Vitu Vyenye Uzima Vilianza Namna Gani?​—Maulizo 5 ya Kujiuliza

Chunguza mambo yenye ushuhuda unaonyesha na uamue kama utaamini mageuzi ao uumbaji.

Mwanafunzi Hajue Aamini Nini

Mara mingi wanafunzi wenye wamefundishwa kama vitu vyenye uzima viliumbwa wanapaswa kuamua wataamini nini.

ULIZO YA 1

Vitu Vyenye Uzima Vilianza Namna Gani?

Jibu ya ile ulizo inaweza kubadilisha namna yako ya kuona mambo.

ULIZO YA 2

Kuko Kitu Yenye Uzima Yenye Tunaweza Kuona Kuwa ya Bure-bure?

Kama fundisho ya mageuzi ni ya kweli, inapaswa kuonyesha waziwazi namna chembe ya kwanza-kwanza ilijitokezaka yenyewe.

ULIZO YA 3

Maagizo Yote Yenye Kuwa mu ADN Ilitoka Wapi?

Wanabiolojia wamepitisha miaka mingi na wako wanajifunza namna tabia zinapitishwa kutoka kwa wazazi mupaka kwa watoto. Wamejifunza pia kuhusu maagizo yenye kuwa wazi yenye kupatikana mu molekile ya ajabu yenye kuitwa ADN.

ULIZO YA 4

Vitu Vyote Vyenye Uzima Vilitokana na Muzazi Mumoja?

Charles Darwin na wanasayansi wengine wa kisha yeye waliwazia kama aina zote za vitu vyenye uzima zilitoka kwa muzazi mumoja. Njo vile mambo ilikuwa kabisa?

ULIZO YA 5

Tunaweza Kuamini Mambo Yenye Biblia Inasema?

Mambo yenye watu wanasemaka juu ya Biblia inafanyaka watu fulani wawaze kama Biblia haipatane na akili, haipatane na sayansi, na iko na mafundisho mingi ya uongo. Inawezekana watu wameisemea uongo?

Vichapo Vyenye Vilitumiwa Juu ya Kutayarisha Hii Broshua

Hii sehemu iko na liste ya vichapo vyenye vilitumiwa ili kuandika mawazo ya hii broshua.