Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 2

Mungu Ni Nani?

Mungu Ni Nani?

1. Juu ya nini tunapaswa kumuabudu Mungu?

Mungu wa kweli njo Muumbaji wa vitu vyote. Hana mwanzo na hana mwisho. (Zaburi 90:2) Habari njema yenye kuwa mu Biblia inatoka kwake. (1 Timoteo 1:11) Tunapaswa kumuabudu yeye tu, juu yeye njo alitupatia uzima.​—Soma Ufunuo 4:11.

2. Mungu iko namna gani?

Hakuna mutu mwenye amekwisha kumuona Mungu juu Mungu ni Roho, ni kusema, uzima wake ni wa hali ya juu zaidi kuliko uzima wa viumbe vyenye kuishi ku dunia. (Yohana 1:18; 4:24) Lakini, tunaweza kuona sifa za Mungu kupitia vitu vyenye aliumba. Kwa mufano, wakati tunaona matunda na maua ya namna mbalimbali, tunajifunza kama Mungu ni mwenye upendo na ni mwenye hekima. Ukubwa wa ulimwengu wote muzima unatuonyesha nguvu za Mungu.​—Soma Waroma 1:20.

Wakati tunasoma Biblia, tunaweza kujifunza mambo mingi zaidi juu ya sifa za Mungu. Kwa mufano, Biblia inatuambia mambo yenye Mungu anapenda na mambo yenye anachukia, namna anatendea watu, na sifa zenye anaonyesha mu hali mbalimbali.​—Soma Zaburi 103:7-10.

3. Mungu iko na jina?

Yesu alisema hivi: “Baba yetu mwenye kuwa mbinguni, jina lako litakaswe.” (Matayo 6:9) Mungu iko na majina mingi ya cheo ao ya heshima, lakini iko na jina moja tu la pekee. Mu kila luga, watu wanasema jina hilo kwa njia tofauti ao ya kuachana. Mu Kiswahili, mara mingi watu wanalisema “Yehova.” Lakini watu fulani wanalisema “Yahweh.”​—Soma Zaburi 83:18.

Mu Biblia za mingi, wametosha jina la Mungu na nafasi ya jina hilo wametia majina ya cheo kama vile Bwana ao Mungu. Lakini wakati Biblia iliandikwa, jina la Mungu lilipatikana ndani mara 7 000 hivi. Yesu alijulisha watu jina la Mungu wakati alikuwa anawafundisha juu ya Mungu.​—Soma Yohana 17:26.

Angalia video Mungu Ana Jina?

4. Yehova anatuhangaikia?

Kama baba huyu mwenye upendo, Mungu anapenda tukuwe na hali ya muzuri milele

Kwa sababu watu wengi wanateseka, watu fulani wanawaza kama Yehova hatuhangaikie. Na wewe unawaza vile? Watu fulani wanasema kama Mungu anatuletea mateso ili kutujaribu, lakini ile haiko kweli.​—Soma Yakobo 1:13.

Mungu ametupatia uhuru wa kuchagua, hilo linaonyesha kama anatuona kuwa watu wa maana. Kwa mufano, tunafurahia uhuru wenye tuko nao wa kuchagua sisi wenyewe kumutumikia Mungu. (Yoshua 24:15) Lakini watu wengi wanachagua kutendea wengine mambo ya mubaya, kwa hiyo, mateso inaongezeka mu dunia. Yehova anahuzunika wakati anaona ukosefu wa haki wa namna hiyo.​—Soma Mwanzo 6:5, 6.

Yehova anatuhangaikia. Anataka tukuwe na furaha mu maisha. Hivi karibuni, atatosha mateso yote na watu wenye wanaleta ile mateso. Lakini leo, iko na sababu ya kuacha watu wateseke kwa wakati fulani. Mu Somo la 8, tutajifunza ile sababu.​—Soma 2 Petro 2:9; 3:7, 13.

5. Tunaweza kufanya nini ili kumukaribia Mungu?

Yehova anatuomba tumukaribie kwa kuzungumuza naye kupitia sala. Anapendezwa na kila mumoja wetu. (Zaburi 65:2; 145:18) Na iko tayari kutusamehe. Hata kama wakati fulani tunamukosea, Yehova anaona namna tunajikaza ili kumupendeza. Kwa hiyo, tunaweza kuwa na urafiki muzuri pamoja naye hata kama hatuko wakamilifu.​—Soma Zaburi 103:12-14; Yakobo 4:8.

Yehova ametupatia uzima, kwa hiyo, tunapaswa kumupenda sana kuliko mutu mwingine yeyote. (Marko 12:30) Wakati unaonyesha kama unamupenda Mungu kwa kujifunza mambo mingi juu yake na kufanya mambo yenye anakuomba, utamukaribia zaidi.​—Soma 1 Timoteo 2:4; 1 Yohana 5:3.