Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mwanafunzi Hajue Aamini Nini

Mwanafunzi Hajue Aamini Nini

Tony anavurugika. Mwalimu wake, mwanamuke mwenye anaheshimia, ametoka kuwafundisha juu ya Charles Darwin na fundisho yake ya mageuzi. Ameonyesha namna Charles Darwin alisaidia kuleta maendeleo mu mambo ya sayansi, na kusaidia watu waachane na mawazo ya uongo. Sasa anaomba wanafunzi wake waseme kama wanawaza nini juu ya ile jambo.

Tony hajue aamini nini. Wazazi wake wamemufundisha kama Mungu njo aliumba dunia na vitu vyote vyenye uzima. Wamemufundisha kama habari ya Biblia juu ya uumbaji ni ya kweli kabisa, na kama hakuna ushuhuda wenye kuonyesha kama vitu vyenye uzima vilitokana na mageuzi. Ikuwe mwalimu wake, ao wazazi wake, wote wanamuhangaikia. Tony aamini nani na aache nani?

Kila mwaka ile hali inafikiaka wanafunzi mu dunia yote. Tony na wanafunzi wengine wanapaswa kufanya nini? Hauone kama wanapaswa kuchunguza mambo na kujiamulia wao wenyewe? Wanapaswa kujiuliza hivi: Kama fundisho ya mageuzi ni ya kweli, nini njo inaonyesha vile? Kama fundisho ya uumbaji ni ya kweli, nini njo inaonyesha vile? Kisha kuchunguza ile mambo, wanaweza sasa kujiamulia ni fundisho gani wataamini.

Na hata Biblia inasema kama haiko muzuri kuamini-amini tu mambo yote yenye watu wanasemaka. Muandikaji mumoja wa Biblia anasema hivi: “Mujinga anaamini kila neno, lakini mwerevu anafikiria sana kila hatua.” (Mezali 14:15) Biblia inashauria Wakristo watumie ‘nguvu zao za kufikiri’ ili wajihakikishie wenyewe kama mambo yenye wanafundishwa ni ya kweli.​—Waroma 12:1, 2.

Kusudi ya hii broshua haiko kuunga mukono watu wa makanisa wenye wanasema wanafunzi wakuwe wanafundishwa kama vitu vyenye uzima viliumbwa. Lakini kusudi ya hii broshua ni kukusaidia uchunguze mawazo ya wale wenye wanafundisha kama vitu vyenye uzima vilijitokeza na wenye wanasema kama habari ya Biblia juu ya uumbaji ni hadisi ya kuwazia-wazia tu.

Tutazungumuzia sana chembe juu chembe njo sehemu ya musingi ya uzima. Utajifunza mambo ya kushangaza sana juu ya namna chembe zinafanyizwa. Tena utakuwa na nafasi ya kuchunguza mawazo yenye inaunga mukono mageuzi.

Siye wote tunapaswa kufikiria hii ulizo: Vitu vyenye uzima viliumbwa ao vilijitokeza? Pengine ulishakafikiria sana ile ulizo. Hii broshua inaonyesha sababu fulani zenye zinafanya watu wengi waamini kama vitu vyenye uzima viliumbwa.