Hamia kwenye habari

Kuhubiri Katika Lugha za Asili za Ireland na Uingereza

Kuhubiri Katika Lugha za Asili za Ireland na Uingereza

Mbali na kuwatafuta watu wanaozungumza Kiingereza, Mashahidi wa Yehova wanajitahidi kuwahubiria watu wanaozungumza lugha za asili za Ireland, Scotland, Wales, na Uingereza.

Mnamo Septemba 2012, tulifungua tovuti ya jw.org inayopatikana katika lugha nyingi kutia ndani lugha ya Ireland (Irish) na ya Wales (Welsh). Kisha lugha ya asili ya Scotland (Gaelic) ikaingizwa mnamo Agosti 2014. Pia, tuna machapisho mengi yanayotegemea Biblia katika lugha hizo. Kumekuwa na matokeo gani?

Kiongozi wa kanisa fulani alipokea trakti inayotegemea Biblia katika lugha ya asili ya Scotland, na kuisoma kwa sauti papohapo, kisha akaanza kutokwa machozi. Ni nini kilichomvutia? Alishangazwa na jinsi trakti hiyo ilivyotasiriwa vizuri sana kisha akauliza: “Ni nani aliyeitafsiri? Ni rahisi sana kuilewa!”

Katika mwezi.ambao lugha ya asili ya Scotland iliongezwa kwenye tovuti ya jw.org, watu 750 waliitembelea

Mwalimu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Ireland, jijini Galway, alimwambia Shahidi fulani kwamba yeye hapendezwi na dini. Hata hivyo, alipojua kwamba anaweza kupata broshua yenye kichwa Biblia​—Ina Ujumbe Gani? katika lugha ya asili ya Ireland, aliomba nakala moja. Alisema kwamba watu wote wanapaswa kupata machapisho ya Biblia katika lugha zao za asili, na akawapongeza Mashahidi wa Yehova kwa kutoa machapisho katika lugha ya asili ya Ireland.

Mwanamke mwenye umri mkubwa alipopokea broshua katika lugha ya asili ya Wales, alisema hivi: “Kwa kweli, ikiwa ingekuwa ya Kiingereza, nisingeikubali, lakini nimefurahi sana kuipata katika lugha yangu.”

Agosti 2014, idadi ya machapisho yetu katika lugha ya asili ya Wales iliongezeka katika jw.org. Kwa sababu hiyo, idadi ya watu wanaotembelea tovuti yetu kusoma machapisho katika lugha hiyo ikaongezeka mara mbili zaidi mwezi huo.

“Tunazungumza Lugha Moja”

Baada ya Yesu kuwafafanulia Maandiko wanafunzi wake, walisema hivi kwa msisimko: “Je, mioyo yetu haikuwa ikiwaka alipokuwa akisema nasi barabarani, alipokuwa akitufungulia Maandiko?” (Luka 24:32) Mara nyingi watu wanapofundishwa kweli za Biblia katika lugha yao wenyewe maisha yao hubadilika.

Mwanamume anayeitwa Emyr nchini Wales, ambaye mke wake ni Shahidi wa Yehova, hakuwahi kujiunga na mke wake katika ibada. Kisha akawa rafiki ya Shahidi anayeitwa Russell. Emyr anaeleza jambo lililobadili mtazamo wake: “Nilianza kujifunza Biblia Russell aliponitembelea akiwa na kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? * Alinipa na kusema, ‘Kitabu hiki ni cha lugha ya Welsh. Tutaanza kujifunza kuanzia sasa.’” Kwa nini Emyr alivutiwa na njia ya moja kwa moja ambayo Russell alitumia? Anaeleza hivi: “Tunazungumza lugha moja, tuna utamaduni mmoja, na tunaelewana.” Moyo wa Emyr ulikuwa “ukiwaka” alipokuwa akijifunza Biblia katika lugha yake kwa sababu alielewa kwa urahisi.

Mashahidi wa Yehova wataendelea kuwasaidia watu kujifunza kumhusu Mungu katika lugha zao za asili, lugha inayogusa moyo.

^ fu. 11 Kitabu cha kujifunzia Biblia kinachochapishwa na Mashahidi wa Yehova.