Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA

Mawazo Yako Ni ya Maana Sana!

Mawazo Yako Ni ya Maana Sana!

Kati ya mambo yenye kufuata, unafikiri ni jambo gani lenye linaweza kufanya sana ukuwe na furaha ao ukose furaha?

  • hali zako

  • chembe zako za uriti

  • mawazo yako

WATU fulani wanaweza kuchagua “hali,” pengine kwa kusema, “Ningekuwa na furaha . . .

  • “kama tu ningekuwa na feza nyingi”

  • “kama tu ningekuwa na ndoa ya muzuri”

  • “kama tu ningekuwa na afya ya muzuri”

Kwa kweli, mara nyingi furaha inategemea sana mawazo yetu kuliko hali zetu ao chembe zetu za uriti. Na hiyo ni habari ya muzuri. Sababu gani? Kwa sababu hata kama hauwezi kuzuia hali zako ao chembe zako za uriti, unaweza kuzuia mawazo yako.

‘DAWA YA MUZURI’

Mezali moja ya Biblia inasema hivi: ‘Moyo wenye shangwe ni dawa ya muzuri, lakini roho iliyopondeka inakausha mifupa.’ (Methali 17:22) Ni kusema kama mawazo yako ni ya maana sana! Mawazo yako yanaweza kufanya ufikie mupango wako ao uvunjike moyo, yanaweza kufanya tukio lenye kuhuzunisha likufanye ukuwe na sifa za muzuri ao za mubaya.

Watu fulani wanaweza kuwa na mashaka juu ya wazo hilo. Wanaweza kuwaza hivi:

  • ‘Sababu gani nifiche magumu yangu kwa kuwa na mawazo ya muzuri?’

  • ‘Hata nikuwe na mawazo ya muzuri kadiri gani, hilo haliwezi kubadilisha hali yangu.’

  • ‘Ninapaswa kuona hali namna iko kabisa kuliko kuwazia-wazia mambo ya muzuri.’

Mawazo hayo yanaweza kuonekana kuwa yenye kufaa. Lakini kuko faida za kuwa na mawazo ya muzuri. Kwa mufano, fikiria hali zenye kufuata.

Mahali penye wanatumikia, Alex na Brian wanafanya kwa bidii kazi za kuachana. Kisha kuchunguza kazi zao, mukubwa wao wa kazi anaonyesha makosa makubwa katika kazi ya kila mumoja.

  • Alex: “Nilifanya yangu yote na nilipitisha wakati mwingi katika kazi hii, lakini sikuitimiza muzuri! Hakuna siku nitaweza kufanya muzuri kazi hii. Hata nijikaze namna gani sitaifanya vile inastahili. Sababu gani hata nijaribu?”

  • Brian: “Mukubwa wangu wa kazi alionyesha mambo fulani yenye alipenda kuhusu kazi yenye nilifanya, lakini nilifanya makosa fulani makubwa. Nimejifunza mambo fulani ya maana yenye yatanisaidia kufanya muzuri zaidi wakati mwengine.”

UNAWAZA NAMNA GANI?

  • Kisha miezi sita kuanzia leo, ni nani kati ya wanaume hao wawili atakuwa na uwezo zaidi, Alex ao Brian?

  • Kama ungekuwa mukubwa wa kazi, ni nani kati yao ungependa kupatia kazi ao aendelee kuwa mufanyakazi wako?

  • Wakati unavunjika moyo, unatenda kama nani kati ya wanaume hao wawili?

Andrea na Brittney, kila mumoja wao anahangaishwa na mawazo ya kujisikia kuwa peke yake. Kila mumoja wao ana namna yake ya kupiganisha hali hiyo.

  • Andrea anajifikiria zaidi yeye mwenyewe. Anakataa kufanya mambo kwa ajili ya wengine ikiwa wao hawamufanyie kwanza yeye. Anafikiri, ‘Sababu gani nipoteze wakati wangu ili kusaidia watu wenye hawatanipatia kitu?’

  • Brittney anafanya yake yote ili kuwa mutu mwema na kufanya mambo kwa ajili ya wengine, hata kama wanaweza kuonekana kuwa wenye shukrani ao hapana. Anaishi kulingana na Kanuni ya Muzuri Sana, ni kusema, kuwatendea wengine kama vile angependa wamutendee. (Luka 6:31) Brittney anaona kama kutendea wengine mema kunaleta baraka.

UNAWAZA NAMNA GANI?

  • Ni nani kati ya wanawake hao wawili ungependa akuwe rafiki yako?

  • Ni nani kati yao anaweza kujisikia kuwa mwenye furaha zaidi juu ya uhusiano wake pamoja na wengine?

  • Kama unajisikia kuwa peke yako, unatenda kama Andrea ao kama Brittney?

Pengine unajua watu wenye kuwa kama Brian na Brittney. Labda unaweza hata kujisikia kuwa uko kama wao. Kama ni vile, unaweza kuona kuwa mawazo ya muzuri ni ya maana sana katika maisha yako. Lakini, tuseme nini ikiwa uko kama Alex ao Andrea? Biblia inaweza kukusaidia ili ukuwe na mawazo ya muzuri zaidi juu ya magumu ya maisha. Chunguza njia tatu.

1 EPUKA KUWA NA MAWAZO YA MUBAYA

BIBLIA INASEMA HIVI: “Je, umejionyesha kuwa umevunjika moyo siku ya taabu? Nguvu zako zitakuwa chache [kidogo].”—Methali 24:10.

ANDIKO HILO LINAMAANISHA NINI? Kuwa na mawazo ya mubaya kutakufanya upoteze nguvu yenye uko nayo lazima ili kufanya hali yako ikuwe muzuri ao ili kuipiganisha.

