Barua kwa Wakolosai 2:1-23

  • Siri takatifu ya Mungu, Kristo (1-5)

  • Jihadharini na wadanganyifu (6-15)

  • Uhalisi ni wa Kristo (16-23)

2  Kwa maana ninataka mjue jinsi ninavyopambana sana kwa ajili yenu na kwa ajili ya wale walio huko Laodikia+ na kwa ajili ya wote ambao hawajaniona mimi binafsi.*  Ninafanya hivyo ili mioyo yao ifarijiwe+ na ili waunganishwe kwa upatano katika upendo+ na wawe na utajiri wote unaotokana na uhakikisho kamili wa uelewaji wao, ili wapate ujuzi sahihi wa siri takatifu ya Mungu, yaani, Kristo.+  Hazina zote za hekima na za ujuzi zimefichwa kwa uangalifu ndani yake.+  Ninasema hivyo ili mtu yeyote asiwadanganye kwa hoja zenye kushawishi.  Ingawa sipo katika mwili, nipo pamoja nanyi katika roho, nikishangilia kuona utaratibu wenu mzuri+ na uthabiti wa imani yenu katika Kristo.+  Kwa hiyo, kama vile ambavyo mmempokea Kristo Yesu aliye Bwana, endeleeni kutembea katika muungano naye,  mkiwa mmetia mizizi na kujengwa katika yeye+ na kuimarishwa katika imani,+ kama vile mlivyofundishwa, mkijawa kabisa na shukrani.+  Jihadharini ili mtu yeyote asiwachukue mateka* kupitia falsafa na udanganyifu+ mtupu kulingana na mapokeo ya wanadamu, kulingana na mambo ya msingi ya ulimwengu na si kulingana na Kristo;  kwa sababu ndani yake ujazo wote wa sifa ya Mungu hukaa kimwili.+ 10  Basi mmepata ujazo kupitia kwake, yule aliye kichwa cha serikali na mamlaka yote.+ 11  Kwa uhusiano wenu pamoja naye, ninyi pia mlitahiriwa kwa tohara iliyofanywa bila mikono kwa kuuvua mwili wenye nyama,+ kwa tohara ambayo ni ya Kristo.+ 12  Kwa maana mlizikwa pamoja naye katika ubatizo wake,+ na kwa uhusiano wenu pamoja naye mlifufuliwa+ pia pamoja kupitia imani yenu katika matendo yenye nguvu ya Mungu, aliyemfufua Kristo kutoka kwa wafu.+ 13  Zaidi ya hilo, ingawa mlikuwa wafu katika makosa yenu na katika hali ya kutotahiriwa ya mwili wenu, Mungu aliwafanya muwe hai pamoja naye.+ Alitusamehe kwa fadhili makosa yetu yote+ 14  na kuifuta* hati iliyoandikwa kwa mkono+ ambayo ilikuwa na amri+ na iliyokuwa ikitupinga.+ Ameiondoa njiani kwa kuipigilia misumari kwenye mti wa mateso.*+ 15  Na kupitia mti huo,* amezivua na kuziacha uchi serikali na mamlaka naye amezionyesha hadharani kwamba zimeshindwa,+ akiziongoza katika maandamano ya ushindi. 16  Kwa hiyo, msimruhusu mtu yeyote awahukumu kuhusu mnachokula na kunywa+ au kuhusu kushika sherehe au mwezi mpya+ au sabato.+ 17  Mambo hayo ni kivuli cha mambo yanayokuja,+ bali uhalisi ni wa Kristo.+ 18  Msimruhusu mtu yeyote anayependezwa na unyenyekevu wa uwongo na namna ya ibada ya malaika awanyang’anye tuzo,+ “akichukua msimamo juu ya”* mambo ambayo ameona. Kwa kweli, anajivuna bila sababu inayofaa kwa akili yake ya kimwili, 19  naye hashiki imara kichwa,+ yeye ambaye kupitia kwake mwili wote huandaliwa na kuunganishwa kwa upatano kupitia viungo na kano zake, na kufanywa ukue kwa ukuzi unaotoka kwa Mungu.+ 20  Ikiwa mlikufa pamoja na Kristo kuhusiana na mambo ya msingi ya ulimwengu,+ kwa nini mnaishi kana kwamba bado ninyi ni sehemu ya ulimwengu kwa kuendelea kujitiisha chini ya amri hizi:+ 21  “Usishike, wala usionje, wala usiguse,” 22  kuhusiana na mambo yote ambayo huangamia pamoja na matumizi yake, kulingana na amri na mafundisho ya wanadamu?+ 23  Ingawa mambo hayo huonekana kana kwamba yana hekima katika ibada ya kujitungia wenyewe na unyenyekevu wa uwongo, na kuutendea mwili kwa ukali,+ hayana thamani yoyote katika kuzuia kuutosheleza mwili.

Maelezo ya Chini

Tnn., “hawajauona uso wangu katika mwili.”
Au “asiwachukue kama mawindo yake.”
Au “kuiondoa.”
Angalia Kamusi.
Au labda, “kupitia yeye.”
Yamenukuliwa kutoka kwenye desturi za mafumbo (jando) ya kipagani.