Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Umekasirikia Mungu?

Umekasirikia Mungu?

“SABABU GANI MIMI? Sababu gani Mungu aliruhusu jambo hili linifikie?” Hayo ni maulizo yenye yalikuwa yanasumbua Sidnei wa inchi ya Brazili wakati alikuwa na miaka 24. Kisha kufanya aksidenti kwenye kitu cha kuteremukia ndani ya maji, amekuwa kilema mwenye kutumia kinga ya vilema.

Kuteseka kwa sababu ya aksidenti, ugonjwa, kifo cha mutu tulikuwa tunapenda, musiba wa asili, ao vita kunaweza kufanya watu wamukasirikie Mungu kwa vyepesi. Hali hiyo haikuanza leo. Ayubu, muzee wa zamani wa jamaa, alipatwa na taabu moja baada ya ingine. Alihukumu Mungu kimakosa hivi: ‘Ninakulilia nipate musaada, lakini wewe haunijibu; nimesimama, ili unikazie fikira; unajibadili ili ukuwe mukatili kwangu; unadumisha uadui kwangu kwa nguvu kamili za mukono wako.’—Ayubu 30:20, 21.

Ayubu hakujua mateso yake yalitoka wapi, sababu gani yalimufikia ao sababu gani Mungu aliyaruhusu. Jambo la kufurahisha ni kwamba, Biblia inatusaidia kujua sababu gani mambo kama hayo yanatokea na namna tunapaswa kufanya wakati yanatokea.

MUNGU ALIPENDA WATU WATESEKE?

Biblia inatuambia hivi juu ya Mungu: ‘Kazi zake ni kamilifu, kwa maana njia zake zote ni haki. Mungu wa uaminifu, ambaye hana ukosefu wowote wa haki; Yeye ni muadilifu na munyoofu.’ (Kumbukumbu la Torati 32:4) Kama ni vile, ni jambo lenye kupatana na akili ao lenye kueleweka kusema kama Mungu ‘muadilifu na munyoofu’ anawatesa wanadamu ao anatumia misiba ili kuwapatia malipizi ao kuwasafisha?

Lakini, Biblia inatuambia hivi: ‘Mutu akiwa chini ya jaribu, yeye asiseme: Mungu ananijaribu. Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na mambo maovu wala yeye mwenyewe hamujaribu yeyote.’ (Yakobo 1:13) Kwa kweli, Biblia inatuambia kama Mungu alipatia wanadamu mwanzo muzuri. Alipatia wanadamu wa kwanza, Adamu na Eva, makao yenye kupendeza, mambo yote yenye walikuwa nayo lazima ili kuishi, na kazi ya muzuri ya kufanya. Mungu aliwaambia hivi: ‘Muzae, muwe wengi, mujaze dunia na kuitiisha.’ Kwa kweli, Adamu na Eva hawakukuwa na sababu yoyote ya kukasirikia Mungu.—Mwanzo 1:28.

Lakini leo, hali za maisha haziko za muzuri. Kwa miaka mingi, magumu ya wanadamu yamekuwa mengi. Kwa hiyo, maneno haya ni ya kweli: ‘Uumbaji wote unaendelea kuugua pamoja na kuwa katika maumivu pamoja mupaka sasa.’ (Waroma 8:22) Ni nini ilitokea?

SABABU GANI KUKO MATESO?

Ili tuelewe sababu gani kuko mateso, tunapaswa kukumbuka wakati yalianza. Kisha kuchochewa na malaika muasi mwenye alifikia kuitwa Shetani Ibilisi, Adamu na Eva walikataa kanuni za Mungu juu ya mema na mabaya, zenye kuonyeshwa na amri yenye iliwakataza kula matunda ya ‘muti wa ujuzi wa mema na mabaya.’ Ibilisi aliambia Eva kuwa hawatakufa ikiwa wanakosa kutii Mungu, kwa kusema hivyo, alishitaki Mungu kuwa ni muongo. Tena, Shetani alishitaki Mungu kuwa ananyima raia wake haki ya kujiamulia mema na mabaya. (Mwanzo 2:17; 3:1-6) Ni kama vile Shetani alisema wanadamu wangekuwa muzuri bila kutawaliwa na Mungu. Mambo hayo yote yalitokeza ulizo la maana sana: Mungu alistahili kutawala?

