Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KITULIZO KWA WALE WENYE KUWA NA MUKAZO

Namna ya Kupambana na Mukazo

Namna ya Kupambana na Mukazo

Juu uweze kupambana muzuri na mukazo unapaswa kufikiria afya yako ya kimwili, namna yako ya kuishi na wengine, miradi yako, na mambo yenye unatia pa nafasi ya kwanza katika maisha yako, ni kusema, mambo yenye unaona kuwa ya maana sana. Habari hii itazungumuzia kanuni fulani zenye kufaa zenye zinaweza kukusaidia upambane muzuri na mukazo na pengine hata kuupunguza.

Hangaikia Tu Mambo ya Leo

“Musihangaike hata kidogo juu ya kesho, kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe.”​—MATAYO 6:34.

Ile inamaanisha nini? Mahangaiko ya kila siku ni sehemu ya maisha yetu. Lakini usifanye mahangaiko ya leo ikuwe mingi kwa kuichanga na ya kesho. Ujikaze kuhangaikia tu mambo ya leo.

  • Mukazo unaweza kuleta mahangaiko. Kwa hiyo, jaribu kufanya hivi: Kwanza, uelewe kama ni kawaida kuwa na mukazo kwa kiasi fulani. Kuwa na wasiwasi juu ya mambo yenye hauwezi kuzuia kutafanya ukuwe na mukazo zaidi. Pili, uelewe kama mara mingi mambo yenye inafanya tuhangaike haitendeke kama vile tulikuwa tunawazia.

Ukuwe Mwenye Usawaziko

“Hekima yenye inatoka juu . . . ni . . . yenye usawaziko.”​—YAKOBO 3:17.

Ile inamaanisha nini? Usitafute ukamilifu. Epuka kujiwekea ao kuwekea wengine sheria zenye kupita mipaka.

  • Ukuwe mwenye kiasi, uweke sheria zenye kuwa na usawaziko, na utambue mipaka yako na ya watu wengine. Wakati unafanya vile, utapunguza mukazo wako na wa watu wengine na ile itafanya mupate matokeo ya muzuri. Pia, ukuwe unacheka ao kuchekesha. Kucheka hata wakati mambo haiende muzuri, kunatuliza mukazo na kunafanya ujisikie muzuri.

Ujue Mambo Yenye Inakuletea Mukazo

“Mutu mwenye utambuzi atabakia mutulivu.”​—MEZALI 17:27.

Ile inamaanisha nini? Kuwa na hisia za mubaya kunaweza kufanya mutu ashindwe kuwaza muzuri, kwa hiyo ujikaze kuwa mutulivu.

  • Tafuta kujua mambo yenye inakuletea mukazo, na namna unatenda mbele ya mukazo. Kwa mufano, wakati uko na mukazo, tambua mawazo, hisia, na tabia zenye unakuwa nazo ile wakati; pengine hata unaweza kuandika mambo hayo. Wakati unatambua namna unatenda mbele ya mukazo, ile inaweza kukusaidia upambane muzuri zaidi na mukazo. Pia, ufikirie njia mbalimbali za kumaliza mambo yenye inafanya ukuwe na mukazo. Kama haiwezekane kufanya vile, tafuta njia za kupunguza matokeo ya mubaya yenye ile mambo inaweza kukuletea, pengine kwa kupanga kazi na wakati wako muzuri zaidi.

  • Uone mambo mu njia mbalimbali. Pengine jambo lenye linakuletea mukazo, halitaletea mutu mwingine mukazo. Ile inategemea namna unaona mambo. Fikiria mapendekezo tatu yenye kufuata:

    1. Usikuwe haraka kuwazia mutu mwingine mubaya. Mutu fulani anaweza kupenda apite mbele yako wakati munangojea jambo fulani. Ikiwa unafikiri kama anajiendesha mubaya, ile inaweza kukufanya ukasirike. Kuliko kufanya vile, juu ya nini usikubali kama hakuwa na nia ya mubaya? Pengine ni vile!

