Ona video zinazopatikana

Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Ninapovunjika Moyo?

Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Ninapovunjika Moyo?

Jibu la Biblia

 Ndiyo, kwa sababu musaada muzuri zaidi unatoka kwa “Mungu mwenye kufariji wenye huzuni.”​—2 Wakorintho 7:6, La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo.

Mungu anawasaidia namna gani wenye kuvunjika moyo?

  •   Anawatolea Nguvu. Mungu ‘anawafariji’ ao kuwatuliza. Hilo halimaanishe kwamba anaondoa matatizo yao yote, lakini anajibu sala ya wale wanaomuomba kwa kuwapatia nguvu ya kuvumilia. (Wafilipi 4:13) Unaweza kuwa hakika kwamba iko tayari kukusikiliza, kwa sababu Biblia inasema hivi: ‘Yehova yuko karibu na wale waliovunjika moyo; naye anawaokoa wale waliopondwa roho.’ (Zaburi 34:18) Kwa hiyo, Mungu anasikia unapomuomba musaada hata ikiwa unakosa maneno ya kutumia ili kueleza namna unavyojisikia.​—Waroma 8:26, 27.

  •   Anawatolea mifano mizuri. Muandikaji mumoja wa Biblia alisali hivi: “Toka shimoni, nakulilia, ee Bwana.” Alipokuwa mwenye kuvunjika moyo, mutunga-zaburi alifarijiwa alipokumbuka kwamba Mungu iko tayari kutusamehe makosa yetu. Kwa hiyo, alimuambia Mungu hivi: “Ukikumbuka zambi, nani atasimama? Lakini kwako kuna maondoleo (musamaha) ili wakutumikie kwa heshima.”​—Zaburi 130:1, 3, 4, Verbum Bible.

  •   Anawatolea Tumaini. Zaidi ya kuwafariji watu sasa, Mungu anaahidi kwamba ataondoa matatizo yote yanayowafanya watu wavunjike moyo. Atakapotimiza ahadi hiyo, “mambo ya zamani [kutia ndani huzuni na kuvunjika moyo] hayatakumbukwa akilini, wala hayataingia moyoni.”​—Isaya 65:17.

 Usisahau jambo hili: Hata ikiwa wanaamini kwamba Mungu anaweza kuwasaidia, Mashahidi wa Yehova wanatafuta matunzo ya kiganga ikiwa wanagonjwa. (Marko 2:17) Hata hivyo, sisi Mashahidi wa Yehova hatutie watu moyo kufuata matunzo fulani, tunajua kwamba kila mutu anapaswa kufanya uamuzi wake kuhusu jambo hilo.