Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mambo Hayo Uwapatie Wanaume Waaminifu

Mambo Hayo Uwapatie Wanaume Waaminifu

‘Mambo hayo uwakabizi [uwapatie] watu waaminifu, ambao nao watakuwa na sifa za kustahili vya kutosha kufundisha wengine.’2 TIMOTHEO 2:2.

NYIMBO: 123, 53

1, 2. Namna gani watu wengi wanaona kazi yao?

WATU wengi wanajiona kuwa wa maana ao hawana maana kulingana na kazi yenye wanafanya. Katika desturi fulani, wakati unapenda kujua mutu fulani, ni jambo la kawaida kumuuliza hivi: “Unafanya kazi gani?”

2 Wakati fulani Biblia inazungumuzia watu kwa kuonyesha kazi yenye walikuwa wanafanya. Kwa mufano, inazungumuzia ‘Mathayo mukusanya-kodi,’ ‘Simoni, mutengenezaji wa ngozi,’ na ‘Luka tabibu [munganga] mupendwa.’ (Mathayo 10:3; Matendo 10:6; Wakolosai 4:14) Wakati mwingine, Biblia inazungumuzia migawo yenye watu walikuwa nayo katika kazi ya Yehova. Fikiria Mufalme Daudi, nabii Eliya, na mutume Paulo. Wanaume hao waliona migawo yenye Yehova aliwapatia kuwa ya maana sana. Kama watu hao, sisi pia tunapaswa kuona mugawo wowote wenye Yehova anatupatia katika kazi yake kuwa wa maana sana.

3. Sababu gani wale wenye kuzeeka wanapaswa kuzoeza vijana? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.)

3 Tunapenda kumutumikia Yehova na tunaona migawo yetu kuwa ya maana sana. Wengi kati yetu tunafurahia sana kazi yetu; ndiyo sababu tunapenda kuendelea kufanya kazi hiyo kadiri inawezekana. Lakini, jambo la kuhuzunisha ni kwamba, wakati watu wanazeeka, hawawezi tena kufanya mambo yote yenye walizoea kufanya wakati walikuwa vijana. (Mhubiri 1:4) Hilo linaleta magumu ya pekee kwa watu wa Yehova. Leo, kazi ya kuhubiri inaendelea kuongezeka, na tengenezo la Yehova linaendelea kutumikisha teknolojia ya sasa ili habari njema ifikie watu wengi zaidi. Lakini wakati fulani inaweza kuwa vigumu kwa wale wenye kuzeeka kujifunza namna ya kutumikisha njia za mupya. (Luka 5:39) Pia, ni jambo la kawaida watu wapungukiwe na nguvu na uwezo wao wakati wanaendelea kuzeeka. (Methali 20:29) Kwa hiyo, ni jambo lenye kuonyesha upendo na lenye kufaa wakati wale wenye kuzeeka wanazoeza vijana ili wapate madaraka zaidi katika tengenezo la Yehova.—Soma Zaburi 71:18.

4. Sababu gani ni vigumu kwa watu fulani kuachia wengine madaraka? (Soma kisanduku “Sababu Gani Tunaweza Kuona Kuwa ni Vigumu Kuachia Wengine Madaraka?”)

4 Haiko vyepesi sikuzote kwa wale wenye kuwa na madaraka kuachia vijana wanaume madaraka yenye walikuwa nayo. Inaweza kufanya ndugu wahuzunike wakati wanafikiri kuwa watapoteza mugawo wenye wanapenda sana. Inaweza kuwaumiza wakati wanafikiria kuacha kazi fulani ya pekee yenye walikuwa wanafurahia kufanya. Ao wanaweza kuogopa kwamba ikiwa hawaongoze tena kazi hiyo, haitafanywa muzuri. Pengine wanafikiri kuwa hawana wakati wa kuzoeza wengine. Wakati huohuo, ni lazima vijana wanaume wakuwe na uvumilivu wakati hawapewe madaraka zaidi.

5. Tutazungumuzia maulizo gani katika habari hii?

5 Kwa hiyo, sababu gani ni jambo la maana wale wenye kuzeeka wasaidie vijana wapate madaraka zaidi? Namna gani wanaweza kufanya hivyo? (2 Timotheo 2:2) Na sababu gani vijana wanapaswa kuwa na mawazo ya muzuri wakati wanatumika pamoja na ndugu wenye kuzeeka, ndugu wenye kuwa na uzoefu zaidi na kuacha ndugu hao wawafundishe mambo fulani? Tuone kwanza namna Mufalme Daudi alitayarisha mutoto wake kwa ajili ya kazi ya maana sana.

