Ona video zinazopatikana

Sababu Gani Wayahudi Wengi Waliuawa? Sababu Gani Mungu Hakuzuia Jambo Hilo?

Sababu Gani Wayahudi Wengi Waliuawa? Sababu Gani Mungu Hakuzuia Jambo Hilo?

 Wengi wanaouliza maulizo hayo walipoteza watu waliokuwa wanapenda na hilo liliwaumiza sana. Watu hao hawahitaji majibu pekee lakini pia wanahitaji faraja. Wengine wanafikiri kwamba mauaji hayo yanayoonyesha kabisa kwamba wanadamu ni wabaya sana, kwa hiyo wanaona kuwa vigumu kuamini kwamba kuna Mungu.

Mawazo ya uongo kuhusu Mungu na kuuawa kwa Wayahudi

 Wazo la kutunga: Ni kosa kuuliza kwa nini Mungu aliruhusu Wayahudi wengi waangamizwe.

 Ukweli ni kwamba: Watu wenye imani kubwa wamejiuliza kwa nini Mungu anaruhusu mambo mabaya. Kwa mufano, nabii Habakuki alimuuliza Mungu hivi: ‘Kwa nini unanifanya nione ukosefu huu mubaya wa haki? Kwa nini unaruhusu jeuri, uasi-sheria, uhalifu na ukatili uenee kotekote?’ (Habakuki 1:3, Contemporary English Version) Mungu hakumukaripia Habakuki, lakini aliandikisha maulizo hayo katika Biblia ili sisi wote tuyasome.

 Wazo la kutunga: Mungu hahangaikie mateso ya wanadamu.

 Ukweli ni kwamba: Mungu anachukia uovu na mateso yanayotokana na uovu huo. (Methali 6:16-19) Katika siku za Noa, Mungu ‘aliumia moyoni’ kwa sababu ya jeuri iliyoenea katika dunia yote. (Mwanzo 6:5, 6) Bila shaka, Mungu pia alisikia uchungu sana Wayahudi wengi walipoangamizwa.—Malaki 3:6.

 Wazo la kutunga: Mauaji hayo yalikuwa malipizi ambayo Mungu aliwapatia Wayahudi.

 Ukweli ni kwamba: Mungu aliruhusu Waroma waharibu Yerusalemu wakati wa mitume. (Mathayo 23:37–24:2) Lakini, tangu wakati huo, Mungu hapendelee ao kupatia malipizi taifa fulani. Kwa maoni ya Mungu, “hakuna tofauti kati ya Wayahudi na wasio Wayahudi.”—Waroma 10:12, Biblia Habari Njema.

 Wazo la kutunga: Ikiwa kuna Mungu mwenye upendo na mwenye uwezo, angezuia Wayahudi wengi wasiuawe.

 Ukweli ni kwamba: Hata ikiwa Mungu hatokeze hata kidogo mateso, wakati fulani anayaruhusu yatokee kwa muda.—Yakobo 1:13; 5:11.

Kwa nini Mungu aliruhusu Wayahudi wengi wauawe?

 Sababu iliyomufanya Mungu aruhusu Wayahudi wengi wauawe, ni ileile ambayo imemufanya Mungu aruhusu wanadamu wote wateseke: Kujibu maulizo ya maana sana yaliyotokezwa miaka mingi iliyopita. Biblia inaonyesha waziwazi kwamba anayeitawala ulimwengu sasa, si Mungu lakini ni Shetani. (Luka 4:1, 2, 6; Yohana 12:31) Kwa kuwa habari hii inatokeza ulizo kwa nini Mungu anaruhusu mabaya, tuchunguze mambo mawili ya kweli katika Biblia yanaonyesha kwa nini Mungu aliruhusu Wayahudi wauawe.

  1.   Ni uhuru wa kuchagua wa nani uliofanya Wayahudi wengi wauawe? Mungu aliwaambia wanadamu wa kwanza, Adamu na Eva, yale aliyopenda wafanye, lakini hakuwakaza wamutii. Walichagua kujiamulia wenyewe yaliyokuwa mema na mabaya. Basi uamuzi wao mubaya—kama uamuzi mubaya ambao wanadamu wamechukua katika historia yao yote—umewaletea wanadamu matokea mabaya sana. (Mwanzo 2:17; 3:6; Waroma 5:12) Ni kama vile kitabu kimoja cha Kiingereza kinavyosema: “Mateso mengi ya ulimwengu yanatokana moja kwa moja na kutumia vibaya uhuru wetu wa kuchagua ambao tumepewa.” (Statement of Principles of Conservative Judaism) Kuliko kuwanyanganya uhuru wao wa kuchagua, Mungu ameachia wanadamu wakati ili wajaribu kushugulikia mambo yao bila yeye kujiingiza katika mambo hayo.

  2.   Mungu anaweza na ataondoa magumu yote yaliyoletwa na kuuawa kwa Wayahudi. Mungu anaahidi kufufua mamilioni ya wafu, kutia ndani wale Wayahudi wengi waliowauawa. Atamaliza pia uchungu ambao wale waliookoka mauaji ya Wayahudi wanasikia wanapokumbuka namna walivyookoka mauaji hayo. (Isaya 65:17; Matendo 24:15) Upendo wa Mungu kwa wanadamu unatuhakikishia kwamba atatimiza ahadi hizo.—Yohana 3:16.

 Wengi waliokufa wakati huo na wale walioponyoka kifo waliendelea kulinda imani yao na kupata kusudi katika maisha kwa kuelewa kwa nini Mungu ameruhusu mambo mabaya na namna anavyokusudia kumaliza mambo hayo.