Yoeli 2:1-32

  • Siku ya Yehova na jeshi lake kubwa (1-11)

  • Wasihiwa wamrudie Yehova (12-17)

    • “Irarueni mioyo yenu” (13)

  • Yehova awajibu watu wake (18-32)

    • “Nitaimimina roho yangu” (28)

    • Maajabu mbinguni na duniani (30)

    • Wale wanaoliitia jina la Yehova wataokolewa (32)

2  “Pigeni pembe Sayuni!+ Pigeni kelele za vita katika mlima wangu mtakatifu. Wakaaji wote wa nchi* na watetemeke,Kwa maana siku ya Yehova inakuja!+ Iko karibu!   Ni siku ya giza na utusitusi,+Siku ya mawingu na utusitusi mzito,+Giza hilo litaenea kama nuru ya mapambazuko juu ya milima. Kuna taifa lenye watu wengi na lenye nguvu;+Halijawahi kamwe kuwepo taifa kama hilo,Na halitakuwepo tena kamwe taifa lingine kama hiloKatika miaka yote ya vizazi vyote.   Moto unateketeza kila kitu kilicho mbele yake,Na vitu vilivyo nyuma yake vinateketezwa na mwali wa moto.+ Kabla halijapita nchi huwa kama bustani ya Edeni,+Lakini baada ya kupita nchi inabaki nyika iliyo ukiwa,Na hakuna chochote kinachoweza kuponyoka.   Linafanana na farasi,Nao hukimbia kama farasi wa vita.+   Wanaporuka juu ya vilele vya milima, sauti yao ni kama ya magari ya vita,+Kama sauti ya moto mkali unaoteketeza majani makavu. Wao ni kama taifa lenye nguvu lililojipanga kivita.+   Kwa sababu yao, mataifa yatakuwa na maumivu makali. Kila uso utageuka na kuwa mwekundu kwa sababu yao.   Wanashambulia kama mashujaa,Wanapanda ukuta kama wanajeshi,Kila mmoja wao anaendelea kufuata mwendo wake mwenyewe,Nao hawatoki katika njia zao.   Hawasukumani;Kila mtu hupiga mwendo kwenye njia yake. Baadhi yao wakiuawa kwa silaha,Wengine hawavunji safu zao.   Wanaingia haraka jijini, nao hukimbia ukutani. Hupanda juu ya nyumba, na kuingia kama mwizi madirishani. 10  Nchi inatetemeka mbele yao na mbingu kutikisika. Jua na mwezi vimekuwa na giza,+Na nyota zimepoteza mwangaza wake. 11  Yehova atapaza sauti mbele ya jeshi lake,+ kwa maana jeshi lake ni kubwa sana.+ Kwa maana anayetekeleza neno Lake ni mwenye nguvu;Kwa maana siku ya Yehova ni kuu na inaogopesha sana.+ Ni nani anayeweza kuistahimili?”+ 12  “Hata sasa,” asema Yehova, “rudini kwangu kwa mioyo yenu yote,+Kwa kufunga+ na kulia na kuomboleza. 13  Irarueni mioyo yenu,+ wala si mavazi yenu,+Nanyi mrudi kwa Yehova Mungu wenu,Kwa maana ni mwenye huruma* na rehema, si mwepesi wa hasira,+ naye ana upendo mwingi mshikamanifu,+Naye atafikiria upya* msiba aliokusudia kuleta. 14  Ni nani ajuaye ikiwa hatabadili nia na kuufikiria upya*+Na kuwaachia baraka,Ili mweze kumtolea Yehova Mungu wenu toleo la nafaka na toleo la kinywaji? 15  Pigeni pembe Sayuni! Tangazeni watu wafunge;* waiteni watu kwenye kusanyiko takatifu.+ 16  Wakusanyeni watu; litakaseni kutaniko.+ Wakusanyeni wanaume wazee;* wakusanyeni watoto wadogo na pia watoto wanaonyonya.+ Bwana harusi na atoke katika chumba chake cha ndani, na bibi harusi atoke katika chumba chake cha bibi harusi. 