Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova Wanaamini Kwamba Dunia Iliumbwa kwa Siku Sita Zenye Urefu wa Saa 24?

Je, Mashahidi wa Yehova Wanaamini Kwamba Dunia Iliumbwa kwa Siku Sita Zenye Urefu wa Saa 24?

 Hapana. Mashahidi wa Yehova huamini kwamba Mungu ndiye aliyeumba kila kitu. Lakini hatuamini kwamba dunia iliumbwa kwa siku sita zenye urefu wa saa 24. Kwa sababu gani? Kwa sababu wazo hilo linapingana na Biblia. Fikiria mifano miwili ifuatayo:

  1.   Urefu wa siku sita za uumbaji. Watu fulani wanaamini kwamba siku sita za uumbaji zilikuwa na urefu wa saa 24. Lakini katika Biblia, neno “siku” linaweza kurejelea muda mrefu.​—Mwanzo 2:4; Zaburi 90:4.

  2.   Muda ambao dunia imekuwapo. Watu fulani wanafundisha kwamba dunia imekuwapo kwa maelfu michache tu ya miaka. Hata hivyo, kulingana na Biblia, dunia na anga zilikuwepo hata kabla ya zile siku sita za uumbaji kuanza. (Mwanzo 1:1) Kwa sababu hiyo, Mashahidi wa Yehova hawapingi utafiti unaotegemeka wa kisayansi unaoonyesha kwamba dunia imekuwapo kwa mabilioni ya miaka.

 Ingawa Mashahidi wa Yehova wanaamini katika uumbaji, sisi hatupingi sayansi. Tunaamini kwamba sayansi inapatana na Biblia.