Ona video zinazopatikana

Mashahidi wa Yehova Wanaamini Kama Mungu Aliumba Mbingu na Dunia kwa Siku Sita Zenye Urefu wa Saa 24?

Mashahidi wa Yehova Wanaamini Kama Mungu Aliumba Mbingu na Dunia kwa Siku Sita Zenye Urefu wa Saa 24?

 Hapana. Mashahidi wa Yehova wanaamini kama Mungu aliumba vitu vyote. Lakini, hawaamini kama Mungu aliumba mbingu na dunia kwa siku sita zenye urefu wa saa 24. Juu ya nini? Juu Biblia haiseme vile. Fikiria mifano mbili yenye kufuata:

  1.   Urefu wa zile siku sita za uumbaji. Watu fulani wanaamini kama siku sita za uumbaji zilikuwa na urefu wa saa 24. Lakini mu Biblia, neno “siku” inaweza kumaanisha wakati murefu sana.​—Mwanzo 2:4; Zaburi 90:4.

  2.   Miaka ya dunia. Watu fulani wanafundisha kama Dunia iko tu na maelfu kidogo ya miaka. Lakini, Biblia inafundisha kama mbingu na dunia vilikuwa mbele ya zile siku sita za uumbaji. (Mwanzo 1:1) Njo maana, Mashahidi wa Yehova wanakubali mawazo ya wanasayansi ya kama inawezekana dunia iko na mamiliare ya miaka hivi.

 Hata kama Mashahidi wa Yehova wanaamini kama Mungu njo aliumba vitu vyote, hawakatalake mambo yenye wanasayansi wanasemaka. Tunaamini kama mambo yenye sayansi ya kweli inasema inapatana na mambo yenye Biblia inasema.