Kwa Waefeso 6:1-24

  • Ushauri kwa watoto na wazazi (1-4)

  • Ushauri kwa watumwa na mabwana (5-9)

  • Mavazi kamili ya silaha kutoka kwa Mungu (10-20)

  • Salamu za mwisho (21-24)

6  Enyi watoto, watiini wazazi wenu+ katika muungano na Bwana, kwa maana hilo ni jambo la uadilifu.  “Mheshimu baba yako na mama yako,”+ hiyo ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi:  “Ili mambo yakuendee vema* nawe ukae muda mrefu duniani.”  Nanyi akina baba, msiwe mkiwakasirisha watoto wenu,+ bali endeleeni kuwalea katika nidhamu+ na maagizo ya* Yehova.*+  Enyi watumwa, watiini mabwana wenu wanadamu,*+ kwa kuogopa na kutetemeka kwa unyoofu wa mioyo yenu, kama vile kwa Kristo,  si wakati tu mnapotazamwa, ili tu kuwapendeza wanadamu,*+ bali kama watumwa wa Kristo mkifanya mapenzi ya Mungu kwa nafsi* yote.+  Tumikieni mkiwa na mtazamo mzuri, kama kwa Yehova,*+ na si kwa wanadamu,  kwa maana mnajua kwamba wema wowote ambao kila mtu hufanya, Yehova* atamlipa wema huo,+ iwe ni mtumwa au mtu huru.  Pia, enyi mabwana, endeleeni kuwatendea kwa njia hiyohiyo, bila kuwatisha, kwa maana mnajua kwamba Bwana wao na wenu pia yuko mbinguni,+ naye hana ubaguzi wowote. 10  Mwishowe, endeleeni kujipatia nguvu+ katika Bwana na katika uwezo wa nguvu zake. 11  Vaeni mavazi kamili ya silaha+ kutoka kwa Mungu ili mweze kusimama imara dhidi ya matendo yenye hila ya* Ibilisi; 12  kwa sababu tunapambana,*+ si dhidi ya damu na mwili, bali dhidi ya serikali, dhidi ya mamlaka, dhidi ya watawala wa ulimwengu wa giza hili, dhidi ya majeshi ya roho waovu+ katika mahali pa kimbingu. 13  Kwa sababu hiyo chukueni mavazi kamili ya silaha kutoka kwa Mungu,+ ili mweze kupinga katika ile siku ya uovu, na baada ya kutimiza mambo yote, mweze kusimama imara. 14  Kwa hiyo, simameni imara, mkiwa mmejifunga kiunoni mshipi wa ile kweli,+ mkiwa mmevaa bamba la kifuani la uadilifu,+ 15  na mkiwa mmevaa viatu miguuni tayari kutangaza habari njema ya amani.+ 16  Mbali na mambo hayo, chukueni ngao kubwa ya imani,+ ambayo kwa kuitumia mtaizima mishale yote inayowaka moto* ya yule mwovu.+ 17  Pia, pokeeni kofia ya chuma ya wokovu,+ na upanga wa roho, yaani, neno la Mungu,+ 18  na kwa kila namna ya sala+ na dua mkiendelea kusali kila wakati katika roho.+ Na hivyo kaeni macho, daima mkiomba dua kwa ajili ya watakatifu wote. 19  Pia, msali kwa ajili yangu, kwamba ninapofungua kinywa changu nipewe maneno, ili niweze kuzungumza kwa ujasiri ninapojulisha siri takatifu ya habari njema,+ 20  ambayo kwa ajili yake ninatenda kama balozi+ aliyefungwa minyororo, na kwamba niweze kuzungumza kuihusu kwa ujasiri, kama ninavyopaswa kuzungumza. 21  Basi ili ninyi pia mjue kunihusu na jinsi ninavyoendelea, Tikiko,+ ndugu mpendwa na mhudumu mwaminifu katika Bwana, atawajulisha mambo yote.+ 22  Ninamtuma kwenu kwa kusudi hili, ili mjue jinsi tunavyoendelea na aifariji mioyo yenu. 23  Akina ndugu na wawe na amani na upendo pamoja na imani kutoka kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo. 24  Fadhili zisizostahiliwa na ziwe pamoja na wote wanaompenda Bwana wetu Yesu Kristo katika hali ya kutoharibika.

Maelezo ya Chini

Au “Ili ufanikiwe.”
Au “mwelekezo wa; mwongozo wa.” Tnn., “kuweka katika akili.”
Tnn., “wa kimwili.”
Angalia Kamusi, “Nafsi.”
Tnn., “si kwa njia ya utumishi wa macho ili kuwapendeza wanadamu.”
Au “njama za.”
Tnn., “tunapigana mweleka.”
Au “makombora.”