DAUDI ALIMUTAYARISHA SULEMANI

6. Mufalme Daudi alipenda kufanya nini? Yehova alimuambia nini?

6 Kwa miaka mingi, Daudi aliteswa na alipaswa kuhama-hama. Kisha kuwa mufalme, aliishi katika nyumba ya muzuri sana. Kwa hiyo, alimuambia nabii Nathani hivi: “Tazama, mimi ninakaa katika nyumba ya mierezi, lakini sanduku la agano la Yehova linakaa ndani ya vitambaa vya mahema.” Daudi alipenda sana kumujengea Yehova hekalu la muzuri zaidi. Nathani alimuambia hivi: “Kila jambo lililo moyoni mwako lifanye, kwa kuwa Mungu wa kweli yupo pamoja nawe.” Lakini, hayo hayakukuwa mapenzi ya Yehova. Alimutuma Nathani amuambie Daudi hivi: “Si wewe utakayenijengea mimi nyumba ya kukaa.” Hata kama Yehova alimuahidi Daudi kama angekuwa pamoja naye sikuzote, Daudi alijulishwa kuwa mumoja kati ya watoto wake ndiye angejenga hekalu. Daudi alitenda namna gani?—1 Mambo ya Nyakati 17:1-4, 8, 11, 12; 29:1.

7. Daudi alitenda namna gani kulingana na muongozo wa Yehova?

7 Daudi alipenda kabisa kumujengea Yehova hekalu, kwa hiyo alipaswa kuvunjika moyo sana. Lakini aliendelea kutegemeza kabisa kazi hiyo yenye mutoto wake Sulemani angeongoza. Daudi alisaidia kupanga wafanyakazi na kukusanya chuma, shaba, feza, zahabu, na miti. Jambo la kujua ni nani mwenye angepewa sifa kwa sababu ya kujenga hekalu hilo lenye lilifikia kuitwa hekalu la Sulemani, halikumuhangaisha. Lakini, alimutia Sulemani moyo kwa kumuambia hivi: ‘Sasa, mwanangu, Yehova na akuwe pamoja nawe, nawe upate mafanikio, ujenge nyumba ya Yehova, Mungu wako, kama alivyosema kukuhusu wewe.’—1 Mambo ya Nyakati 22:11, 14-16.

8. Sababu gani Daudi angefikiri kuwa Sulemani hataweza kujenga hekalu? Lakini Daudi alifanya nini?

8 Soma 1 Mambo ya Nyakati 22:5. Daudi angeweza kuona kuwa Sulemani hakukuwa tayari kuongoza kazi hiyo ya maana. Hekalu lilipaswa kuwa ‘lenye utukufu zaidi,’ na Sulemani alikuwa ‘muchanga [mudogo] na mwororo [mwenye hana uzoefu].’ Lakini Daudi alijua kama Yehova angemusaidia Sulemani afanye kazi hiyo ya pekee. Kwa hiyo, Daudi alifanya yote yenye aliweza ili kumusaidia kutayarisha kazi hiyo kubwa zaidi.

UFURAHIE KUZOEZA WENGINE

Tunafurahi wakati tunaona vijana wanatimiza madaraka zaidi (Picha hii inapatana na fungu la 9)

9. Namna gani wale wenye kuzeeka wanaweza kuwa na furaha ya kupatia wengine madaraka? Toa mufano.

9 Ndugu wenye kuzeeka hawapaswe kuvunjika moyo wakati inakuwa lazima wapatie vijana madaraka fulani. Tunajua sisi wote kama jambo la maana zaidi leo, ni kazi ya Yehova. Kuzoeza vijana wanaume watimize madaraka kutasaidia kazi hiyo ifanywe. Fikiria jambo hili: Wakati ulikuwa mutoto mudogo, pengine ulikuwa unaona namna baba yako anatembeza motokari yake. Wakati uliendelea kukomaa, alikufasiria namna alikuwa anatembeza motokari hiyo. Kisha, ulipata kikaratasi cha kukuruhusu kutembeza motokari hiyo wewe mwenyewe. Hata kisha kuanza kutembeza, baba yako aliendelea kukupatia mashauri. Wakati fulani mulikuwa munaachiana kutembeza. Lakini, wakati baba yako alizeeka, mara nyingi ni wewe ndiye ulitembeza motokari hiyo. Baba yako alikasirika? Hapana, inawezakana alifurahi kukuona unatembeza. Vilevile, ndugu wenye kuzeeka wanafurahi kuona vijana wanaume wenye wamezoeza wanakuwa tayari kutimiza madaraka zaidi katika tengenezo la Yehova.

