe ndiye unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wale wanaotoka katika ile dhiki kuu,+ nao wamefua kanzu zao na kuzifanya nyeupe katika damu ya Mwanakondoo.+ 15  Ndiyo sababu wako mbele ya kile kiti cha ufalme cha Mungu, nao wanamtolea utumishi mtakatifu mchana na usiku katika hekalu lake; na Yule anayeketi kwenye kiti cha ufalme+ atatandaza hema lake juu yao.+ 16  Hawatakuwa na njaa wala kiu tena, wala jua halitawachoma wala joto lolote lenye kuunguza,+ 17  kwa sababu Mwanakondoo,+ aliye katikati ya kile kiti cha ufalme, atawachunga+ na kuwaongoza kwenye chemchemi za maji* ya uzima.+ Na Mungu atafuta kila chozi katika macho yao.”+

Maelezo ya Chini

Au “mawio ya jua.”
Au “mabubujiko ya maji.”