    2. Ukuwe na mawazo ya muzuri kuhusu hali fulani. Ikiwa unangojea munganga ao ndege kwa wakati murefu, unaweza kuvumilia ikiwa unatumia ile wakati ili kusoma ao kufanya kazi fulani ao kutumiana ujumbe ku Enternete.

    3. Fikiria tatizo lako kwa ujumla. Ujiulize hivi, ‘Tatizo hili litakuwa kubwa kesho ao juma kesho?’ Utofautishe matatizo yenye haiko ya nguvu na matatizo ya nguvu.

Upange Mambo Muzuri

“Mambo yote yatendeke kwa adabu na kwa utaratibu.”​—1 WAKORINTO 14:40.

Ile inamaanisha nini? Ukuwe mwenye kupanga mambo muzuri katika maisha yako.

  • Tunapendaka kupanga mambo muzuri kwa kiasi fulani mu maisha. Jambo moja lenye linaweza kufanya mutu akose utaratibu na akuwe na mukazo ni tabia ya kuchelewesha mambo, na ile inaweza kufanya mutu akuwe na kazi mingi zenye haziishe. Jaribu kutumia mapendekezo mbili yenye kufuata:

    1. Ukuwe na programu yenye kufaa na uiheshimie.

    2. Tambua na uachane na kila mwelekeo wenye unakufanya ucheleweshe mambo.

Ukuwe na Maisha Yenye Usawaziko

“Mukono mumoja wa pumuziko ni muzuri zaidi kuliko mikono mbili ya kazi ya nguvu na kufuatilia upepo.”​—MUHUBIRI 4:6.

Ile inamaanisha nini? Watu wenye kupenda kazi kupita kiasi wanaweza kujiima faida ya “mikono [yao] mbili ya kazi ya nguvu.” Kisha kazi wanaweza kujikuta hawana tena wakati ao nguvu ya kufurahia matokeo ya kazi yao.

  • Ukuwe na mawazo yenye kufaa kuhusu kazi na feza. Kuwa na feza mingi hakumaanishe kupata furaha zaidi ao kukosa mukazo. Kwa kweli, kunaweza njo kupoteza furaha na kuleta mukazo. Muhubiri 5:12 inasema: “Vitu vingi vyenye tajiri iko navyo havimuruhusu alale.” Kwa hiyo, ujikaze kuishi kulingana na mapato yako.

  • Upange wakati wa kujifurahisha. Unatuliza mukazo wakati unafanya mambo yenye unafurahiaka. Lakini, kujifurahisha na uko mwenye kukaa tu, kama vile kuangalia TV, hakuwezi kusaidia.

  • Acha teknolojia pa nafasi yake. Epuka kuangalia ao kusoma kila mara ujumbe wenye walikutumia ku telefone ao ku adresi yako ya Enternete ao habari zenye kuwa ku site za Enternete za kupashana habari. Kama haiko lazima, epuka kusoma kisha saa za kazi ujumbe wenye kupatana na kazi wenye walikutumia ku Enternete.

Uhangaikie Afya Yako

“Mazoezi ya mwili ni yenye faida.” ​—1 TIMOTEO 4:8.

Ile inamaanisha nini? Kufanya mazoezi kwa ukawaida kunasaidia kuwa na afya ya muzuri.

  • Ukomalishe tabia zenye kuwa muzuri kwa afya. Mazoezi ya mwili inaweza kukusaidia ujisikie muzuri na inaweza kusaidia mwili wako utende muzuri zaidi mbele ya mukazo. Kula chakula chenye kujenga mwili, na ujikaze kuepuka tabia ya kujiima chakula. Uhakikishe kama unalala saa za kuenea.