10. Musa alikuwa na mawazo gani juu ya kupewa utukufu na kuwa na madaraka?

10 Tunapaswa kuwa waangalifu ili tusionee wivu migawo ya wengine. Namna Musa alitenda wakati Waisraeli fulani walianza kutenda kama manabii inaweza kutufundisha jambo fulani. (Soma Hesabu 11:24-29.) Yoshua alipenda kuwakataza, lakini Musa alisema hivi: “Je, unaona wivu kwa ajili yangu? Hapana, laiti watu wote wa Yehova wangekuwa manabii, kwa sababu Yehova angeiweka roho yake juu yao!” Musa alijua kama Yehova alikuwa anaongoza kazi hiyo. Kuliko kujitafutia utukufu, Musa alipenda watumishi wote wa Yehova wapate migawo. Halafu sisi? Tunafurahi wakati wengine wanapewa migawo katika kazi ya Yehova?

11. Ndugu mumoja alisema nini juu ya kupatia wengine madaraka?

11 Kuko ndugu wengi wenye wametumika sana katika kazi ya Yehova kwa miaka mingi na wamezoeza vijana watimize madaraka zaidi. Kwa mufano, tuzungumuzie ndugu mumoja mwenye kuitwa Peter. Katika miaka 74 yenye amefanya katika utumishi wa wakati wote, alitumika miaka 35 kwenye biro moja ya tawi katika Ulaya. Alikuwa mwangalizi wa Biro ya Utumishi kwa miaka mingi. Kisha kijana mumoja mwenye kuitwa Paul ambaye Peter alikuwa amezoeza, alipewa mugawo huo. Peter alihuzunika kwa sababu ya mabadiliko hayo? Hapana. Alisema hivi: “Ninafurahi sana kuona kuwa kuko ndugu wenye wamezoezwa ili wakubali madaraka makubwa na kutimiza muzuri madaraka yao.”

ONA NDUGU WENYE KUZEEKA KUWA WA MAANA

12. Mufano wa Rehoboamu unaweza kutufundisha nini?

12 Wakati Rehoboamu, mutoto wa Sulemani alikuwa mufalme, aliomba wanaume wenye kuzeeka mashauri juu ya namna ya kutimiza mugawo wake mupya. Lakini kisha, alikataa mashauri yao na akafuata mashauri ya vijana wenye walikomaa pamoja naye. Matokeo yalikuwa ya mubaya sana. (2 Mambo ya Nyakati 10:6-11, 19) Mufano huo unaweza kutufundisha nini? Ni jambo la hekima kuomba mashauri kwa wale wenye kuzeeka na wenye kuwa na uzoefu mwingi zaidi kuliko sisi. Vijana hawapaswe kuona kuwa wanalazimika kuendelea kufanya mambo sawasawa kabisa kama vile yalikuwa yanafanywa zamani. Lakini, wanapaswa kuheshimia kwa moyo wote mawazo ya wale wenye kuzeeka na hawapaswe kuwa haraka kufikiri kama namna yao ya kufanya mambo haitaleta matokeo ya muzuri.

13. Namna gani vijana wanapaswa kutumika pamoja na ndugu wenye kuzeeka?

13 Wakati fulani, vijana wanapewa daraka la kusimamia kazi za ndugu wenye kuzeeka na wenye kuwa na uzoefu zaidi. Litakuwa jambo la hekima waache ndugu hao wenye kuzeeka wawafundishe mambo fulani. Katika mufano wenye tulizungumuzia hapo juu, kisha Paul kuchukua nafasi ya Peter ya kuwa mwangalizi wa biro fulani ya Beteli, alisema hivi, “Nilipanga wakati wa kutafuta mashauri kwa Peter, na nilitia moyo wengine katika biro hiyo wafanye hivyo.”

