Ona video zinazopatikana

Ubatizo Maana Yake Nini?

Ubatizo Maana Yake Nini?

Jibu ya Biblia

 Ubatizo ni kuzamishwa ndani ya maji na kutoka. * Njo maana Yesu alibatizwa mu muto wenye ulikuwa na maji mingi. (Matayo 3:13, 16) Vilevile, mwanaume Mwetiopia aliomba abatizwe wakati alikaribia “mahali kwenye kuko maji.”​—Matendo 8:36-​40.

Ubatizo maana yake nini?

 Biblia inafananisha ubatizo na kuzikwa. (Waroma 6:4; Wakolosai 2:12) Wakati mutu anazamishwa katika maji, ni sawa vile anakufa kwa kuacha maisha yake ya zamani na kuanza sasa maisha ya mupya ya kujitoa kwa Mungu. Mungu anapatia mutu nafasi ya kuwa na zamiri safi yenye kutegemea imani katika zabihu ya Yesu Kristo. Juu mutu afikie kupata ile zamiri safi, anapaswa kufanya mambo yenye inaombwa juu astahili kubatizwa, na kisha anapaswa kubatizwa. (1 Petro 3:21) Njo maana Yesu alifundisha kama wanafunzi wake wanapaswa kubatizwa.​—Matayo 28:19, 20.

Ubatizo unamalizaka zambi ya mutu?

 Hapana. Biblia inafundisha kama ni damu ya Yesu tu njo inaweza kuondoa zambi zetu. (Waroma 5:8, 9; 1 Yohana 1:7) Lakini, juu damu ya Yesu iondoe zambi ya mutu, ule mutu anapaswa kumuamini Yesu, kubadilisha maisha yake juu ipatane na mafundisho ya Yesu, na kisha anapaswa kubatizwa.​—Matendo 2:38; 3:19.

Biblia inafundisha kama inaomba kubatiza watoto wadogo?

 Hapana, haifundishe vile. Hakuna kwenye Biblia inazungumuzia kubatiza watoto. Dini fulani zinabatizaka watoto kwa kuwamwangia maji kidogo ku kichwa na kuwapatia majina ya ubatizo. Ubatizo wa Kikristo ni wa watu wenye walishakomala wenye wanaweza kuelewa na kuamini “habari njema ya Ufalme wa Mungu.” (Matendo 8:12) Juu mutu abatizwe, anapaswa kusikia Neno ya Mungu, kuikubali, na kutubu. Mutoto mudogo hawezi kufanya ile mambo yote.​—Matendo 2:22, 38, 41.

 Zaidi ya ile, Biblia inaonyesha kama Mungu anaona watoto wa Wakristo kuwa watakatifu, ao safi, juu ya imani ya wazazi wao. (1 Wakorinto 7:14) Kama Mungu anakubali ubatizo wa watoto wadogo, hangewaona kuwa safi kwa sababu ya imani ya wazazi wao. *

Mawazo yenye haiko ya kweli juu ya ubatizo wa Kikristo

 Wazo yenye haiko ya kweli: Kumwangia mutu maji ku kichwa ni sawa tu na kumuzamisha mu maji.

 Kweli njo hii: Watu wote wenye walibatizwa wenye Biblia inazungumuzia walizamishwa ndani ya maji. Kwa mufano, wakati mwanafunzi Filipo alibatiza mwanaume Mwetiopia, wote wawili ‘waliingia ndani ya maji’ juu amubatize. Kisha, “walipanda kutoka katika maji.”​—Matendo 8:36-​39. *

 Wazo yenye haiko ya kweli: Wakati Biblia inasema kama watu wa nyumba muzima walibatizwa, ile inaonyesha kama na watoto walibatizwa. Kwa mufano, inasema hivi juu ya mulinzi fulani wa gereza katika Filipi: “Yeye na nyumba yake yote wakabatizwa.”​—Matendo 16:31-​34.

 Kweli njo hii: Habari ya Biblia yenye kuzungumuzia ule mulinzi wa gereza inaonyesha kama wale wenye walibatizwa walielewa “neno la Yehova” na ‘walifurahi sana.’ (Matendo 16:32, 34) Ile inaonyesha kama watoto wote wenye walikuwa mu nyumba ya ule mulinzi wa gereza hawangeweza kubatizwa, juu hawangeelewa neno ya Yehova.

 Wazo yenye haiko ya kweli: Yesu alifundisha kama watoto wadogo wanapaswa kubatizwa wakati alisema kama Ufalme wa Mungu ni wa watoto wadogo.​—Matayo 19:13-​15; Marko 10:13-​16.

 Kweli njo hii: Yesu hakukuwa nazungumuzia ubatizo wakati alisema ile maneno. Lakini, alikuwa naonyesha kama wale wenye wangestahili kuingia mu Ufalme wa Mungu wanapaswa kuwa kama watoto, ni kusema wanapaswa kuwa wapole na tayari kufundishwa.​—Matayo 18:4; Luka 18:16, 17.

^ Neno ya Kiebrania yenye kutafsiriwa “ubatizo” inatoka mu neno yenye kumaanisha “kuzamisha.” Ona Theological Dictionary of the New Testament, Buku ya I, ukurasa wa 529.

^ Kitabu The International Standard Bible Encyclopedia inasema kama “hakuna fasi kwenye Agano Jipya inazungumuzia ubatizo wa watoto wadogo.” Ile kitabu inasema tena kama ile tabia ilianza juu watu walikuwa na “mawazo yenye haifae kuhusu faida ya ubatizo.” Waliwaza kama ubatizo unaweza kumaliza zambi ya mutu.​—Buku ya 1, ukurasa wa 416-​417.

^ Chini ya kichwa “Ubatizo (mu Biblia),” kitabu New Catholic Encyclopedia inasema hivi: “Ni wazi kama Wakristo wa kwanza-kwanza walikuwa nazamisha mutu mu maji wakati wa ubatizo.”​—Buku ya 2, Ukurasa wa 59.