17  Kati ya ukumbi na madhabahu+Acheni makuhani, wahudumu wa Yehova, walie na kusema: ‘Ee Yehova, wahurumie watu wako;Usifanye urithi wako uwe kitu cha kudharauliwa,Kwa kuacha mataifa yawatawale. Kwa nini mataifa yaseme: “Yuko wapi Mungu wao?”’+ 18  Kwa hiyo Yehova atakuwa na bidii kwa ajili ya nchi yakeNa kuwahurumia watu wake.+ 19  Yehova atawajibu hivi watu wake: ‘Tazama, ninawaletea nafaka na divai mpya na mafuta,Nanyi mtatosheka kabisa;+Sitafanya tena mshutumiwe miongoni mwa mataifa.+ 20  Nitamfukuza mbali nanyi mkaaji wa kaskazini;Nitamtawanya katika nchi kavu iliyo ukiwa,Walinzi wake wa mbele kuelekea bahari ya mashariki*Na walinzi wake wa nyuma kuelekea bahari ya magharibi.* Na harufu yake mbaya itapanda juu,Na uvundo wake utaendelea kupanda juu;+Kwa maana Atafanya mambo makuu.’ 21  Usiogope, Ee nchi. Uwe na shangwe na furaha, kwa maana Yehova atafanya mambo makuu. 22  Msiogope, enyi wanyama wa mwituni,Kwa maana malisho ya nyikani yatakuwa kijani kibichi,+Na miti itazaa matunda;+Mitini na mizabibu itazaa kwa wingi.*+ 23  Enyi wana wa Sayuni, iweni na shangwe na kumshangilia Yehova Mungu wenu;+Kwa maana atawapa kiasi kinachofaa cha mvua ya vuli,Naye atawaletea mvua kubwa,Mvua ya vuli na mvua ya masika, kama ilivyokuwa awali.+ 24  Viwanja vya kupuria vitajaa nafaka safi,Na mashinikizo yatafurika divai mpya na mafuta.+ 25  Nami nitafidia miaka ambayoMazao yenu yaliliwa na nzige wanaoruka katika makundi, tunutu, parare wanaokula sana, na nzige* wanaokula sana,Jeshi langu kubwa ambalo nililituma miongoni mwenu.+ 26  Kwa hakika mtakula na kutosheka,+Nanyi mtalisifu jina la Yehova Mungu wenu,+Ambaye ametenda mambo yenye kustaajabisha kwa niaba yenu;Watu wangu hawataaibishwa tena kamwe.+ 27  Nanyi mtalazimika kujua kwamba nimo miongoni mwa Waisraeli+Na kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu+—hakuna mwingine! Watu wangu hawataaibishwa tena kamwe. 28  Kisha nitaimimina roho yangu+ juu ya kila aina ya mwili,Na wana wenu na mabinti wenu watatoa unabii,Na wanaume wenu wazee wataota ndoto,Na wanaume wenu vijana wataona maono.+ 29  Na hata juu ya watumwa wangu wa kiume na watumwa wa kikeNitaimimina roho yangu siku hizo. 30  Nami nitafanya mambo ya ajabu* mbinguni na duniani,Damu na moto na nguzo za moshi.+ 31  Jua litatiwa giza na mwezi utatiwa damu+Kabla ya kuja kwa ile siku ya Yehova iliyo kuu na yenye kuogopesha.+ 32  Na kila mtu anayeliitia jina la Yehova ataokolewa;+Kwa maana kwenye Mlima Sayuni na katika Yerusalemu kutakuwa na wale wanaosalimika,+ kama Yehova alivyosema,Waokokaji wanaoitwa na Yehova.”

Maelezo ya Chini

Au “dunia.”
Au “neema.”
Au “ataghairi kuhusu.”
Au “kughairi.”
Tnn., “Takaseni mfungo.”
Au “wazee.”
Yaani, Bahari ya Chumvi.
Yaani, Bahari ya Mediterania.
Tnn., “kikamili.”
Au “panzi.”
Au “miujiza.”