  • Epuka kutumia “njia” za mubaya ili kumaliza mukazo, kama vile kuvuta tumbako ao kutumia dawa za kulewesha na kunywa pombe kupita mipaka. Kisha siku mingi, njia hizo zitafanya ukuwe na mukazo zaidi, pengine kwa kufanya upatwe na magonjwa na kukupotezea feza zenye ulipata kwa jasho.

  • Uonane na munganga wako kama mukazo unafikia kukulemea. Usisikie haya kumuomba musaada.

Panga Mambo ya Kutia pa Nafasi ya Kwanza

“Muhakikishe mambo ya maana zaidi.”​—WAFILIPI 1:10.

Ile inamaanisha nini? Ufikirie kwa uangalifu mambo yenye unatia pa nafasi ya kwanza.

  • Fanya liste ya mambo ya kufanya kwa kuanza na ya maana zaidi. Ile itakusaidia kufikiria kazi za maana zaidi, na itakusaidia kujua ni kazi gani zenye unaweza kufanya saa ingine, kazi zenye unaweza kupatia mutu mwingine ao hata zenye unaweza kuacha.

  • Kwa muda wa juma moja, uandike namna unatumia wakati wako. Kisha fikiria namna unaweza kutumia muzuri zaidi wakati wako. Kadiri unatumia muzuri wakati wako, ni vile utapunguza mukazo.

  • Panga wakati fulani wa kupumuzika. Hata kupumuzika wakati kidogo kunaweza kukusaidia upate tena nguvu na upunguze mukazo wako.

Tafuta Musaada

“Mahangaiko katika moyo wa mutu yanalemea moyo, lakini neno la muzuri linauchangamusha.”​—MEZALI 12:25.

Ile inamaanisha nini? Maneno yenye upole na huruma yenye wengine wanakuambia inaweza kukusaidia ujisikie muzuri.

  • Uzungumuze na mutu mwenye anaweza kukuelewa. Mutu mwenye unatumainia anaweza kukusaidia uone mambo mu njia tofauti ao hata kukusaidia umalize tatizo kwa kutumia njia yenye haukuwazia. Na hata kumuelezea tu magumu yako kunaweza kukusaidia ujisikie muzuri.

  • Omba musaada. Unaweza kuomba mutu mwingine afanye kazi fulani ao kuomba wengine wakusaidie kufanya kazi mbalimbali?

  • Kama mufanyakazi mwenzako anakuletea mukazo, tafuta njia za kufanya hali ikuwe muzuri. Kwa mufano, unaweza kumuambia kwa busara na kwa upole namna anakufanya ujisikie? (Mezali 17:27) Kama kufanya vile hakusaidie, unaweza kupunguza wakati wenye unapitisha pamoja naye?

Uhangaikie Uhitaji Wako wa kiroho

“Wenye furaha ni wale wenye wanatambua uhitaji wao wa kiroho.”​—MATAYO 5:3.

Ile inamaanisha nini? Sisi wanadamu, hatuhitaji tu chakula, nguo, na nafasi ya kuishi. Tuko na uhitaji wa kiroho. Ili tukuwe na furaha, tunapaswa kutambua uhitaji huo na kuutimiza.

  • Sala inaweza kusaidia sana. Mungu anakuomba ‘umutupie mahangaiko yako yote, kwa sababu yeye anakuhangaikia.’ (1 Petro 5:7) Kusali na kufikiri sana juu ya mambo yenye inajenga kunaweza kukusaidia upate amani ya moyoni.​—Wafilipi 4:6, 7.

  • Usome mambo yenye itakusaidia umukaribie Mungu zaidi. Kanuni zenye kuzungumuziwa katika gazeti hili zinatoka katika Biblia, yenye iliandikwa ili kutimiza uhitaji wetu wa kiroho. Kanuni hizo zinaweza pia kukusaidia ukuwe na “hekima yenye kutenda na uwezo wa kufikiri.” (Mezali 3:21) Juu ya nini usijiwekee muradi wa kusoma Biblia? Inaweza kuwa muzuri kuanza na kitabu cha Mezali.