Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova Wanafikiri Ni Wao Peke Yao Watakaookolewa?

Je, Mashahidi wa Yehova Wanafikiri Ni Wao Peke Yao Watakaookolewa?

 Hapana. Mamilioni ya watu walioishi katika karne zilizopita na ambao hawakuwa Mashahidi wa Yehova watapata nafasi ya kuokolewa. Biblia inaeleza kwamba katika ulimwengu mpya wa Mungu ulioahidiwa, “kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.” (Matendo 24:15) Isitoshe, watu wengi wanaoishi leo wanaweza kuanza kumtumikia Mungu, nao pia watapata wokovu. Vyovyote vile, si kazi yetu kuamua ni nani atakayeokolewa au ambaye hataokolewa. Kazi hiyo iko mikononi mwa Yesu.—Yohana 5:22, 27.