Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

KITU HIKI KILIJIFANYA CHENYEWE?

Taa ya Kidudu Anayetoa Mwangaza

Taa ya Kidudu Anayetoa Mwangaza

TAA, ao sehemu ya mwili, ya Kimulimuli, kidudu anayetoa mwangaza, inafunikwa na magamba membamba yanayoongeza nuru ya mwangaza ambao kidudu huyo anatokeza. *

Fikiria hili: Wachunguzi wamevumbua kwamba magamba membamba yanayofunika taa ya aina fulani ya vidudu hao yanaingiana-ingiana, kama vile magamba ya samaki. Magamba yanainuka upande moja kwa mikrometa 3, ni kusema, nafasi kati ya magamba mawili ni ndogo mara 20 kuliko unene wa unywele wa mwanadamu. Hata hivyo, muinuko huo mudogo unafanya taa ya kidudu huyo iangaze zaidi ya mara 50 juu ya 100 kuliko vile ingeangaza ikiwa magamba hayangekuwa na muinuko!

Je, wazo hilo linaweza kusaidia kutengeneza taa za umeme zenye kutoa mwangaza vizuri zaidi ambazo zinatumiwa ndani ya vyombo vya kielektroniki? Wanasayansi walitengeneza taa za umeme na wakazifunika na kitu kilicho kama magamba ya taa ya kimulimuli. Kulikuwa na matokeo gani? Taa hiyo iliwaka na kutoa mwangaza mara 55 juu ya 100 zaidi kuliko kawaida! Annick Bay, mwanasayansi wa fizikia anasema hivi: “Jambo la maana zaidi kuhusu kazi hii ni kwamba tunaweza kujifunza mambo mengi kwa kuchunguza uumbaji kwa uangalifu.”

Unawaza namna gani? Taa ya vidudu hao wanaotoa mwangaza ilijifanya yenyewe? Ao je, iliumbwa?

^ Wanasayansi hawajajifunza aina zote za kidudu huyo anayetoa mwangaza.