Yobu 1:1-22

  • Uaminifu-mushikamanifu na utajiri wa Yobu (1-5)

  • Shetani anatilia mashaka nia ya Yobu (6-12)

  • Yobu anapoteza mali na watoto wake (13-19)

  • Yobu hamulaumu Mungu (20-22)

1  Katika inchi ya Usi kulikuwa mutu mumoja mwenye jina lake lilikuwa Yobu.*+ Alikuwa mutu munyoofu na muaminifu-mushikamanifu;*+ alikuwa anamuogopa Mungu na kuepuka mambo ya mubaya.+  Alizaa watoto wanaume saba (7) na watoto wanamuke tatu (3).  Mifugo yake ilikuwa kondoo elfu saba (7 000), ngamia elfu tatu (3 000), ngombe elfu moja (1 000), punda mia tano (500), na alikuwa na watumishi wengi sana, kwa hiyo akakuwa mukubwa kuliko watu wote wa Mashariki.  Kila mumoja wa wana wake alikuwa anafanya karamu kwenye nyumba yake katika siku yake mwenyewe yenye ilipangwa.* Na walikuwa wanaalika dada zao watatu (3) ili kula na kunywa pamoja nao.  Wakati siku za karamu zilikuwa zinamalizika, Yobu alikuwa anawaita kusudi awatakase. Kwa hiyo alikuwa anaamuka asubui sana na kutoa zabihu za kuteketezwa+ kwa ajili ya kila mumoja wao. Kwa maana Yobu alikuwa anasema: “Pengine wana wangu wametenda zambi na kumutukana Mungu katika moyo wao.” Ni vile Yobu alikuwa anafanya sikuzote.+  Basi siku ikafika yenye wana wa Mungu* wa kweli+ waliingia ili kusimama mbele ya Yehova,+ na Shetani+ pia akaingia kati yao.+  Kisha Yehova akamuambia Shetani: “Unatoka wapi?” Shetani akamujibu Yehova: “Ninatoka kuzunguka-zunguka katika dunia na kutembea-tembea ndani yake.”+  Na Yehova akamuambia Shetani: “Je, umemuona* mutumishi wangu Yobu? Hakuna mutu kama yeye juu ya dunia. Yeye ni mutu munyoofu na muaminifu-mushikamanifu,*+ mwenye kumuogopa Mungu na kuepuka mambo ya mubaya.”  Kwa hiyo Shetani akamujibu Yehova: “Je, Yobu anamuogopa Mungu bure?+ 10  Je, haukutia ukuta wa ulinzi kumuzunguka yeye+ na nyumba yake na kila kitu chenye iko* nacho? Umebariki kazi ya mikono yake,+ na mifugo yake imeenea katika inchi yote. 11  Lakini, ili mambo yabadilike, unyooshe mukono wako na upige kila kitu chenye iko* nacho, na hakika atakulaani mbele ya uso wako.” 12  Basi Yehova akamuambia Shetani: “Angalia! Kila kitu chenye iko* nacho kiko katika mukono wako. Lakini tu usiweke mukono wako juu ya mutu huyo!” Kwa hiyo Shetani akatoka mbele ya* Yehova.+ 13  Sasa siku moja yenye watoto wake wanaume na watoto wake wanamuke walikuwa wanakula na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mukubwa,+ 14  mujumbe mumoja akakuja kwa Yobu na kusema: “Ngombe walikuwa wanalima na punda walikuwa wanakula majani pembeni yao 15  wakati Wasabea waliwashambulia na kuwakamata, na wakaua watumishi kwa upanga. Mimi tu ndiye niliponyoka ili kukuletea habari.” 16  Wakati alikuwa angali anasema, mwingine akakuja na kusema: “Moto kutoka kwa Mungu* ulianguka kutoka mbinguni na kuwaka kati ya kondoo na watumishi na kuwateketeza! Mimi tu ndiye niliponyoka ili kukuletea habari.” 17  Wakati alikuwa angali anasema, mwingine akakuja na kusema: “Wakaldayo+ walifanya vikundi tatu (3) na wakavamia ngamia na kuwakamata, na kuua watumishi kwa upanga. Mimi tu ndiye niliponyoka ili kukuletea habari.” 18  Wakati alikuwa angali anasema, mwingine tena akakuja na kusema: “Watoto wako wanaume na watoto wako wanamuke walikuwa wanakula na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mukubwa. 19  Upepo mukali ukakuja kwa kushitukia kutoka katika jangwa, na ukapiga pembe ine (4) za nyumba, na nyumba hiyo ikaangukia vijana hao na wakakufa. Mimi tu ndiye niliponyoka ili kukuletea habari.” 20  Basi Yobu akasimama na kupasua nguo yake na akanyoa nywele za kichwa chake; kisha akaanguka chini na kuinama 21  na kusema: “Nilitoka katika tumbo la uzazi la mama yangu nikiwa uchi,Na nitarudia nikiwa uchi.+ Yehova ametoa,+ na Yehova amenyanganya. Jina la Yehova liendelee kusifiwa.” 22  Katika mambo haya yote, Yobu hakutenda zambi wala kumulaumu Mungu kwa jambo lolote la mubaya.*

Maelezo ya Chini

Ao “mutu mwenye hana lawama na munyoofu.”
Inawezekana jina hilo linamaanisha “Kitu Chenye Kuchukiwa.”
Ao “kwenye nyumba ya kila mumoja wao kwa zamu yake.”
Huu ni usemi wa Kiebrania wenye kumaaanisha wana wa Mungu ambao ni malaika.
Ao “mutu mwenye hana lawama na munyoofu.”
Tnn., “umeweka moyo wako juu ya.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Tnn., “mbele ya uso wa.”
Ao pengine, “Umeme wa radi.”
Ao “kusema kwamba Mungu amefanya jambo lolote la mubaya.”