14. Namna Timotheo na mutume Paulo walitumika pamoja inaweza kutufundisha nini?

14 Timotheo alikuwa kijana sana kuliko mutume Paulo, lakini walitumika pamoja kwa miaka mingi. (Soma Wafilipi 2:20-22.) Mutume Paulo aliambia Wakorintho hivi: ‘Ninamutuma Timotheo kwenu, kwa kuwa yeye ni mutoto wangu mupendwa na muaminifu katika Bwana; naye atawakumbusha ninyi njia zangu kuhusiana na Kristo Yesu, kama vile ninavyofundisha kila mahali katika kila kutaniko.’ (1 Wakorintho 4:17) Hilo linatuonyesha wazi kama Paulo na Timotheo walitumika muzuri pamoja na walitegemezana. Mutume Paulo alichukua wakati wa kumufundisha Timotheo “njia [zake] kuhusiana na Kristo,” na Timotheo alijifunza muzuri njia hizo. Paulo alimupenda sana Timotheo na alikuwa hakika kama angehangaikia muzuri ndugu na dada wa kutaniko la Korintho. Wazee wanaweza kuiga mufano wa mutume Paulo wakati wanazoeza wanaume wengine ili waongoze kutaniko.

KILA MUMOJA WETU ANA DARAKA LA MAANA

15. Namna gani andiko la Waroma 12:3-5 linaweza kutusaidia wakati tunapatwa na mabadiliko?

15 Tunaishi wakati wa maana sana. Sehemu ya duniani ya tengenezo la Yehova inaendelea kukomaa katika njia mbalimbali. Hilo linamaanisha kama mambo yataendelea kubadilika. Mabadiliko fulani kati ya mabadiliko hayo yanatufikia kipekee na haiko vyepesi kupambana nayo. Yatatusaidia ikiwa tuko wanyenyekevu na kukaza akili juu ya faida za kazi ya Ufalme kuliko mambo yenye tunaweza kupenda sisi wenyewe. Wakati tunafanya hivyo, tunaendelea kuwa na umoja. Mutume Paulo aliandikia Wakristo wa Roma hivi: ‘Ninamuambia kila mutu hapo kati yenu asijifikirie mwenyewe zaidi kuliko ilivyo lazima kufikiri.’ Kisha alieleza kwamba kama vile tu kila sehemu ya mwili wetu iko na kazi yake, kila mutu katika kutaniko ana daraka lake.​—Waroma 12:3-5.

16. Kila Mukristo anaweza kufanya nini ili kuendeleza amani na umoja katika tengenezo la Yehova?

16 Watumishi wote wa Yehova wanapenda kutegemeza Ufalme na kufanya mambo yote yenye wanaombwa. Ndugu wenye kuzeeka wanaweza kuzoeza vijana. Ndugu vijana wanaweza kutimiza madaraka zaidi kwa unyenyekevu na heshima. Na ndugu wenye kuoa wanafurahi wakati bibi zao wanawategemeza hata wakati hali zao zinabadilika. Wanawake hao wanaweza kuiga mufano wa Prisila, mwenye alitumika kwa uaminifu pamoja na bwana yake Akila.​—Matendo 18:2.

17. Yesu alizoeza wanafunzi wake kufanya kazi gani?

17 Yesu alituachia mufano muzuri zaidi wa kuwa tayari kuzoeza wengine. Yesu alijua kama wengine wangeendelea kufanya kazi yake. Kwa kweli, alijua kama wanafunzi wake hawakukuwa wakamilifu. Lakini, alikuwa hakika kama wangetangaza habari njema katika maeneo ya mbali sana kuliko namna alifanya. (Yohana 14:12) Aliwazoeza muzuri, na waliweza kuhubiri katika kila inchi kwenye wangeweza kuenda.​—Wakolosai 1:23.

18. Tutakuwa na kazi gani wakati unaokuja? Tuko na kazi gani leo?

18 Kisha kifo cha Yesu, Yehova alimufufua na kumupatia kazi nyingi zaidi, na pia mamlaka ya “juu zaidi kuliko kila serikali na mamlaka na nguvu na utawala.” (Waefeso 1:19-21) Hata kama tunakufa waaminifu kwa Yehova mbele Har-Magedoni ifike, tutaishi tena na kuwa na kazi nyingi za muzuri katika dunia mupya. Na leo, sisi wote tuko na kazi yenye kupendeza ya kuhubiri habari njema na kufanya wanafunzi. Kwa hiyo, iwe tuko vijana ao wenye kuzeeka, kila mumoja wetu anaweza kuendelea ‘kuwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.’—1 Wakorintho 15:58.