Hamia kwenye habari

Maonyesho ya Biblia Yanayotukuza Jina la Yehova

Maonyesho ya Biblia Yanayotukuza Jina la Yehova

Tangu tulipofungua maonyesho ya Biblia kwenye makao yetu makuu ya ulimwenguni pote mwaka wa 2013, tumepokea Biblia nyingi za pekee na zisizopatikana kwa urahisi, zitakazoboresha maonyesho hayo. Biblia hizo zinatia ndani Biblia ya Complutensian Polyglot na matoleo ya kwanza ya Biblia ya King James na “Agano Jipya” la Kigiriki la Erasmus.