Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Vijana Huuliza

Nitazamie Nini Katika Ndoa?—Sehemu ya 2

Nitazamie Nini Katika Ndoa?—Sehemu ya 2

KATIKA TOLEO LILILOTANGULIA, tulichunguza faida na magumu ambayo unaweza kutazamia katika ndoa.

KATIKA TOLEO HILI, tutazungumzia kwa nini utarajie mambo yasiyotazamiwa.

Tia alama ya ✔ kando ya sanduku linalofaa, kisha andika nambari kando ya masanduku uliyotia alama ukianza na jambo unaloona kuwa muhimu zaidi.

Ninatazamia mwenzi wangu wa wakati ujao awe . . .

  • mwenye sura nzuri

  • ananifanya nijihisi vizuri

  • na miradi kama yangu

  • anapendezwa na aina ya burudani ninayoipenda

Ikiwa unatafuta mwenzi wa ndoa, hakuna ubaya kutarajia mambo yaliyoorodheshwa kwenye ukurasa uliotangulia. Huenda hata ukapata mwenzi anayetimiza mambo hayo yote. Hata hivyo, ukweli wa mambo ni kwamba watu hubadilika kadiri wakati unavyopita​—nazo hali hubadilika pia.

Jambo kuu: Ili ufaulu katika ndoa, lazima utarajie mambo yasiyotazamiwa.

Mambo yanayopendeza. Unaweza kushangaa kwamba mambo fulani ambayo hukutazamia katika ndoa yanaweza kukupendeza.

“Kwa kuwa sasa tumeoana, Maria * anaonekana kuwa mcheshi kuliko nilivyofikiria nilipokuwa nikimchumbia. Kwa kuwa sasa tuna maoni yenye usawaziko kuelekea hali yetu, hatuoni matatizo yanayotokea kuwa magumu sana.”​—Mark.

Mambo yasiyopendeza. Huenda mambo fulani usiyotazamia katika ndoa yasikupendeze. Fikiria mfano ufuatao.

Itakuwaje ikiwa baada ya kufunga ndoa, mwenzi wako anapatwa na tatizo la afya ambalo linafanya msifikie mradi wenu? Kwa kweli, hilo linawezekana, kwa kuwa Biblia inasema kwamba “mambo mabaya huwapata watu wote!” (Mhubiri 9:11, Holy Bible​—Easy-to-Read Version) Bila shaka, utahuzunika kwa sababu ya ugonjwa wa mwenzi wako—​na utavunjika moyo hukufikia mradi wako. Hata hivyo, hali kama hiyo isiyotazamiwa inapotokea utalazimika kukubali ukweli wa mambo na kubadilika kulingana na hali. Ulifunga ndoa na mtu, si mradi.

Jambo kuu: Kama Biblia inavyosema, wale wanaofunga ndoa watakuwa na “dhiki” ya kadiri fulani. (1 Wakorintho 7:28) Nyakati nyingine, dhiki hiyo hutokezwa na hali zisizotazamiwa.

Unawezaje kujitayarisha kwa ajili ya mambo usiyotazamia? Ukifunga ndoa, utahitaji mambo mawili.

1. KUONA MAMBO KIHALISI

Hata muwe mnapatana kadiri gani na mchumba wako, unapaswa kutazamia kwamba

  • hamtakubaliana kuhusu kila jambo.

  • hamtatanguliza mambo yaleyale sikuzote.

  • hamtafurahia mambo yaleyale sikuzote.

  • hamtahisi kwamba mnapendana kwa kiwango kilekile sikuzote kama mlivyohisi mlipoanza uhusiano wenu.

Hali kama hizo zilizoorodheshwa hapo juu ni za kawaida. Lakini hazitaharibu ndoa yako isipokuwa uziruhusu! Kumbuka, Biblia inasema kwamba upendo “huvumilia mambo yote” na “haushindwi kamwe.”​—1 Wakorintho 13:4, 7, 8.

Ukweli wa mambo: Si matatizo unayokabili yatakayoamua ikiwa ndoa yako itafanikiwa au ikiwa itavunjika, bali ni jinsi unavyoyashughulikia.​Wakolosai 3:13.

2. KUWAJIBIKA

Wewe na mwenzi wako mkiazimia kuendelea kuishi pamoja, hata chini ya hali yoyote ile, mtakuwa na uwezo wa kukabiliana na matatizo yasiyotazamiwa.​—Mathayo 19:6.

Watu fulani wanadai kwamba kuwajibika hufanya ndoa iwe mzigo. Kinyume na hilo, kuwajibika hufanya uhusiano wenu uwe imara. Hali zisizotazamiwa zinapotokea, wewe na mwenzi wako mtatafuta njia za kuzitatua badala ya kutafuta njia ya kuachana.

Ili uwe na mtazamo wa kuwajibika, utahitaji kufikiria ndoa kwa usawaziko badala ya kuwa na matazamio yasiyo halisi. Ili kuonyesha tofauti, jaribu zoezi lifuatalo.

1. Wazia kwamba umepewa tiketi ya ndege bila malipo ili usafiri kwenda sehemu yoyote duniani. Ungechagua kwenda wapi, na kwa nini?

Ningeenda:

Sababu:

  • mandhari

  • utamaduni

  • hali ya hewa

  • burudani

  • sababu nyingine

2. Wazia kwamba tiketi hiyo ya ndege ni ya kukufikisha tu mahali pamoja bila kukurudisha na hivyo mahali unapoelekea ndipo patakuwa makao yako ya kudumu.

Sasa ungechagua kwenda wapi?

  • Ningeenda:

  • au

    nisingeenda mahali popote.

Katika zoezi lililo hapo juu, huenda jibu lako la kwanza linatofautiana na la pili. Hata ikiwa umechagua sehemu ileile, kuna uwezekano mkubwa kwamba ulifikiria kwa njia tofauti kuhusu eneo utakaloenda katika swali la pili. Badala ya kujiona kama mtalii tu anayejivinjari ufuoni au anayepanda milima, ulilazimika kujiwazia ukiwa mkazi anayekabiliwa na hali nzuri na magumu ya maisha ya kila siku.

Hivyo ndivyo unavyopaswa kufikiria kuhusu ndoa. Kadiri wakati unavyopita, hali hubadilika. Bila shaka, wewe na mwenzi wako mtabadilika pia. Sehemu kubwa ya mafanikio yenu yatategemea uwezo wenu wa kutarajia mambo yasiyotazamiwa na kushughulika nayo yanapotokea.

Jambo la kufikiria: Unashughulikaje na hali zisizotazamiwa sasa hivi ukiwa mseja?

 

^ fu. 15 Baadhi ya majina katika makala hii yamebadilishwa.

MBONA USIWAULIZE WAZAZI WAKO?

Ni baraka na magumu gani mliyokabili baada tu ya kuoana? Ninaweza kujitayarisha jinsi gani kwa ajili ya mambo yasiyotazamiwa wakati ambapo mimi nitafunga ndoa?