Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 2

Uwe Mwaminifu-mushikamanifu kwa Mwenzako

Uwe Mwaminifu-mushikamanifu kwa Mwenzako

‘Kile ambacho Mungu ameunganisha mutu yeyote asikitenganishe.’​—Marko 10:9

Yehova anataka ‘tupende ushikamanifu.’ (Mika 6:8) Hilo ni jambo la maana zaidi sana katika ndoa yako, kwa sababu ikiwa bibi ao bwana yako haiko mushikamanifu ni vigumu kumutumainia. Na ni lazima kumutumainia mwenzako ili uendelee kumupenda.

Leo, ushikamanifu unakosekana katika ndoa nyingi. Ili muendelee kuwa washikamanifu katika ndoa yenu, ni lazima muazimie kufanya mambo mawili.

1 UHANGAIKIE NDOA YENU KWANZA

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Uhakikishe mambo yaliyo ya maana zaidi.’ (Wafilipi 1:10) Ndoa yenu ni moja kati ya mambo yaliyo ya maana sana katika maisha yako. Ni lazima uihangaikie kwanza.

Yehova anataka umuhangaikie sana bibi ao bwana yako na “kufurahia maisha” pamoja naye. (Mhubiri 9:9) Anaonyesha wazi kwamba haupaswi kumuzarau bibi ao bwana yako, lakini, kila mutu anapaswa kutafuta namna ya kumufurahisha mwenzake. (1 Wakorintho 10:24) Umufanye mwenzako ajisikie kuwa wa maana na mwenye kupendwa.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Mupitishe wakati pamoja kwa ukawaida, na umupatie mwenzako uangalifu wote

  • Uwe unafikiri kwa njia ya “sisi” kuliko “mimi”

2 ULINDE MOYO WAKO

MAMBO AMBAYO BIBLIA INASEMA: ‘Kila mutu ambaye anaendelea kumutazama mwanamuke na kumutamani tayari amefanya uzinzi pamoja naye moyoni mwake.’ (Mathayo 5:28) Ikiwa mutu anaendelea kuwaza juu ya mambo ya uasherati, kwa kadiri fulani, anakosa uaminifu kwa bibi ao bwana yake.

Yehova anasema kwamba ni lazima ‘ulinde moyo wako.’ (Methali 4:23; Yeremia 17:9) Ili kulinda moyo wako, ni lazima uzuie macho yako. (Mathayo 5:29, 30) Fuata mufano wa Ayubu, ambaye alifanya agano na macho yake ili asimutazame hata kidogo mwanamuke kwa kumutamani. (Ayubu 31:1) Epuka kabisa kutazama ponografia ao picha za ngono. Na uepuke kwa njia yoyote kufanya urafiki wa kimapenzi na mutu mwingine asiyekuwa bibi ao bwana yako.

MAMBO YA KUFANYA:

  • Acha wengine waone waziwazi kwamba unashikamana kabisa na bibi ao bwana yako

  • Fikiria mawazo ya moyoni ya mwenzako na ukate urafiki wowote ambao unaweza kumuchukiza bibi ao bwana yako