Ibilisi alitokeza shitaka lingine. Alishitaki wanadamu kuwa wanatumikia Mungu kwa sababu ya faida zao wenyewe. Juu ya Ayubu, mutu muaminifu, Ibilisi aliambia Mungu hivi: ‘Je, wewe hukuweka ukuta kumuzunguka yeye na kuzunguka nyumba yake na kuzunguka kila kitu alicho nacho pande zote? . . . Lakini, ili kuwe na badiliko, tafazali nyoosha mukono wako, uguse kila kitu alicho nacho, uone kama hatakulaani wewe mbele za uso wako.’ (Ayubu 1:10, 11) Hata kama maneno ya Shetani yalizungumuzia Ayubu, kile alimaanisha ni kwamba wanadamu wote wanatumikia Mungu kwa sababu ya faida zao wenyewe.

NAMNA MUNGU ANAMALIZA MASHITAKA HAYO

Ni njia gani ingekuwa ya muzuri zaidi ili kumaliza mashitaka hayo makubwa mara moja? Mungu mwenye hekima nyingi zaidi, alikuwa na njia ya muzuri zaidi ya kumaliza mashitaka hayo, njia hiyo haitufanye tumukasirikie. (Waroma 11:33) Aliamua kuacha wanadamu wajitawale wenyewe kwa muda fulani ili matokeo yaonyeshe ni utawala wa nani wenye kuwa mukubwa zaidi.

Hali mbaya zenye kuwa katika dunia leo zinaonyesha waziwazi kama utawala wa mwanadamu umeshindwa kabisa. Serikali za wanadamu hazina uwezo wa kuleta amani, usalama, na furaha na tena zimeharibisha dunia sana. Hilo linaonyesha kuwa maneno haya ya Biblia ni ya kweli kabisa: “Mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua yake.” (Yeremia 10:23) Utawala wa Mungu tu ndio unaweza kuletea wanadamu amani, furaha na maisha ya muzuri sikuzote kwa sababu hilo ni kusudi la Mungu.—Isaya 45:18.

Kwa hiyo, namna gani Mungu atatimiza kusudi lake juu ya wanadamu? Kumbuka kuwa Yesu alifundisha wanafunzi wake kusali hivi: ‘Ufalme wako uje. Mapenzi yako yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.’ (Mathayo 6:10) Kwa wakati unaofaa, kupitia Ufalme wake, Mungu ataondoa mambo yote yenye kuleta mateso. (Danieli 2:44) Umasikini, magonjwa, na kifo havitakuwa tena. Juu ya masikini, Biblia inasema kuwa Mungu ‘atamukomboa masikini anayelilia musaada.’ (Zaburi 72:12-14) Na juu ya wagonjwa, Biblia inatoa ahadi hii: ‘Hakuna mukaaji atakayesema: Mimi ni mugonjwa.’ (Isaya 33:24) Na hata juu ya watu waliokufa wenye kuwa katika kumbukumbu la Mungu, Yesu alisema hivi: “Saa inakuja ambayo wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake, na kutoka.” (Yohana 5:28, 29) Hizo ni ahadi zenye kuchangamusha moyo sana!

Kuwa na imani katika ahadi za Mungu kunatusaidia tuache kumukasirikia

NAMNA YA KUACHA KUKASIRIKIA MUNGU

Miaka 17 kisha Sidnei, mwenye tulitaja mwanzoni mwa habari hii kufanya aksidenti, alisema hivi: “Hata siku moja sikuhukumu Mungu juu ya aksidenti hiyo, lakini kusema kweli, mwanzoni nilimukasirikia. Kuko siku zenye ninasikia huzuni kabisa, na ninalia wakati ninafikiria ulemavu wangu. Lakini, kupitia Biblia nimeelewa kama aksidenti hiyo haikukuwa malipizi ya Mungu. Kama vile Biblia inasema, ‘wakati na tukio lisilotazamiwa vinatupata sote.’ Kusali kwa Yehova na kusoma maandiko fulani kumefanya nikuwe nguvu kiroho na niendelee kuwa na mawazo ya muzuri.”—Mhubiri 9:11; Zaburi 145:18; 2 Wakorintho 4:8, 9, 16.

Kufikiria juu ya sababu zenye zinafanya Mungu aruhusu mateso na namna atayamaliza hivi karibuni, kunatusaidia tuache kumukasirikia. Tuko hakika kuwa Mungu ni ‘musawabishaji wa wale wanaomutafuta kwa bidii.’ Mutu yeyote mwenye kuamini Mungu na Mwana wake hatavunjika moyo.—Waebrania 11:6; Waroma 10:11.