Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

KUKABILIANA NA HUZUNI YA KUFIWA

Kitabu Kinachotoa Ushauri Bora na Faraja

Kitabu Kinachotoa Ushauri Bora na Faraja

KATIKA MIAKA YA HIVI KARIBUNI, UTAFITI MWINGI UMEFANYWA KUHUSU JINSI YA KUKABILIANA NA UCHUNGU WA KUFIWA NA MTU WA KARIBU. Hata hivyo, kama ilivyotajwa awali, ushauri bora unaotolewa na wataalamu mara nyingi unapatana na hekima iliyo katika Biblia, kitabu kilichoandikwa zamani. Hilo linaonyesha wazi kwamba mwongozo wa Biblia haupitwi na wakati. Lakini zaidi ya kutoa ushauri wenye kutegemeka, Biblia hutoa habari ambazo hatuwezi kupata mahali pengine popote zinazoweza kumfariji sana mtu aliyefiwa.

  • Inatuhakikishia kwamba wapendwa wetu hawateseki

    Biblia inasema hivi katika Mhubiri 9:5: “Waliokufa hawajui jambo lolote.” ‘Mawazo yao hupotea.’ (Zaburi 146:4) Pia, Biblia inafananisha kifo na usingizi mtulivu.—Yohana 11:11.

  • Tunapata faraja kujua kwamba kuna Mungu anayetupenda

    Katika Zaburi 34:15, Biblia inasema kwamba, “macho ya Yehova * yanawatazama waadilifu, na masikio yake yanasikiliza kilio chao cha kuomba msaada.” Hatumwelezi Mungu hisia zetu ili tu tuhisi vizuri au tupange mawazo yetu. Badala yake, sala hutuwezesha kusitawisha uhusiano wa kibinafsi na Muumba wetu, ambaye hutumia nguvu zake kutufariji.

  • Inatupatia tumaini zuri la wakati ujao

    Wazia wakati ambapo wale walio katika makaburi watafufuliwa na kuishi tena duniani! Tumaini hilo linatajwa mara nyingi katika Biblia. Vilevile, Biblia inaeleza jinsi hali itakavyokuwa duniani wakati huo. Inasema kwamba Mungu “atafuta kila chozi kutoka katika macho [yetu], na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.”—Ufunuo 21:3, 4.

Wengi ambao wanamwamini Yehova, Mungu aliyeitunga Biblia, wanapata nguvu za kukabiliana na huzuni wanapofiwa, kwa sababu wanaamini kabisa watawaona tena wapendwa wao. Kwa mfano, Ann, ambaye alifiwa na mume wake aliyekuwa ameishi naye kwa miaka 65, anasema: “Biblia hunihakikishia kwamba wapendwa wetu waliokufa hawateseki na kwamba Mungu atawafufua wote walio katika kumbukumbu yake. Mimi hutafakari jambo hilo kila mara ninapomfikiria mume wangu aliyekufa, na kwa njia hiyo, ninafaulu kustahimili pigo hilo kubwa zaidi maishani mwangu!”

Tiina, aliyetajwa awali, anasema: “Tangu Timo alipokufa, nimeona Mungu akinitegemeza. Kwa kweli, nimehisi kabisa Yehova akinisaidia katika kipindi hiki kigumu. Na tumaini la ufufuo linalotajwa katika Biblia ni halisi sana kwangu. Linaniimarisha na kunipa nguvu za kuvumilia hadi nitakapomwona tena Timo.”

Maelezo hayo yanapatana na ya mamilioni ya watu wanaoiamini Biblia. Ikiwa unahisi kwamba ahadi za Biblia si za kweli au ni ndoto tu, tafadhali, angalau chunguza ili ujithibitishie mwenyewe ikiwa ushauri na ahadi zake ni zenye kutegemeka. Bila shaka, utatambua kwamba Biblia ndicho kitabu kinachotoa ushauri bora na faraja kwa wale waliofiwa.

JIFUNZE MENGI ZAIDI KUHUSU TUMAINI LA WAFU

Tazama video zinazohusiana na habari hiyo kwenye tovuti yetu, jw.org/sw

Biblia inaahidi kwamba, tutawakaribisha tena wapendwa wetu waliokufa watakapofufuliwa wakati ujao

WAFU WAKO KATIKA HALI GANI?

Ni nini hutupata tunapokufa? Jibu la Biblia linafariji na kutia moyo sana

Tafuta kwenye MACHAPISHO > VIDEO (Kisha, Biblia)

JE, UNGEPENDA HABARI NJEMA?

Kukiwa na habari nyingi mbaya, unaweza kupata wapi habari njema? Video hii inatoa utangulizi wa broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!

Tafuta kwenye MACHAPISHO > VIDEO (Kisha, Mikutano na Huduma Yetu)

^ fu. 7 Yehova ni jina la Mungu kama linavyoonyeshwa katika Biblia.