MUFANO: Wakati Juliza alikuwa mutoto, hakukuwa na furaha katika maisha yake. Baba yake alikuwa mulevi, na familia yao ilikuwa masikini. Walikuwa wanahama-hama sana. Kwanza, Juliza alikuwa na mawazo ya mubaya juu ya hali yake. Lakini, mawazo yake yalibadilika. Ni nini kilimusaidia? Juliza anasema hivi: “Hata mbele wazazi wangu wamalize matatizo yao, Biblia ilinisaidia nikuwe na mawazo ya muzuri. Na mupaka leo, mambo Biblia inasema yananisaidia niendelee kuachana na mawazo ya mubaya. Leo, wakati ninaona watu wanafanya mambo ya kunichukiza, ninapima kuelewa sababu gani wanatenda hivyo.”

Kama vile Juliza alijionea, Biblia ni kitabu chenye kuwa na kanuni zenye hekima. Mashauri yake yanaweza kukusaidia upiganishe hali za mubaya. Kwa mufano, andiko la Waefeso 4:23 linasema hivi: ‘Munapaswa kufanywa upya katika nguvu zinazoendesha akili yenu.’

Kama vile andiko hilo linaonyesha, unaweza kubadilisha mawazo yako. Unaweza “kufanywa upya” katika akili yako. Lakini, kufanya badiliko hilo ni jambo la kuendelea.

2 KAZA AKILI JUU YA MAMBO YA MUZURI

BIBLIA INASEMA HIVI: ‘Siku zote za mwenye kuteseka ni mubaya, lakini mutu aliye muchangamufu moyoni ana karamu sikuzote.’—Methali 15:15.

ANDIKO HILO LINAMAANISHA NINI? Kama uko na mawazo ya mubaya juu ya mambo yote, utajisikia kuwa mwenye “kuteseka” na kila siku itaonekana kuwa ya ‘mubaya,’ ao ya huzuni. Lakini, kama unakaza akili yako juu ya mambo ya muzuri, utakuwa ‘muchangamufu moyoni’ na hata mwenye furaha. Uamuzi ni wako.

MUFANO: Kisha kupasuliwa mara nyingi ili kuondoa kivimba kwenye ubongo wake, Yanko alikuwa na matatizo ya kimwili kama vile kutembea, kusema, na mambo mengine. Yanko alivunjika moyo sana kwa miaka mingi, kwa sababu aliona kama mambo hayo yangemufanya akose kutimiza mipango yake. Kisha alibadilika. Namna gani? Anasema hivi: “Kuliko kukaza akili juu ya magumu yangu, nilijifunza kujaza akili yangu mawazo ya kutia moyo.”

Njia moja yenye Yanko anafanya vile ni kusoma maandiko ya Biblia. Anasema hivi: “Kufanya vile kunanisaidia niendelee kuwa na mawazo ya muzuri. Sijasahau mambo yenye nilikuwa mimepanga kufanya wakati unaokuja, lakini ninakaza akili juu ya mambo madogo-madogo yenye ninaweza kutimiza leo. Wakati mawazo ya kuvunja moyo yanaanza kuingia katika akili yangu, ninafikiri juu ya sababu nyingi zenye niko nazo za kuwa na furaha.”

Kama Yanko, unaweza kupinga mawazo yako ya mubaya na kuwa na mawazo ya muzuri. Kama unapambana na hali za mubaya, pengine magumu ya afya, kama vile Yanko, ujiulize hivi: ‘Hali yangu haina tumaini kabisa? Nimefikia mwisho kabisa, ao jambo hili ni kizuizi tu?’ Jifunze kuzuia mawazo ya mubaya kwa kukaza akili juu ya jambo fulani lenye kujenga.

3 FANYA MAMBO KWA AJILI YA WENGINE

BIBLIA INASEMA HIVI: “Kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” —Matendo 20:35.

ANDIKO HILO LINAMAANISHA NINI? Mutu mwenye kutoa bila uchoyo anasikia furaha nyingi. Sababu gani? Kwa sababu tuliumbwa ili kufanya mambo mengi kuliko tu kuhangaikia yenye tuko nayo lazima. (Wafilipi 2:3, 4; 1 Yohana 4:11) Furaha ya kutoa inaweza kutusaidia sana kupiganisha hali ngumu katika maisha.

MUFANO: Josué anateswa na spina bifida, ni kusema, tatizo kubwa la mufupa wa katikati ya mugongo. Mara nyingi anasikia maumivu makali sana. Lakini Josué ana maisha ya furaha kwa sababu anasaidia wengine. Anasema hivi: “Kuliko kusema, ‘siwezi kufanya jambo hilo,’ ninawaza juu ya namna za kusaidia wengine katika mambo yenye wako nayo lazima kila siku. Ninapata njia za kufanya mambo kwa ajili ya wengine, na hilo linaniletea furaha katika maisha.”

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Tafuta nafasi za kujitoa kwa ajili ya wengine. Kwa mufano, unaweza kutayarisha chakula kwa ajili ya jirani mwenye kuwa mugonjwa? Unajua watu wenye kuzeeka wenye kuwa na lazima ya mutu wa kuwasaidia kufanya kazi mbalimbali katika nyumba zao?

Hangaikia mawazo yako kama vile unaweza kuhangaikia shamba. Ondoa mimea ya mubaya, ni kusema, mawazo ya mubaya. Panda mbegu za muzuri, ni kusema, mawazo ya muzuri na tia mbolea yenye kuleta mawazo hayo. Utavuna hali ya muzuri yenye itafanya maisha yako yakuwe yenye furaha zaidi. Na jambo hilo litahakikisha kama mawazo ya muzuri ni ya maana sana!

Kuko watu wenye wanakataa kula vyakula fulani kwa sababu ya afya yao, wewe pia unaweza kukataa mawazo ya mubaya.